Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp16 Na. 5 kur. 4-5
  • Jinsi Mungu Anavyotufariji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Mungu Anavyotufariji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JUKUMU LA YESU LA KUWAFARIJI WOTE WANAOOMBOLEZA
  • ‘Wafariji Wote Wanaoomboleza’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Wafariji Wale Wanaohuzunika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Faraja ya Kweli Inaweza Kupatikana Wapi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Farijiwa na Nguvu za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
wp16 Na. 5 kur. 4-5
Yesu akimgusa mtu mwenye ukoma kabla ya kumponya

HABARI KUU | UNAWEZA KUPATA WAPI FARAJA?

Jinsi Mungu Anavyotufariji

Mtume Paulo alisema kwamba Yehovaa ni “Mungu wa faraja yote, ambaye hutufariji katika dhiki yetu yote.” (2 Wakorintho 1:3, 4) Hivyo, Biblia inatuhakikishia kwamba Mungu anaweza kutusaidia na kwamba Baba yetu wa mbinguni atatufariji chini ya hali yoyote.

Bila shaka, ni lazima tufanye jambo fulani ikiwa tunataka Mungu atufariji. Je, daktari anaweza kumtibu mgonjwa ikiwa hajaenda kupata matibabu? Nabii Amosi aliuliza hivi: “Je, watu wawili watatembea pamoja isipokuwa wawe wamekutana kwa mapatano?” (Amosi 3:3) Hivyo, Maandiko yanatuhimiza hivi: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.”—Yakobo 4:8.

Tunawezaje kuwa na uhakika kwamba Mungu atatukaribia? Kwanza kabisa, mara kwa mara yeye hutuambia kwamba anataka kutusaidia. (Ona sanduku.) Pili, kwa sababu tuna ushahidi kutoka kwa watu walioishi nyakati za kale na leo pia ambao wamefarijiwa na Mungu.

Leo watu wengi hutafuta msaada kutoka kwa Mungu, kama Mfalme Daudi alivyofanya alipokabili matatizo maishani. Wakati fulani, alimwomba Yehova hivi: “Uisikie sauti ya kusihi kwangu ninapokulilia unisaidie.” Je, Mungu alimjibu? Ndiyo. Daudi aliongezea hivi: “Nami nimesaidiwa, hivi kwamba moyo wangu unashangilia.”—Zaburi 28:2, 7.

JUKUMU LA YESU LA KUWAFARIJI WOTE WANAOOMBOLEZA

Mungu amempa Yesu jukumu muhimu la kuwafariji watu. Miongoni mwa kazi ambazo Mungu alimpa Yesu ni “kufunga majeraha ya waliovunjika moyo” na “kuwafariji wote wanaoomboleza.” (Isaya 61:1, 2) Kama ilivyotabiriwa, Yesu aliwahangaikia sana ‘wote waliotaabika na kulemewa na mizigo.’—Mathayo 11:28-30.

Yesu aliwafariji watu kwa kuwapa ushauri wenye hekima, kuwatendea kwa fadhili, na wakati mwingine kuwaponya. Siku moja mtu mwenye ukoma alimsihi Yesu hivi: “Ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.” Yesu akamsikitikia na kumjibu: “Ninataka. Takasika.” (Marko 1:40, 41) Yule mtu mwenye ukoma akapona.

Leo, Mwana wa Mungu hayuko duniani ili kutufariji moja kwa moja. Hata hivyo, Yehova, “Mungu wa faraja yote,” anaendelea kuwafariji wale walio na uhitaji. (2 Wakorintho 1:3) Fikiria njia nne ambazo Mungu hutumia kuwafariji watu.

  • Biblia. “Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutokana na Maandiko tuwe na tumaini.”—Waroma 15:4.

  • Roho Takatifu ya Mungu. Muda mfupi baada ya kifo cha Yesu, kutaniko lote la Kikristo liliingia katika kipindi cha amani. Kwa nini? Kwa sababu ‘lilitembea katika kumwogopa Yehova na katika faraja ya roho takatifu.’ (Matendo 9:31) Roho takatifu ya Mungu, yaani, nguvu yake ya utendaji, ina nguvu nyingi. Mungu anaweza kuitumia kumfariji mtu yeyote katika hali yoyote.

  • Sala. Biblia inatushauri hivi: “Msihangaike juu ya kitu chochote.” Kisha inaongeza, “maombi yenu na yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kwa njia ya Kristo Yesu.”—Wafilipi 4:6, 7.

  • Wakristo Wenzetu wanaweza kuwa marafiki wa kweli na kutufariji tunapopatwa na matatizo. Mtume Paulo alieleza kwamba waandamani wake walikuwa ‘msaada wenye kutia nguvu’ katika ‘uhitaji na dhiki.’—Wakolosai 4:11; 1 Wathesalonike 3:7.

Mashahidi wa Yehova wakimfariji Mkristo mwenzao

Hata hivyo, huenda ukajiuliza ikiwa kweli mambo hayo yanaweza kukusaidia. Hebu tuchunguze watu ambao walikabili matatizo yaliyotajwa mwanzoni mwa makala hii. Kama wao, utatambua kwamba Mungu anaendelea kutimiza ahadi hii yenye kutia moyo: “Kama vile mtu ambaye mama yake mwenyewe anaendelea kumfariji, ndivyo mimi nitakavyoendelea kuwafariji ninyi.”—Isaya 66:13.

a Yehova ni jina la Mungu kama linavyoonyeshwa katika Biblia.

Jinsi Tunavyojua Kwamba Mungu Anapenda Kutufariji

  • “Wewe mwenyewe, Ee Yehova, umenisaidia na kunifariji.”​—Zaburi 86:17.

  • “‘Wafarijini, wafarijini watu wangu,’ asema Mungu wenu.”​—Isaya 40:1.

  • “Yehova amesema hivi: . . . ‘Kama vile mtu ambaye mama yake mwenyewe anaendelea kumfariji, ndivyo mimi nitakavyoendelea kuwafariji ninyi.’”​—Isaya 66:12, 13.

  • “Wenye furaha ni wale wanaoomboleza, kwa kuwa watafarijiwa.”​—Mathayo 5:4.

  • ‘Mtupieni [Mungu] mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawajali ninyi.’​—1 Petro 5:7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki