28 Umuweke Yoshua+ katika madaraka yake na umutie moyo na kumutia nguvu, kwa sababu yeye ndiye atavuka+ mbele ya watu hawa na yeye ndiye atawafanya wariti inchi yenye utaona.’
14 Kisha Yehova akamuambia Musa, “Angalia! Wakati wako wa kufa umekaribia.+ Ita Yoshua, na muende* kwenye hema ya mukutano, ili nimuweke katika madaraka yake.”+ Kwa hiyo Musa na Yoshua wakaenda na kusimama kwenye hema ya mukutano.
23 Kisha akamuweka* Yoshua+ mwana wa Nuni katika madaraka yake na kusema: “Ukuwe hodari na mwenye nguvu,+ kwa sababu ni wewe utaingiza Waisraeli katika inchi yenye nimewaapia,+ na nitaendelea kuwa pamoja na wewe.”