Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 8/1 uku. 6
  • Mungu Anaweza Kukufariji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Anaweza Kukufariji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Mungu Anavyotufariji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Faraja ya Kweli Inaweza Kupatikana Wapi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • ‘Wafariji Wote Wanaoomboleza’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Zawadi Bora Zaidi ya Mungu​—Kwa Nini Ni Yenye Thamani Sana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 8/1 uku. 6

HABARI KUU | JE, MUNGU ANAKUJALI?

Mungu Anaweza Kukufariji

“Mungu, ambaye huwafariji wale walioshushwa chini, alitufariji.” —2 WAKORINTHO 7:6.

Mwanamke akisoma Biblia

‘Mwana wa Mungu alinipenda mimi na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.’​—WAGALATIA 2:20

KWA NINI WENGINE HAWAAMINI? Hata wanapohitaji faraja kwa hali na mali, baadhi ya watu hudhani haifai kuomba msaada kutoka kwa Mungu ili kukabiliana na matatizo yao. “Ninapofikiria idadi ya watu duniani—na matatizo wanayokabili,” anasema mwanamke aitwaye Raquel, “shida zangu huonekana kidogo sana zikilinganishwa na matatizo yao na hivyo mimi husita kumwomba Mungu msaada.”

BIBLIA INAFUNDISHA NINI? Mungu amefanya mengi kuwasaidia na kuwafariji wanadamu. Wanadamu wote wamerithi dhambi, hivyo hakuna anayeweza kufuata viwango vya Mungu kikamili. Hata hivyo, Mungu “alitupenda akamtuma [Yesu Kristo] Mwana wake kuwa dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu.” (1 Yohana 4:10) Kupitia kifo cha kidhabihu cha Yesu, Mungu amefanya iwezekane kwa wanadamu kupata msamaha wa dhambi, dhamiri njema, na tumaini la uzima wa milele katika ulimwengu mpya wenye amani.a Je, dhabihu hiyo ni kwa ajili ya wanadamu wote, au pia inaweza kukunufaisha wewe binafsi?

Mfikirie mtume Paulo. Alichochewa sana na dhabihu ya Yesu hivi kwamba akaandika: “Naishi kwa imani ambayo ni kumwelekea Mwana wa Mungu, aliyenipenda mimi na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.” (Wagalatia 2:20) Kwa kweli, Yesu alikufa kabla Paulo hajawa Mkristo. Hata hivyo, Paulo aliona dhabihu hiyo kuwa zawadi ya Mungu kwake binafsi.

Kifo cha kidhabihu cha Yesu ni zawadi ya kibinafsi kwako wewe pia. Zawadi hiyo inaonyesha jinsi Mungu anavyokuthamini. Inaweza kukupatia “faraja ya milele na tumaini jema” na hivyo ‘kukuimarisha wewe katika kila tendo na neno jema.’—2 Wathesalonike 2:16, 17.

Hata hivyo, Yesu alidhabihu uhai wake karibu miaka 2,000 iliyopita. Kuna uthibitisho gani kwamba Mungu anataka umkaribie leo?

a Ili ujifunze mengi kuhusu dhabihu ya Yesu, ona sura ya 5 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki