Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 8/1 kur. 3-4
  • Ni Nini Hutukia Baada ya Kifo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nini Hutukia Baada ya Kifo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wafu wako katika hali gani?
  • Je, Kweli Kuna Mahali Penye Moto wa Mateso?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kutakuwa na Ufufuo!
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ufufuo—wa Nani, na Wapi?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Je, Moto wa Mateso Ni Halisi? Kuzimu Ni Wapi Kulingana na Biblia?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 8/1 kur. 3-4

HABARI KUU | UHAI BAADA YA KIFO​—JE, HILO LINAWEZEKANA?

Ni Nini Hutukia Baada ya Kifo?

Watu wazima pamoja na watoto wakiwa wamesimama kando ya jeneza makaburini

“Nilifikiri kwamba kuna sehemu tatu ambazo mtu huenda anapokufa: mbinguni, motoni, au toharani. Nilijua kwamba sikuwa mtu mwema sana hivi kwamba nistahili kwenda mbinguni au mtu mbaya sana hivi kwamba niende motoni. Sikujua waziwazi mambo yanayompata mtu toharani. Sikuona mambo hayo katika Biblia. Yalikuwa tu maoni ya watu.”—Lionel.

“Nilifundishwa kwamba watu wote huenda mbinguni baada ya kufa, ingawa sikuridhishwa na fundisho hilo. Nilifikiri kifo ndiyo mwisho wa mambo yote na kwamba hakuna tumaini lolote kwa wafu.”—Fernando.

Je, umewahi kujiuliza: ‘Ni nini humpata mtu anapokufa? Je, wapendwa wetu waliokufa wanateseka sehemu fulani? Je, tutawaona tena? Tunawezaje kuwa na uhakika?’ Tafadhali ona kile ambacho Maandiko yanafundisha. Kwanza, acheni tuchunguze kile kinachofananishwa na kifo katika Biblia. Kisha tutazungumzia tumaini linalotolewa na Neno la Mungu, Biblia.

Wafu wako katika hali gani?

JIBU LA BIBLIA: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe, wala hawana malipo tena, kwa maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Yote ambayo mkono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote, kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi, mahali unapokwenda.”a—Mhubiri 9:5, 10.

Kwa ufupi, Kaburi, ni mahali ambapo wanadamu huenda wanapokufa; na ni mahali pa mfano au hali ya kutotenda. Mwanamume mwaminifu Ayubu alielewa nini kuhusu Kaburi? Alipoteza mali zake zote na watoto wake wote kwa siku moja, na kupigwa na majipu yenye maumivu makali mwilini. Ayubu alimsihi Mungu hivi: “Laiti ungenificha katika Kaburi [“motoni,” kulingana na Biblia ya Douay Version ya Wakatoliki], kwamba ungenificha.” (Ayubu 1:13-19; 2:7; 14:13) Ni wazi kwamba, Ayubu alijua kwamba Kaburi si mahali penye moto wa mateso, ambapo angeenda kuteseka zaidi. Badala yake, alipaona kuwa mahali ambapo angepata kitulizo.

Kuna njia nyingine ya kujifunza kuhusu hali ya wafu. Tunaweza kuchunguza habari za Kimaandiko zilizoongozwa na roho ya Mungu kuhusu watu nane waliofufuliwa.—Tazama sanduku “Masimulizi Nane ya Ufufuo Yanayotajwa Katika Biblia.”

Hakuna yeyote kati ya watu hao aliyesimulia kwamba alikuwa sehemu fulani akifurahia maisha au akiteseka. Ikiwa watu waliofufuliwa wangekuwa wameenda sehemu hizo walipokufa, je, wasingewasimulia watu kuhusu hilo? Na je, jambo hilo lisingeandikwa katika Biblia iliyoongozwa na roho ya Mungu ili watu wajue? Hakuna jambo lolote kati ya hayo linaloelezwa katika Maandiko. Kati ya wote nane waliofufuliwa hakuna aliyesimulia jambo lolote. Kwa nini? Kwa sababu hawakuwa na fahamu, kama tu kuwa katika usingizi mzito. Kwa kweli, mara nyingi Biblia hutumia usingizi kama mfano wa kuelezea maana ya kifo. Kwa mfano, watumishi waaminifu Daudi na Stefano ‘wamelala usingizi katika kifo.’—Matendo 7:60; 13:36.

Hivyo, kuna tumaini gani kwa wafu? Je, wanaweza kuamshwa kutoka kwenye usingizi huo?

a Katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, neno “Kaburi” ni tafsiri ya neno la Kiebrania “Sheoli” na neno la Kigiriki “Hadesi.” Baadhi ya tafsiri za Biblia hutumia neno “motoni,” hata hivyo, fundisho la kwamba wafu wanateseka katika moto wa mateso si la Kimaandiko.

MASIMULIZI NANE YA UFUFUO YANAYOTAJWA KATIKA BIBLIAb

Mwana wa mjane Nabii Eliya alimfufua mwana wa mjane aliyeishi Sarefathi, kaskazini mwa Israeli.—1 Wafalme 17:17-24.

Mvulana Mshunamu Nabii Elisha, mrithi wa Eliya, alimfufua mvulana katika mji wa Shunemu na kumkabidhi kwa wazazi wake.—2 Wafalme 4:32-37.

Mwanamume katika eneo la mazishi Maiti ya mwanamume ilitupwa ndani ya kaburi lililokuwa na mifupa ya Elisha. Mtu huyo alifufuliwa baada ya mwili wake kugusa mifupa ya nabii huyo.—2 Wafalme 13:20, 21.

Mwana wa mjane aliyeishi Naini Yesu alisimamisha msafara wa mazishi nje ya jiji la Naini na kumfufua kijana huyo, kisha kumkabidhi kwa mama yake aliyekuwa akilia.—Luka 7:11-15.

Binti ya Yairo Yairo, ofisa-msimamizi wa sinagogi, alimsihi Yesu amponye binti yake aliyekuwa mgonjwa. Yesu alimfufua binti huyo aliyekufa muda mfupi tu uliopita.—Luka 8:41, 42, 49-56.

Lazaro, rafiki mpendwa wa Yesu Lazaro alikuwa amekufa kwa siku nne wakati Yesu alipomfufua mbele ya watazamaji.—Yohana 11:38-44.

Dorkasi Mtume Petro alimfufua mwanamke huyo mpendwa aliyejulikana kwa matendo yake ya fadhili.—Matendo 9:36-42.

Eutiko Kijana aliyeitwa Eutiko alikufa baada ya kuanguka kutoka ghorofani; na mtume Paulo alimfufua.—Matendo 20:7-12.

b Ufufuo wa Yesu Kristo ni wa muhimu hata zaidi na unatofautiana sana na ule wa watu nane kama itakavyoonyeshwa kwenye makala inayofuata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki