Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp17 Na. 2 kur. 3-4
  • Zawadi ya Pekee Sana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Zawadi ya Pekee Sana
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Zawadi Bora Zaidi ya Mungu​—Kwa Nini Ni Yenye Thamani Sana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Ni Zawadi Gani Bora Kuliko Zote?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Yesu Kristo—Ujumbe Wake Unavyokuhusu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Fidia—Zawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
wp17 Na. 2 kur. 3-4
Mtu mwenye umri mkubwa akimpatia mvulana kichongeo chenye umbo la mashua

HABARI KUU | JE, UTAITHAMINI ZAWADI BORA ZAIDI YA MUNGU?

Zawadi ya Pekee Sana

HUENDA kichongeo cha Jordan chenye umbo la mashua kisionekane kuwa chenye thamani yoyote. Hata hivyo, ni moja kati ya vitu ambavyo anathamini sana. Jordan anaeleza hivi: “Russell, rafiki ya familia yetu mwenye umri mkubwa alinipatia kichongeo hicho nilipokuwa na umri mdogo.” Baada ya Russell kufa, Jordan alielezwa kwamba Russell aliwasaidia na kuwategemeza sana babu na wazazi wake walipokuwa na matatizo. Jordan anaendelea kusema hivi: “Kwa kuwa ninamfahamu vizuri Russell, sasa ninaithamini zaidi zawadi hii ndogo aliyonipa.”

Kama katika kisa cha Jordan, huenda zawadi ikaonekana kuwa yenye thamani ndogo au haina thamani kabisa machoni pa watu wengine. Hata hivyo, kwa mtu anayethamini, zawadi ni kitu cha pekee sana. Biblia inaeleza kuhusu zawadi yenye thamani kubwa kwa kutumia maneno haya yanayojulikana na wengi: “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee, ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.”—Yohana 3:16.

Zawadi hiyo inaweza kumfanya mpokeaji apate uzima wa milele! Je, kuna zawadi iliyo na thamani zaidi kuliko hiyo? Ingawa huenda wengine wasitambue thamani ya zawadi hiyo, Wakristo wa kweli wanaiona kuwa yenye “thamani sana.” (Zaburi 49:8; 1 Petro 1:18, 19) Hata hivyo, kwa nini Mungu alimtoa Mwana wake awe zawadi kwa ajili ya ulimwengu?

Mtume Paulo anafafanua sababu kwa kusema hivi: “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote.” (Waroma 5:12) Mwanadamu wa kwanza, Adamu, alikataa kumtii Mungu kimakusudi na hivyo akafa. Kupitia kwa Adamu, kifo kikaenea kwa wazao wake wote, yaani, jamii yote ya wanadamu.

“Mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo, lakini zawadi ambayo Mungu hutoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.” (Waroma 6:23) Ili kuwakomboa wanadamu kutoka katika utumwa wa kifo, Mungu alimtuma Mwana wake, Yesu Kristo, ili atoe uhai wake mkamilifu kuwa dhabihu kwa ajili ya wanadamu. Kwa msingi wa dhabihu hiyo, inayoitwa “fidia,” wote wanaomwamini Yesu watapata uzima wa milele.—Waroma 3:24.

Kuhusiana na baraka zote ambazo Mungu huwapatia waabudu wake kwa njia ya Yesu Kristo, Paulo anasema hivi: “Mungu apewe shukrani kwa ajili ya zawadi yake ya bure isiyoelezeka.” (2 Wakorintho 9:15) Naam, fidia ni zawadi ya pekee sana hivi kwamba hatuwezi kuielezea kikamili. Lakini kwa nini fidia ni zawadi ya pekee sana ikilinganishwa na zawadi zingine ambazo Mungu amewapatia wanadamu? Ni ya pekee jinsi gani?a Tunapaswa kuionaje? Tunakutia moyo usome makala mbili zinazofuata ili upate majibu yanayotegemea Biblia.

a Kwa hiari, Yesu “aliitoa nafsi yake kwa ajili yetu.” (1 Yohana 3:16) Hata hivyo, kwa kuwa dhabihu hiyo ilikuwa sehemu ya kusudi la Mungu, makala zifuatazo zinakazia jukumu la Mungu akiwa Mwandaaji wa fidia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki