Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp17 Na. 1 uku. 4
  • Nianze Jinsi Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nianze Jinsi Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Unavyoweza Kunufaika Zaidi Unaposoma Biblia
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Jitahidi Uwe Msomaji Mzuri
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kunufaika kwa Usomaji wa Biblia Kila Siku
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Kwa Nini Kusoma Ni Muhimu kwa Watoto—​Sehemu 1: Kusoma au Kutazama?
    Msaada kwa Ajili ya Familia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
wp17 Na. 1 uku. 4

HABARI KUU | JINSI YA KUFAIDIKA KATIKA USOMAJI WAKO

Mwanamke akisali kabla ya kusoma Biblia
Nianze Jinsi Gani?

Unaweza kufanya ili ufurahie usomaji wako wa Biblia na kufaidika zaidi? Chunguza mapendekezo matano ambayo yamewasaidia watu wengi.

Andaa mazingira mazuri. Tafuta mazingira tulivu. Epuka mambo yanayoweza kukukengeusha unaposoma. Kusomea mahali penye mwanga wa kutosha na hewa safi kunaweza kufanya ufaidike zaidi.

Uwe na mtazamo mzuri. Kwa kuwa Biblia ina ujumbe kutoka kwa Baba yetu wa mbinguni, utafaidika zaidi ukiwa na mtazamo kama wa mtoto aliye tayari kufundishwa na mzazi wake mwenye upendo. Ikiwa una mtazamo au maoni yasiyofaa kuihusu Biblia, ondoa mtazamo huo ili uweze kufundishwa na Mungu.—Zaburi 25:4.

Sali kabla ya kuanza kusoma. Biblia ina mawazo ya Mungu, kwa hiyo tunahitaji msaada wake ili kuielewa. Mungu ameahidi kuwapa “roho takatifu wale wanaomwomba.” (Luka 11:13) Roho takatifu itakusaidia kuelewa mawazo ya Mungu. Baada ya muda, itakusaidia kuelewa hata “mambo mazito ya Mungu.”—1 Wakorintho 2:10.

Soma ili uelewe. Usisome tu ili kumaliza sehemu fulani. Tafakari kwa kina mambo unayosoma. Jiulize maswali kama haya: ‘Mtu huyu ninayesoma habari zake alikuwa na sifa gani? Ninaweza kutumiaje habari hii maishani mwangu?’

Uwe na malengo hususa. Ili ufaidike na usomaji wa Biblia, uwe na lengo la kujifunza mambo hususa yatakayoboresha maisha yako. Unaweza kujiwekea malengo kama vile: ‘Kujifunza mengi kumhusu Mungu.’ ‘Kuboresha utu wangu, kuwa mume au mke bora.’ Kisha, chagua sehemu za Biblia zitakazokusaidia kutimiza malengo hayo.a

Mapendekezo hayo matano yatakusaidia kuanza kuisoma Biblia. Lakini unaweza kufanya nini ili ufurahie zaidi usomaji wako? Makala inayofuata inatoa mapendekezo kadhaa.

a Ikiwa hujui jinsi ya kupata habari za Biblia kuhusu mambo hayo, wasiliana na Mashahidi wa Yehova nao watafurahi kukusaidia.

JINSI YA KUFAIDIKA KATIKA USOMAJI WAKO

  • Soma taratibu

  • Tafakari unayosoma na uwazie matukio hayo

  • Elewa muktadha wa mistari unayosoma

  • Tafuta mambo ya kujifunza katika usomaji wako

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki