Bafu batafufukaka?
Unawaza . . .
batafufukaka?
abastafufukaka?
ao banezi kufufuka?
SHIKIA VILE BIBLE INASEMA
“Kutakuwa ufufuko.”—Matendo 24:15, Tradiksion ya dunia ya sasa.
KUYUWA VILE KUTAKUSAIDIA JE?
Kutakutuliza kama unafisha.—2 Wakorinto 1:3, 4.
Kutakufanya ushongope lufu.—Waebrania 2:15.
Kutakusaidia ukuwe na kitumaini ya kusema, unezi kuonana tena na banduku yako bale bashakufwaka.—Yohana 5:28, 29.
ILE MAMBO BIBLE INASEMA NI YA BYA KWERI TU?
Ni ya bya kweri, nju:
Mungu njo ariumbaka bujima. Bible inasema kama Jeova Mungu njo “Mwanzo ya bujima.” (Zaburi 36:9; Matendo 17:24, 25) Ule mwenye aripachiaka biumbe byote bujima, eko na nguvu ya kurudishia bujima muntu ule ashakufwa.
Mungu arifufulaka bantu nzamani. Mu Bible muko ma abari ya bantu 8 bale Mungu arifufulaka. Mu bale bantu murikuwa: ba biyana, bazee, banaume na banamuke. Bamoya barikufwaka na akuyakawiya tu sana, lakini mwingine ye arikuwa ashakufanya mashiku 4 mu tuburi!—Yohana 11:39-44.
Mungu eko na amu sana ya kufufula tena bantu. Jeova anachukiaka lufu; analuonaka sa enemi. (1 Wakorinto 15:26) Eko na amu sana ya kuwina ule enemi. Ni kusema, atatosha lufu kupitia ufufuko. Anapenda sana kufufula bantu bale beko mu akiri yake, na anapenda kubaona beko bajima.—Yobu 14:14, 15.
WAZA MBELE
Nju ya nini tunazekaka na kufwa?
Bible inajibu ile ulizo mu MWANZO 3:17-19 na mu WAROMA 5:12.