Unawaza maisha itakuwa je uku ku mbele?
Iyi dunia . . .
itabakia tu paka ivi?
italabika kupita?
ao itakuwa ya muzuri sana?
SHIKIA VILE BIBLE INASEMA
“Mungu . . . atabapangusha machozi yote ku mancho, na lufu alutakuyako tena, na kirio, na kuomboleza, na maumivu, byote abitakuyako tena. Mambo ya nzamani ainako tena.”—Ufunuo 21:3, 4, Tradiksion ya dunia ya sasa.
KUYUWA VILE KUTAKUSAIDIA JE?
Utakuwa na kaji ya muzuri na ya kufuraisha.—Isaya 65:21-23.
Autalukulaka ao kuteswa tena.—Isaya 25:8; 33:24.
Utaishi na furaa milele pamoya na famiye yako na barafiki yako.—Zaburi 37:11, 29.
ILE MAMBO BIBLE INASEMA NI YA BYA KWERI TU?
Ni ya bya kweri, nju:
Mungu eko na nguvu ya kufanya bile analaka. Ni Jeova Mungu tu njo Bible inaita “Muweza-Yote,” nju eko na nguvu yashipo mwisho. (Ufunuo 15:3) Njo pale eko kapable ya kufanya bile analaka nju iyi dunia ikuwe fashi ya muzuri sana. Bible yo yenyewe inasema kama “kwa Mungu mambo yote inawezekanaka.”—Matayo 19:26.
Mungu anapenda kufanya bile analaka. Kwa mufano, Mungu eko na amu sana ya kufufula bafu.—Yobu 14:14, 15.
Tena, Bible inaonesha asema Yesu, Mutoto wa Mungu, ariponeshaka ba malari. Nju ya nini arifanyaka vile? Ni nju aripendaka kubasaidia. (Marko 1:40, 41) Vile arikuwa tayari kusaidia bantu, ile inaonesha asema njo vile Baba yake na ye anekalaka.—Yohana 14:9.
Njo pale, tukuwe sire asema Jeova na Yesu banapendaka kutusaidia nju tukuwe na maisha ya muzuri uku ku mbele!—Zaburi 72:12-14; 145:16; 2 Petro 3:9.
WAZA MBELE
Mungu atafanya nini nju maisha ikuwe ya muzuri uku ku mbele?
Bible inajibu ile ulizo mu MATAYO 6:9, 10 na mu DANIELI 2:44.