Uko wa maana mu kutaniko ata kama ushakuzeka
“Saa minangaria bintu bile mirianzaka kufanya pale mirikuwaka kiyana, minashangaa sana. Nju minazeka mishiwezi tena kufanya mambo ile mirianzaka kufanya nzamani.”—Dada Connie, wa miaka 83.
Pengine na weye auwezi tena kufanya mambo ya mingi sa ile urianzaka kufanya pale urikuwaka ukingariki kiyana. Ata kama urimutumikia Jeova miaka ya mingi na ukingariki mwaminifu kwake, saa unakomparé mambo ile urianzaka kufanya mu kaji ya Jeova na ile uko nafanya leo, unezi kurishikia mubaya. Kama njo vile uko narishikia, ni nini njo itakusaidia wendelee kuwa na furaa?
WAZA NJU YA MAMBO ILE JEOVA ANAPENDA UFANYE
Uriulize ivi: ‘Jeova anapenda nifanye nini?’ Misemo ile iko mu kitabu kya Kumbukumbu la Torati 6:5, inezi kukupachia nguvu. Inasema ivi: “Unapashwa kumupenda Jeova Mungu wako na roo yako yote na bumuntu bwako bote na nguvu yako yote.”
Iyi versé inaonesha asema Jeova anapenda umutumikie na uwezo yako yote ile uko nayo. Kuyuwa vile kutakusaidia ushijikomparé na bengine, ao kukomparé mambo ile uko nafanya leo na ile urianzaka kufanya nzamani saa urikuwaka kiyana.
Waza mbele: Saa urikuwaka kiyana, ni mambo kani ile urianzaka kumupachia Jeova? Batumishi ba mingi ba Jeova banezi kusema kama barianzaka kumupachia Jeova yabo yote. Na weye, ile mambo urianzaka kumupachia mu ile wakati njo iripatanaka na uwezo yako ya ile wakati. Lakini nju sitwasion yako ishakushanjé, mambo ile pengine uko nafanya leo njo ile inapatana na uwezo ile uko nayo leo. Kama unaweka ile mawazo mu akiri, utafikia kuona asema ukingariki tu namupachia Jeova yako yote sa vile urianzaka kufanya nzamani.
Saa urikuwaka kiyana urianzaka kumupachia Jeova yako yote. Na ata apa ushakuzeka uko namupachia Jeova yako yote
UNEZI KUSAIDIA BENGINE
Ona kintu kingine kile unapashwa kufanya: Ushangarie tu mambo ile autaweza kufanya nju ushakuzeka, lakini angaria mambo ya mingi ile unezi kufanya nju ya kusaidia bengine ata kama ushakuzeka. Kusema tu bya kweri, kuko mambo ya mingi ile unezi kufanya leo, ile aukupashake kuweza kufanya pale urikuwaka kiyana. Kwa mufano ona mambo ile unezi kufanya:
Ambia bengine mambo ile uririonea mu maisha. Kwa mufano, ona mambo ile Bible inasema mu iyi maversé:
Mufalme David: “Mirikuwaka kiyana na sasa minazeka, lakini mishiyaonaka muntu ata moya wa aki banamwachiria tu paka ivi, ao batoto yake beko natafuta mukate.”—Zb. 37:25.
Josué: “Sasa, mushikie! Minakuwa karibu na kufwa. Munayuwa muzuri na roo yenu yote na bumuntu bwenu bote asema, akuna ata musemo moya mu malako yote ya Jeova ile irishinda kufanshika. Yote irifanshika nju yenu. Akuna ata musemo moya ile aikufanshike.”—Yos. 23:14.
Pengine na weye ushakusemaka misemo ya kufanana na ile. David na Josué barisemaka mambo ile barijioneaka mu maisha yabo. Nju bale batumishi bamifu ba Jeova barisemaka mambo ile barijioneaka na kurishikiria bo benyewe mu bwingi bwa miaka ile bariishi, njo pale mambo ile barisemaka irikuwaka na bujito sana.
Kama urianzaka kumutumikia Jeova tangu nzamani, na weye unezi kuonesha bengine mabaraka ile uripata mu kaji ya Jeova na vile aribariki bengine. Eske unakumbuka wakati moya ile urijioneaka vile Jeova anabariki batumishi bake? Kama ni vile, ushibakie na ile mambo we moya, ambiayo bengine. Ile itakusaidia ukumbuke mambo ya muzuri ile urijioneaka. Na saa banduku na badada yako batashikia ile mambo, itabapachia nguvu sana.—Ro. 1:11, 12.
Tena, nju ya kwankurajé banduku na badada yako, ufanye nguvu wanze kwenda kufwatia marenion ku salle du royaume kama utaweza. Kama unafanya vile, utapachia nguvu banduku na badada yako, na bo batakupachia nguvu. Dada Connie, ule turitaya, anasema ivi: “Kwenda kufwatia marenion ku salle du royaume kunanisaidiaka nishikuwe dekurajé. Kama niko ku salle du royaume, biko nguvu nikuwe dekurajé. Nju minarioneaka vile banduku na badada banaoneshaka asema bashakunipenda. Nju ya kuonesha asema bile banifanshiaka ni bya valere, minabapachiaka tu makado. Ku marenion, minankurajaka bengine, na bo bananiankurajaka.”
JEOVA ANAFURAIAKA SANA KAJI ILE UKO NAMUFANSHIA
Mu Bible muko mifano ya mingi ya bantu bale abakukuwake tena na uwezo ya kufanya mambo ya mingi mu kaji ya Jeova. Lakini Jeova aribapendaka sana. Tubebe mufano ya Siméon. Arikuwaka ashakuzeka ile saa barimuzalaka Yesu. Saa arianzaka kwenda ku tample, pengine arianzaka kuona ba biyana beko nafanya makaji ya lazima ku tample. Lakini pengine ye moya arianzaka kuriona asema ashina wa valere ku mancho ya Jeova nju ashikukuyake na nguvu ya kufanya tena ma kaji ile ba biyana barianzaka kufanya. Lakini Jeova yeye ashikwanzake kumuona vile. Arianzaka kumuona sa muntu ule arikuwaka na ‘matendo ya kunyoloka na ule arianzaka kuritoa sana mu kaji Yake.’ Njo pale arimubariki na arimupachia privilège ao pendeleo ya kumuona Yesu saa arikuwaka mutoto. Tena Jeova arimutumikishaka nju ya kuleta profesi ile inaonesha asema Yesu atakuwa Masiya. (Lu. 2:25-35) Jeova ashikwanzake tu kumuona Siméon sa mwanaume ule ashakuzeka na ule ashina na nguvu. Lakini arianzaka kumuona sa mwanaume wa imani ya nguvu sana na ule ‘arikuwa na roo takatifu.’
Jeova arimubariki Siméon na arimupachia privilège ya kumuona Yesu. Tena arimupachia privilège ya kutoa profesi ile inaonesha asema Yesu njo Masiya
Na weye ukuwe sire asema Jeova anaonaka kaji yako kuwa ya lazima sana ata kama pengine autaweza kufanya byote bile unapenda kufanya mu kaji yake. Jeova anaichikaka sana mambo ile tunafanyaka kupatana na kile tuko nakyo, apana kupatana na kile atuna.—2 Ko. 8:12.
Njo pale, angaikia bile utaweza kufanya, apana bile autaweza. Kwa mufano, ni maubiri ya je ile unezi kufanya ata mu wakati kiloko? Tena unezi kupachia nguvu banduku na badada yako saa unabaitako ku telefone ao kubatumiako ka message. Matendo ya kiloko-kiloko ile inaonesha mapendo inapachiaka sana nguvu banduku na badada, surtout kama inatoka kwa bantu saa mweye, bale bashakumutumikia Jeova miaka mingi.
Banduku na badada bengine bale bashakuzeka abana na uwezo ya kufanya byote bile banapenda. Angaria mambo ile irifanshika mu Afrique de l’Est mu ankadré “Dada moya ariokoa maisha ya muntu.”
Ushisabu asema mufano yako ya muzuri ya vile urimutumikia Jeova tangu nzamani na vile uko naendelea kumutumikia tii paka na leo, inezi kupachia nguvu bantu bengine. Uko mufano muzuri sana nju ushakuvumilia bya mingi sana. Njo pale ukuwe sire asema “Mungu ashezi kukosa shukrani nju asabu kaji yenu na mapendo ile murionesha nju ya njina yake pale murianza kutumikia batakatifu na vile muko naendelea kubatumikia.”—Ebr. 6:10.
ENDELEA KUFANYA YAKO YOTE NJU YA KUSAIDIA BENGINE
Ma étude inaonesha asema banaume na banamuke bale bashakuzeka bale banasaidiaka bengine banekalaka na santé ya muzuri, banawazaka muzuri, na banekalaka naishi maisha ya murefu.
Kusema tu bya kweri, kufanshia bantu mambo ya muzuri, akutashimamisha buzee. Ni ufalme ya Mungu tu njo itatutosha mu nzambi, na ile njo itafanya tushizeke tena na tushikufwe.—Ro. 5:12.
Lakini, vile uko naendelea kumutumikia Jeova, ni kusema, vile uko nasaidia bengine bamuyuwe, ile itakusaidia ushipoteshe tumaini yako na ukuwe na santé ya muzuri. Mweye banduku na badada bale bashakuzeka, muyuwe asema kwa Jeova kaji ile muko nafanya ni ya lazima sana. Na tena, muyuwe asema banduku na badada mu kutaniko banamipendaka sana nju muko na imani ya nguvu.