Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w18 Oktoba uku. 32
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Habari Zinazolingana
  • Stefano—“Amejaa Kibali cha Mungu na Nguvu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Stefano Anapigwa kwa Mawe
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Tembea Katika Hofu kwa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
w18 Oktoba uku. 32

Je, Wajua?

Mwanafunzi Stefano alifanikiwaje kuendelea kuwa mtulivu alipokuwa akiteswa?

Stefano aliendelea kuwa mtulivu alipokuwa mbele ya Sanhedrini

STEFANO alikabili kundi la wanaume wenye hasira kali. Wanaume hao 71 waliotumikia kama waamuzi, walikuwa washiriki wa mahakama kuu zaidi katika Israeli, yaani, Sanhedrini, na walikuwa miongoni mwa watu wenye mamlaka zaidi wa taifa hilo. Kuhani Mkuu Kayafa ambaye miezi michache mapema alikuwa amesimamia mahakama hiyo Yesu alipohukumiwa kifo, ndiye aliyekuwa amewakusanya tena wanaume hao. (Mt. 26:57, 59; Mdo. 6:8-12) Walipokuwa wakiwaleta mashahidi wa uwongo mbele yao, mmoja baada ya mwingine, wanaume hao walitambua jambo fulani la ajabu kumhusu Stefano kwamba uso wake ulikuwa “kama uso wa malaika.”—Mdo. 6:13-15.

Stefano alifanikiwaje kuendelea kuwa mtulivu na bila wasiwasi chini ya hali hiyo yenye kutia woga? Kabla ya kukokotwa mbele ya Sanhedrini, Stefano alikuwa amezama kabisa katika huduma yake, akiongozwa na roho ya Mungu yenye nguvu. (Mdo. 6:3-7) Alipokuwa akishtakiwa, roho hiyohiyo ilikuwa ikitenda kazi ndani yake kama mfariji na kama mkumbushaji. (Yoh. 14:16, maelezo ya chini) Stefano alipokuwa akijitetea kwa ujasiri, kama tunavyosoma kwenye kitabu cha Matendo sura ya 7, roho takatifu ilimkumbusha vifungu 20 hivi au zaidi vya Maandiko ya Kiebrania. (Yoh. 14:26) Lakini imani ya Stefano iliimarishwa hata zaidi alipomwona Yesu katika maono akiwa amesimama kwenye mkono wa kuume wa Mungu.—Mdo. 7:54-56, 59, 60.

Huenda siku moja sisi pia tutakabili vitisho na mateso. (Yoh. 15:20) Ikiwa tutajilisha Neno la Mungu kwa ukawaida na kushiriki kikamili katika huduma, tutairuhusu roho ya Yehova itende kazi ndani yetu. Pia, tutapata nguvu za kukabiliana na upinzani wowote huku tukiendelea kuwa na amani ya akili.—1 Pet. 4:12-14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki