Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w20 Mei kur. 8-11
  • Wafalme Wanaopingana Katika Wakati wa Mwisho

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wafalme Wanaopingana Katika Wakati wa Mwisho
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Habari Zinazolingana
  • “Mfalme wa Kaskazini” Katika Wakati wa Mwisho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Yehova Anafunua Mambo Ambayo “Lazima Yatendeke Upesi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mfalme wa Kaskazini” Ni Nani Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Ule Msafara Mrefu wa Serikali Kubwa za Ulimwengu Wakaribia Mwisho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
w20 Mei kur. 8-11

Wafalme Wanaopingana Katika Wakati wa Mwisho

Baadhi ya unabii unaotajwa kwenye chati hii unafafanua matukio yanayotendeka katika kipindi kilekile cha wakati. Unabii huo unatoa uthibitisho mbalimbali kwamba tunaishi katika “wakati wa mwisho.”—Dan. 12:4.

Chati inayoonyesha unabii mbalimbali na utambulisho wa mfalme wa kaskazini na mfalme wa kusini kuanzia mwaka wa 1870 mpaka leo.
  • Chati ya 1, inaonyesha unabii unaotimia katika kipindi kilekile cha wakati katika siku za mwisho kuanzia mwaka wa 1870 hivi hadi mwaka wa 1918. Kipindi kinachoanzia mwaka wa 1914 na kuendelea kinatambulishwa kuwa wakati wa mwisho. Unabii wa 1: Mnyama wa mwituni mwenye vichwa saba ambaye kuonekana kwake kunaanza hata kabla ya tarehe ya mwanzoni kabisa ya chati. Katika Vita vya Kwanza vya Ulimwengu, kichwa cha saba cha mnyama huyo kinajeruhiwa. Kuanzia mwaka wa 1917 na kuendelea, kichwa cha saba cha mnyama huyo kinapona na mnyama huyo wa mwituni anapata nguvu tena. Unabii wa 2: Mfalme wa kaskazini na mfalme wa kusini wanaweza kutambuliwa mwaka wa 1870. Mfalme wa kaskazini anaibuka tena mwaka wa 1871 akiwa serikali ya Ujerumani. Mwanzoni mfalme wa kusini anatambuliwa kuwa Uingereza, lakini katika mwaka wa 1917 mahali pake panachukuliwa na Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani. Unabii wa 3: Kuanzia miaka ya 1870, Charles T. Russell na wenzake wanatambuliwa kuwa yule ‘mjumbe.’ Mwanzoni mwa miaka ya 1880, gazeti la ‘Zion’s Watch Tower’ linawatia moyo wasomaji wake wahubiri habari njema. Unabii wa 4: Kuanzia mwaka wa 1914 na kuendelea ni kipindi cha mavuno. Magugu yanatenganishwa na ngano. Unabii wa 5: Kuanzia mwaka wa 1917 na kuendelea, miguu ya chuma na udongo inatokea. Pia tunaona yafuatayo: Matukio ya ulimwengu kuanzia mwaka wa 1914 hadi mwaka wa 1918, Vita vya Kwanza vya Ulimwengu. Matukio yanayowaathiri watu wa Yehova: Kuanzia mwaka wa 1914 hadi mwaka wa 1918, Wanafunzi wa Biblia nchini Uingereza na Ujerumani wanafungwa gerezani. Mwaka wa 1918, akina ndugu kutoka makao makuu nchini Marekani wanafungwa gerezani.
    Unabii wa 1.

    Maandiko Ufu. 11:7; 12:13, 17; 13:1-8, 12

    Unabii “Mnyama wa mwituni” amewatawala watu duniani kwa zaidi ya miaka 3,000. Katika wakati wa mwisho, kichwa chake cha saba kinajeruhiwa. Baadaye, kichwa hicho kinapona na “dunia yote” inamfuata mnyama huyo. Shetani anamtumia mnyama huyo wa mwituni “kupigana na wale waliobaki.”

    Utimizo Baada ya Gharika, serikali za wanadamu zinazompinga Yehova zajitokeza. Karne nyingi baadaye, wakati wa Vita vya Kwanza vya Ulimwengu, Milki ya Uingereza inadhoofika sana. Inapata nguvu tena inapoungana na Marekani. Katika wakati wa mwisho, Shetani amekuwa akitumia mfumo wake wote wa kisiasa kuwatesa watu wa Mungu.

  • Unabii wa 2.

    Andiko Dan. 11:25-45

    Unabii Mapambano kati ya mfalme wa kaskazini na mfalme wa kusini katika wakati wa mwisho.

    Utimizo Serikali ya Ujerumani na ile Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani zapambana. Katika mwaka wa 1945 Muungano wa Sovieti na nchi zinazouunga mkono zinakuwa mfalme wa kaskazini. Mwaka wa 1991, Muungano wa Sovieti unavunjika, na baadaye, serikali ya Urusi na nchi zinazoiunga mkono zinakuwa mfalme wa kaskazini.

  • Unabii wa 3.

    Maandiko Isa. 61:1; Mal. 3:1; Luka 4:18

    Unabii Yehova anamtuma “mjumbe” wake ili ‘afungue njia’ kabla ya Ufalme wa Kimasihi kusimamishwa. “Mjumbe” huyo anaanza ‘kuwatangazia wapole habari njema.’

    Utimizo Kuanzia mwaka wa 1870 na kuendelea, C. T. Russell na wenzake wanajifunza Biblia kwa bidii ili wafafanue mafundisho ya kweli. Katika miaka ya 1880, wanaanza kukazia kwamba watumishi wa Mungu wanapaswa kuhubiri. Wanachapisha makala kama vile “Wahubiri 1,000 Wanahitajika” na “Walitiwa Mafuta Ili Kuhubiri.”

  • Unabii wa 4.

    Andiko Mt. 13:24-30, 36-43

    Unabii Adui anapanda magugu katika shamba la ngano, na magugu hayo yanaachwa yaendelee kukua, nayo yanaficha ngano hadi kipindi cha mavuno kitakapofika; kisha magugu yanatenganishwa na ngano.

    Utimizo Kuanzia mwaka wa 1870 na kuendelea, tofauti kati ya Wakristo wa kweli na wa uwongo inazidi kuwa wazi. Katika wakati wa mwisho, Wakristo wa kweli wanakusanywa na kutenganishwa na Wakristo wa uwongo.

  • Unabii wa 5.

    Andiko Dan. 2:31-33, 41-43

    Unabii Miguu ya chuma na udongo ni sehemu ya sanamu iliyotengenezwa kwa madini mbalimbali.

    Utimizo Udongo unafananisha watu wanaotawaliwa na Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani ambao wanapinga utawala wa serikali hiyo. Watu hao wanadhoofisha uwezo wa serikali hiyo ya ulimwengu wa kutumia nguvu zake kikamili kama chuma.

  • Chati ya pili, inaonyesha unabii unaotimia katika kipindi kilekile cha wakati katika siku za mwisho kuanzia mwaka wa 1919 hivi hadi mwaka wa 1945. Mfalme wa kaskazini anatambuliwa kuwa serikali ya Ujerumani hadi kufikia mwaka wa 1945. Mfalme wa kusini anatambuliwa kuwa Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani. Unabii wa 6: Katika mwaka wa 1919, Wakristo watiwa-mafuta wanakusanywa katika kutaniko lililopangwa upya. Kuanzia mwaka wa 1919 na kuendelea, kazi ya kuhubiri yapamba moto na kusonga mbele. Unabii wa 7: Katika mwaka wa 1920, Ushirika wa Mataifa waanzishwa na unaendelea kuwapo hadi Vita vya Pili vya ulimwengu vinapoanza. Pia tunaona yafuatayo: Unabii wa 1, mnyama wa mwituni mwenye vichwa saba anaendelea. Unabii wa 5, miguu ya chuma na udongo inaendelea. Matukio ya ulimwengu kuanzia mwaka wa 1939 hadi mwaka wa 1945, Vita vya Pili vya Ulimwengu. Matukio yanayowaathiri watu wa Yehova: Nchini Ujerumani kuanzia mwaka wa 1933 mpaka mwaka wa 1945, zaidi ya Mashahidi 11,000 wanafungwa gerezani. Nchini Uingereza kuanzia mwaka wa 1939 hadi mwaka wa 1945, karibu Mashahidi 1,600 wanafungwa gerezani. Nchini Marekani kuanzia mwaka wa 1940 mpaka mwaka wa 1944, kuna mashambulizi zaidi ya 2,500 dhidi ya Mashahidi.
    Unabii wa 6.

    Maandiko Mt. 13:30; 24:14, 45; 28:19, 20

    Unabii “Ngano” inakusanywa “ghalani,” na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” anawekwa rasmi ili asimamie “watumishi wa nyumbani.” Kazi ya kuhubiri “habari njema ya Ufalme” inaanza kuenea katika “dunia yote inayokaliwa.”

    Utimizo Mwaka wa 1919 mtumwa mwaminifu anawekwa rasmi ili awasimamie watu wa Mungu. Kuanzia wakati huo na kuendelea, Wanafunzi wa Biblia wamekuwa wakihubiri zaidi na zaidi. Leo, Mashahidi wa Yehova wanahubiri katika nchi zaidi ya 200 na wanachapisha machapisho yanayotegemea Biblia katika lugha zaidi ya 1,000.

  • Unabii wa 7.

    Maandiko Dan. 12:11; Ufu. 13:11, 14, 15

    Unabii Mnyama wa mwituni mwenye pembe mbili anawaambia watu duniani watengeneze “sanamu ya yule mnyama wa mwituni” na anaipa ‘pumzi sanamu hiyo.’

    Utimizo Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani yawa mstari wa mbele katika kuanzisha Ushirika wa Mataifa. Ushirika huo unaungwa mkono na mataifa mengine. Hatimaye, mfalme wa kaskazini anajiunga na Ushirika huo pia—lakini anafanya hivyo kuanzia mwaka wa 1926 hadi 1933 tu. Kama ilivyo kwa Umoja wa Mataifa (UM) leo, Ushirika huo unasifiwa kwamba unaweza kutimiza mambo yanayoweza tu kutimizwa na Ufalme wa Mungu.

  • Chati ya 3, unabii unaotimia katika kipindi kilekile cha wakati katika siku za mwisho kuanzia mwaka wa 1945 mpaka mwaka wa 1991. Mfalme wa kusini anatambuliwa kuwa Muungano wa Sovieti na nchi zinazouunga mkono hadi kufikia mwaka wa 1991, na baada ya hapo ni serikali ya Urusi na nchi zinazoiunga mkono. Mfalme wa kusini anatambuliwa kuwa Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani. Unabii wa 8: Moshi mzito wa bomu la atomu, ukiashiria uharibifu mkubwa uliosababishwa na Serikali Kuu ya Uingereza na Marekani. Unabii wa 9: Shirika la Umoja wa Mataifa laanzishwa mwaka wa 1945, likichukua mahali pa Ushirika wa Mataifa. Pia tunaona yafuatayo: Unabii wa 1, mnyama wa mwituni mwenye vichwa saba anaendelea. Unabii wa 5, miguu ya chuma na udongo inaendelea. Unabii wa 6, mwaka wa 1945 kuna zaidi ya wahubiri 156,000. Mwaka wa 1991, kuna zaidi ya wahubiri 4,278,000. Matukio yanayowaathiri watu wa Yehova: Katika Muungano wa Sovieti kuanzia mwaka wa 1945 mpaka mwaka wa 1951, maelfu ya Mashahidi walipelekwa uhamishoni Siberia.
    Unabii wa 8.

    Andiko Dan. 8:23, 24

    Unabii Mfalme mwenye uso mkali analeta “uharibifu kwa njia isiyo ya kawaida.”

    Utimizo Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani imesababisha uharibifu mkubwa sana. Kwa mfano, wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu, Marekani ilisababisha uharibifu ambao haujawahi kuonekana kamwe ilipomwangushia adui yake mabomu mawili ya atomu.

  • Unabii wa 9.

    Maandiko Dan. 11:31; Ufu. 17:3, 7-11

    Unabii Mnyama wa mwituni mwenye “rangi nyekundu” na pembe kumi anapanda kutoka katika shimo refu lisilo na mwisho, naye ni mfalme wa nane. Kitabu cha Danieli kinamtaja mfalme huyo wa nane kuwa, “kile kitu chenye kuchukiza sana kinachosababisha ukiwa.”

    Utimizo Ushirika wa Mataifa unaingia katika kipindi cha kutotenda wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu. Baada ya vita, UM ‘unasimamishwa.’ Kama ilivyokuwa kwa Ushirika wa Mataifa, UM unapewa utukufu ambao Ufalme wa Mungu unapaswa kupewa. UM utashambulia dini.

  • Chati ya 4, unabii unaotimia katika kipindi kilekile cha wakati katika siku za mwisho na unahusu siku zetu hadi kufikia vita vya Har–​Magedoni. Mfalme wa kaskazini anatambuliwa kuwa serikali ya Urusi na nchi zinazoiunga mkono. Mfalme wa kusini anatambuliwa kuwa Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani. Unabii wa 10: Viongozi wa ulimwengu watangaza ‘amani na usalama.’ Baada ya hapo, dhiki kuu yaanza. Unabii wa 11: Mataifa yashambulia mashirika ya dini ya uwongo. Unabii wa 12: Serikali za ulimwengu zawashambulia watu wa Mungu. Watiwa-mafuta waliobaki wanakusanywa kwenda mbinguni. Unabii wa 13: Har–​Magedoni. Yule anayeketi juu ya farasi mweupe anakamilisha ushindi wake. Yule mnyama wa mwituni mwenye vichwa saba anaharibiwa; ile sanamu kubwa inapondwapondwa kwenye miguu yake ya chuma na udongo. Pia tunaona yafuatayo: Unabii wa 1, mnyama wa mwituni mwenye vichwa saba aendelea mpaka wakati wa Har–​Magedoni. Unabii wa 5, miguu ya chuma na udongo inaendelea mpaka wakati wa Har–​Magedoni. Unabii wa 6, leo kuna zaidi ya wahubiri 8,580,000. Matukio yanayowaathiri watu wa Yehova: Mwaka wa 2017, wenye mamlaka nchini Urusi wawafunga Mashahidi na kuchukua kwa lazima majengo ya ofisi ya tawi.
    Unabii wa 10 na 11.

    Maandiko 1 The. 5:3; Ufu. 17:16

    Unabii Mataifa yanatangaza “amani na usalama,” kisha “zile pembe kumi” na “yule mnyama wa mwituni” wanamshambulia “yule kahaba” na kumwangamiza. Baada ya hapo, mataifa yanaharibiwa.

    Utimizo Mataifa yatadai kwamba yamefanikiwa kupata amani na usalama. Kisha, mataifa yanayounga mkono UM yataharibu mashirika ya dini ya uwongo. Huo utakuwa mwanzo wa dhiki kuu. Dhiki hiyo itakwisha wakati mfumo wote wa ulimwengu utakapoharibiwa katika vita vya Har–Magedoni.

  • Unabii wa 12.

    Maandiko Eze. 38:11, 14-17; Mt. 24:31

    Unabii Gogu ashambulia nchi ya watu wa Mungu. Kisha, malaika wanawakusanya wale “waliochaguliwa.”

    Utimizo Mfalme wa kaskazini, pamoja na serikali nyingine za ulimwengu, zitawashambulia watu wa Mungu. Wakati fulani baada ya shambulizi hilo kuanza, watiwa-mafuta waliobaki watakusanywa kwenda mbinguni.

  • Unabii wa 13.

    Maandiko Eze. 38:18-23; Dan. 2:34, 35, 44, 45; Ufu. 6:2; 16:14, 16; 17:14; 19:20

    Unabii “Yule aliyeketi” juu ya “farasi mweupe” anakamilisha “ushindi wake” kwa kumharibu Gogu na jeshi lake. “Yule mnyama wa mwituni” ‘anatupwa ndani ya ziwa la moto,’ na sanamu ile kubwa inapondwapondwa.

    Utimizo Yesu, Mfalme anayetawala wa Ufalme wa Mungu anawaokoa watu wa Mungu. Akiwa pamoja na watawala wenzake 144,000 na majeshi ya malaika, Yesu anauharibu muungano wa mataifa, yaani, mfumo wote wa kisiasa wa Shetani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki