Dunia iko mu mikono ya nani?
Unawaza iko mu mikono . . .
ya Mungu?
ya bantu?
ao ya Shetani?
SHIKIA VILE BIBLE INASEMA
“Dunia mujima iko mu mikono ya ule Mubaya.”—1 Yohana 5:19.
“Mutoto wa Mungu arikuya kwalabisha kaji ya Shetani.”—1 Yohana 3:8, Tradiksion ya dunia ya sasa.
KUYUWA VILE KUTAKUSAIDIA JE?
Kutakusaidia uyuwe nju ya nini mu dunia muko mateso ya mingi.—Ufunuo 12:12.
Kutakusaidia uamini kama iyi dunia itakuwa ya muzuri sana.—1 Yohana 2:17.
ILE MAMBO BIBLE INASEMA NI YA BYA KWERI TU?
Ni ya bya kweri, nju:
Guvernema ya Shetani iko nendelea tu kwalabika. Jeova eko determiné kutosha guvernema ya Shetani. Analaka asema “atamutosha Shetani” na kutengeneza mambo yote ile Shetani arialabisha.—Waebrania 2:14, Tradiksion ya dunia ya sasa.
Mungu arimuchakula Yesu Kristo nju atawale iyi dunia. Yesu anachana sana na ba shefu ba mu iyi dunia, bale beko nafanshia bantu bintu bibaya, na bale beko na tamaa sana. Mungu analaka asema Yesu “atashikiria buluma muntu wa nivo ya chini na maskini . . . Atabatosha mu mateso na mu bubaya.”—Zaburi 72:13, 14.
Mungu ashilandake. Bible inasema ivi: “Mungu ashiwezi kulanda.” (Waebrania 6:18) Kama tu Jeova analaka kufanya kintu, iko sa ashakukifanya deja! (Isaya 55:10, 11) “Batamutosha ule eko natawala iyi dunia.”—Yohana 12:31.
WAZA MBELE
Pale batamutosha Shetani, dunia itakuwa je?
Bible inajibu ile ulizo mu ZABURI 37:10, 11 na mu UFUNUO 21:3, 4.