Siku ya Ine, 17 Mwezi wa 7
Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote Naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.—Mez. 17:17.
Maria, mama ya Yesu, alikuwa na lazima ya kutiwa nguvu. Hakukuwa na bwana lakini alipaswa kupata mimba. Hakukuwa alishakomalisha mutoto yeyote, lakini sasa alipaswa kuhangaikia mutoto mwenye angefikia kuwa Masiya. Na juu alikuwaka hayafanya ngono, namna gani angefasiria Yosefu, muchumba wake, ile mambo yote? (Lu. 1:26-33) Maria alipata wapi nguvu? Alitafuta musaada kwa Yehova. Kwa mufano, alimuomba Gabrieli amupatie mafasirio zaidi kuhusu mugao wake. (Lu. 1:34) Kisha wakati kidogo alisafiri kuenda mu eneo ya “inchi ya milima” ya Yuda ili kutembelea Elizabeti, mutu wa jamaa yake. Elizabeti alimupongeza Maria na aliongozwa na Yehova ili kutoa unabii wenye kutia moyo kuhusu mwana wa Maria mwenye alikuwa hayazaliwa. (Lu. 1:39-45) Maria alisema kama Yehova alikuwa “ametenda kwa nguvu kwa mukono wake.” (Lu. 1:46-51) Yehova alimutia nguvu Maria kupitia Gabrieli na Elizabeti. w23.10 14-15 fu. 10-12
Siku ya Tano, 18 Mwezi wa 7
Alitufanya tukuwe ufalme, makuhani kwa Mungu na Baba yake.—Ufu. 1:6.
Hesabu kidogo ya wanafunzi wa Kristo wametiwa mafuta na roho takatifu, na wanafurahia uhusiano wa pekee pamoya na Yehova. Wale wanafunzi 144000 watatumika kama makuhani mbinguni pamoya na Yesu. (Ufu. 14:1) Mahali Patakatifu yenye ilikuwa mu tabenakulo inafananisha hali yao ya kufanywa kuwa wana wa Mungu wakati wangali ku dunia. (Ro. 8:15-17) Mahali Patakatifu Zaidi ya mu tabenakulo inafananisha mbinguni, kwenye Yehova anakuwaka. “Pazia” yenye ilitenganisha Patakatifu na Patakatifu Zaidi ilifananisha mwili wa kibinadamu wa Yesu wenye ulimuzuia kuingia mbinguni akiwa Kuhani Mukubwa zaidi wa hekalu ya kiroho. Kwa kutoa mwili wake wa kibinadamu kuwa zabihu kwa ajili ya wanadamu, Yesu alifanya iwezekane kwa Wakristo wote watiwa-mafuta kuenda mbinguni. Wanapaswa pia kuacha miili yao ya kibinadamu ili wapate zawabu ya kuishi mbinguni.—Ebr. 10:19, 20; 1 Ko. 15:50. w23.10 28 fu. 13
Siku ya Posho, 19 Mwezi wa 7
Nitakosa wakati kama ninaendelea kueleza juu ya Gideoni.—Ebr. 11:32.
Gideoni hakukasirika wakati watu wa Efraimu walimulaumu. (Amu. 8: 1-3) Hakuwajibia kwa kasirani. Alionyesha unyenyekevu kwa kusikiliza mambo yenye walikuwa nasema, na aliwajibia kwa upole; na ile ilifanya watulie. Wazee wenye kuwa na hekima wanaiga Gideoni kwa kusikiliza kwa uangalifu na kujibia kwa upole wakati wengine wanawalaumu. (Yak. 3:13) Kama wanafanya vile, kutaniko itaendelea kuwa na amani. Wakati watu walianza kumusifu Gideoni juu alishinda Wamidiani, alimupatia Yehova sifa. (Amu. 8:22, 23) Wazee wanaweza kufanya nini ili kumuiga Gideoni? Wanapaswa kumusifu Yehova juu ya mambo yote yenye wako natimiza. (1 Ko. 4:6, 7) Kwa mufano, kama watu fulani wanaanza kumusifu muzee fulani juu iko na uwezo wa kufundisha, anaweza kusema kama mambo yote yenye tuko najifunza inatoka mu Neno ya Mungu na kama siye wote tuko tu nazoezwa na tengenezo yake. Wakati fulani wazee wanaweza kufikiria ikiwa wako nafundisha mu njia yenye inamuletea Yehova sifa ao mu njia yenye itawaletea wao wenyewe sifa. w23.06 4 fu. 7-8