Unawaza Bible ni nini?
Unawaza ni . . .
kitabu kya mawazo ya bantu?
kitabu kya ma arishi?
ao ni Sauti ya Mungu?
SHIKIA VILE BIBLE INASEMA
“Kila andiko irianjikiwa na roo ya Mungu.”—2 Timoteo 3:16, Tradiksion ya dunia ya sasa.
KUYUWA VILE KUTAKUSAIDIA JE?
Utapata majibu ya maulizo ya lazima ya mu maisha.—Mezali 2:1-5.
Utapata mashauri ya muzuri ya kukuongoza mu maisha.—Zaburi 119:105.
Kutakusaidia utumainie kama maisha itakuwa muzuri uku ku mbele.—Waroma 15:4.
ILE MAMBO BIBLE INASEMA NI YA BYA KWERI TU?
Ni ya bya kweri, nju:
Bible inapatana ku mwanzo tii na ku mwisho. Bantu 40 ba kuachana-achana njo barianjikaka Bible. Barifanyaka ile kaji mu miaka 1 600 na bya yulu. Kya kushangaisha, mu bale bantu 40, ba mingi abakuyuwanaka ata. Kwa lakini, Bible yote inapatana ku mwanzo tii na ku mwisho, na yote iko nasemeya kintu kimoya!
Bible iko na ma istware ya bya kweri. Leo bantu ba mingi bale bananjikaka mambo ya istware banazobeleaka tu kuanjika mambo ya muzuri ile ba kwabo barifanya, apana ya mubaya. Kwa lakini, bale barianjikaka Bible bo abana vile, barianjikaka mankosa yabo na ya ba kwabo.—2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16; Zaburi 51:1-4.
Bible iko na ma profesi ya bya kweri. Kurikuwa kushakupita miaka 200 tangu Bible itabiri asema mukini ya Babilone batayalabisha. (Isaya 13:17-22) Irionesha vile batayalabisha, na tena iritaya na njina ya ule atayalabisha!—Isaya 45:1-3.
Ma profesi ingine ya mingi ya mu Bible, irifanshika ata mu mambo ya kiloko-kiloko. Shi njo vile Sauti ya Mungu inapashwa kuwa!—2 Petro 1:21.
WAZA MBELE
Sauti ya Mungu inezi kukusaidia je nju ukuwe na maisha ya muzuri?
Bible inajibu ile ulizo mu ISAYA 48:17, 18 na mu 2 TIMOTEO 3:16, 17.