Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 6/1 uku. 16
  • Dunia iliumbwa kwa kusudi gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dunia iliumbwa kwa kusudi gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Anaahidi Kwamba Dunia Yetu Itaokoka
    Amkeni!—2023
  • Zawadi ya Milele Kutoka kwa Muumba
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Sayari Yenye Uhai Tele
    Uhai—Ulitokana na Muumba?
  • Katika Gazeti Hili la Amkeni!
    Amkeni!—2023
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 6/1 uku. 16

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Dunia iliumbwa kwa kusudi gani?

Mwanamume atazama uumbaji umaridadi

Dunia ilikusudiwa kuwa makao yenye kupendeza kwa ajili ya wanadamu

Sayari yetu ina hali zinazofaa kabisa kutegemeza uhai. Ina maji mengi ambayo ni muhimu ili kuendeleza uhai. Mwinamo wa dunia, jinsi inavyozunguka, na njia inayofuata angani ni sawa kabisa ili kuzuia maji ya bahari yasiwe barafu au kuwa mvuke. Nalo angahewa la dunia na mfumo wake wa sumaku hufyonza miale hatari. Inashangaza pia kuona jinsi mimea inavyofaidika kutokana na wanyama nao wanyama wanavyofaidika kutokana na mimea. Hivyo, watu wengi wanakubali kwamba dunia iliumbwa kwa kusudi fulani.—Soma Isaya 45:18.

Lakini huenda ukajiuliza, ‘Je, kusudi hilo linatia ndani kuteseka na ukosefu wa haki?’—Soma Kumbukumbu la Torati 32:4, 5.

Je, kusudi la dunia litatimizwa?

Dunia ilikusudiwa kuwa makao yenye kupendeza kwa ajili ya watu wanaoheshimiana na wanaompenda Muumba wao. Hivyo, uhai wa wanadamu una kusudi kubwa kuliko uhai wa mimea na wanyama. Tunaweza kumfahamu Muumba wetu na kuvutiwa na sifa zake kama vile upendo na haki na kuchochewa kumwiga.—Soma Mhubiri 12:13; Mika 6:8.

Muumba wetu anaweza kutimiza chochote anachokusudia. Basi tunaweza kuwa na hakika kwamba ataondoa kuteseka na ukosefu wa haki na kuifanya dunia kuwa makao bora kabisa kwa ajili ya wanadamu.—Soma Zaburi 37:11, 29; Isaya 55:11.

Kwa habari zaidi, soma sura ya 3 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Pia, kinapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki