Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w12 10/1 kur. 4-5
  • Kwa Nini Ufisadi Unazidi Kuongezeka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Ufisadi Unazidi Kuongezeka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Ufisadi Utakwisha!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Ahadi ya Ulimwengu Usio na Ufisadi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Sababu Gani Tunazeeka na Kufa?
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Mbona Kuna Ufisadi Mwingi Mno?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 10/1 kur. 4-5

Kwa Nini Ufisadi Unazidi Kuongezeka?

“Mwanadamu amemtawala mwanadamu kwa kumuumiza.”—MHUBIRI 8:9.

MANENO ya andiko hilo yanaonyesha kikamili historia ya utawala wa wanadamu. Utawala huo umesababisha kuteseka na huzuni nyingi. Kwa muda mrefu, jitihada za watu wenye nia nzuri ambao wamejaribu kutokeza jamii iliyo na haki, sikuzote zimezuiwa na tamaa na ufisadi. Kwa nini hali iko hivyo? Kwa nini ufisadi unazidi kuongezeka? Kwa ujumla, ni kwa sababu ya mambo matatu yafuatayo ambayo husababisha uvutano usiofaa.

1. Uvutano wa dhambi.

Biblia inataja waziwazi kwamba ‘sote tuko chini ya dhambi.’ (Waroma 3:9) Kama tu ugonjwa wa kurithiwa usioweza kutibiwa, dhambi ‘inakaa’ ndani yetu. Kwa maelfu ya miaka, dhambi ‘imewatawala’ wanadamu kama mfalme. “Sheria” yake imeendelea kufanya kazi ndani yetu. Mwelekeo wa kutenda dhambi umewafanya watu wengi watangulize mapendezi yao au kutafuta mali na mamlaka huku wakiwaumiza watu wengine.—Waroma 5:21; 7:17, 20, 23, 25.

2. Uvutano wa ulimwengu mwovu tunamoishi.

Ulimwengu wetu umejaa pupa na ubinafsi. Watu wengi wanaona kuwa ni vigumu kujiendesha kwa njia tofauti na watu wanaowazunguka. Wakisukumwa na ubinafsi wanakuwa wenye njaa ya kutaka mamlaka. Pia, wanakuza tamaa ya kupata pesa na mali kwa wingi hata kuliko wanavyohitaji. Jambo la kusikitisha ni kwamba wako tayari kujihusisha na ukosefu wa haki ili watimize malengo yao. Badala ya kukataa uvutano usiofaa, watu kama hao “[wanafuata] umati kwa ajili ya makusudio maovu.”​—Kutoka 23:2.

3. Uvutano wa Shetani Ibilisi.

Shetani, kiumbe mwasi wa kiroho, ‘anaipotosha dunia nzima inayokaliwa.’ (Ufunuo 12:9) Anafurahia kuwapotosha wanadamu. Kwa ujanja anaweza kumshawishi mtu atumie vibaya tamaa ya asili ya kutaka kuwa na vitu vya kimwili na pesa na hata kumfanya atende kwa udanganyifu.

Je, hilo linamaanisha sisi ni kama vikaragosi ambavyo vinaongozwa na Shetani, yaani, tunapaswa kutii kila jambo analotuamuru? Tutapata jibu katika makala inayofuata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki