Mwezi wa 7
Siku ya Pili, 1 Mwezi wa 7
Akapita katika inchi akitenda mema na kuponyesha.—Mdo. 10:38.
Mambo yote yenye Yesu alisema na kufanya, kutia ndani miujiza yenye alifanya, ilionyesha kama aliiga kwa ukamili mawazo na hisia za Baba yake. (Yoh. 14:9) Miujiza ya Yesu inaweza kutufundisha nini? Yesu na Baba yake wanatupenda sana. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alionyesha kama alipenda sana watu kwa kutumia nguvu yake ya ajabu ili kusaidia wale wenye walikuwa nateseka. Siku moya, vipofu wawili wanaume walimuomba awasaidie. (Mt. 20:30-34) Yesu “akawasikilia huruma” na kisha akawaponyesha. Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “akawasikilia huruma” yenye inatumiwa hapa, inaonyesha kama Yesu alisikia sana huruma wakati aliona ule mwanaume anateseka. Ile huruma ni namna ya kuonyesha upendo, na njo yenye ilimuchochea pia Yesu alishe watu wenye walikuwa na njala na aponyeshe mutu fulani mwenye alikuwa na ukoma. (Mt. 15:32; Mk. 1:41) Tuko hakika kama Yehova, Mungu wa “huruma nyingi,” na Mwana wake, wanatupenda sana na wanahuzunikaka wakati wanaona tunateseka. (Lu. 1:78; 1 Pe. 5:7) Wanatamani sana kutosha mambo yote ya mubaya yenye iko nahangaisha watu! w23.04 3 fu. 4-5
Siku ya Tatu, 2 Mwezi wa 7
Enyi wenye kumupenda Yehova, muchukie mambo ya mubaya. Analinda uzima wa washikamanifu wake; anawaokoa katika mukono wa waovu.—Zb. 97:10.
Tunaweza kujaza akili yetu na mawazo ya muzuri kwa kusoma na kujifunza Biblia. Kuhuzuria mikutano na kuhubiri kutalinda pia mawazo yetu. Na Yehova anatuahidi kama hataacha tujaribiwe kupita vile tunaweza kuvumilia. (1 Ko. 10:12, 13) Juu tuendelee kuwa waaminifu kwa Yehova mu hizi siku za mwisho zenye kuwa nguvu, tunapaswa kusali sana. Yehova anapenda ‘tumwange mioyo yetu mbele yake’ katika sala. (Zb. 62:8) Umusifu Yehova na umushukuru juu ya mambo yote yenye anakufanyiaka. Umuombe akupatie uhodari wa kuhubiri. Umuombe akusaidie uvumilie magumu yoyote na upinge majaribu yoyote yenye unaweza kupata. Usiruhusu jambo ao mutu yeyote akuzuie kusali kwa Yehova kila mara. w23.05 7 fu. 17-18
Siku ya Ine, 3 Mwezi wa 7
Tufikiriane . . . , tutiane moyo.—Ebr. 10:24, 25.
Juu ya nini tunaendaka ku mikutano? Kwanza, ni juu ya kumutukuza Yehova. (Zb. 26:12; 111:1) Tunaendaka pia ku mikutano juu ya kutiana moyo mu hii wakati ya magumu. (1 Te. 5:11) Wakati tunatoa maelezo ku mikutano tutakuwa tumetimiza ile mambo mbili. Lakini, kuko mambo yenye inaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kutoa maelezo. Tunaweza kuogopa kutoa maelezo, ao pengine tunaweza kupenda kutoa maelezo mara mingi, lakini wakati fulani kiongozi hatupatie nafasi ya kufanya vile. Mu ile hali, nini njo inaweza kutusaidia? Mutume Paulo alisema kama tunapaswa kujikaza “kutiana moyo.” Kukumbuka kama wengine watatiwa moyo hata kupitia maelezo yetu ya mwepesi, yenye kuonyesha imani yetu, kutatutia moyo tukuwe natoa maelezo. Na kama kiongozi hatupatie nafasi ya kufanya vile, tunaweza kufurahi juu ile itasaidia wengine wapate nafasi ya kutoa maelezo.—1 Pe. 3:8. w23.04 20 fu. 1-3
Siku ya Tano, 4 Mwezi wa 7
Apande kuenda Yerusalemu, . . . na kujenga upya nyumba ya Yehova. —Ezr. 1:3.
Mufalme alitoa tangazo! Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho mu Babiloni kwa miaka 70 hivi, walikuwa sasa huru kurudia mu inchi yao Israeli. (Ezr. 1:2-4) Ni Yehova tu njo alifanya ile iwezekane. Juu kwa kawaida, Wababiloni hawakukuwa naachilia huru waamishwa wao. (Isa. 14:4, 17) Lakini, wakati mufalme mwenye alikuwa natawala mu Babiloni alitoshwa ku kiti, mufalme mwenye alianza kutawala pa nafasi yake aliambia Wayahudi warudie. Kila Muyahudi, zaidi sana vichwa vya familia, alipaswa kukamata uamuzi: Kutoka Babiloni ao kubakia. Pengine haikukuwa mwepesi kuamua. Juu wengi walikuwa walishazeeka, haikukuwa mwepesi kwao kufanya ile safari ya murefu. Na juu Wayahudi wengi walizaliwa mu Babiloni, walikuwa hawayaishi fasi ingine, waliona Israeli kuwa muji wa mababu zao. Pengine Wayahudi fulani walifikia kuwa matajiri sana mu Babiloni. Kwa hiyo, haingekuwa mwepesi kwao kuacha nyumba zao za muzuri ao biashara yenye walikuwa nafanya juu waende mu inchi yenye hawakujua. w23.05 14 fu. 1-2
Siku ya Posho, 5 Mwezi wa 7
Mukuwe tayari.—Mt. 24:44.
Neno ya Mungu inatutia moyo tuendelee kukomalisha sifa ya uvumilivu, huruma, na upendo. Luka 21:19 inasema hivi: “Kupitia uvumilivu wenu mutaokoa uzima wenu.” Wakolosai 3:12 inasema hivi: “Muvae . . . huruma.” Na 1 Watesalonike 4:9, 10 inasema hivi: “Ninyi wenyewe mumefundishwa na Mungu kupendana. . . . Lakini, tunawachochea ninyi, ndugu, muendelee kufanya vile kwa ukamili zaidi.” Wanafunzi wenye tayari walikuwa walishaonyesha sifa ya uvumilivu, huruma, na upendo njo waliambiwa ile maneno. Lakini, walipaswa kuendelea kukomalisha zile sifa. Tunapaswa kufanya pia vile. Juu uweze, ona namna Wakristo wa kwanza-kwanza walionyesha zile sifa. Kisha, utaona namna unaweza kuwaiga na namna unaweza kuonyesha kama uko tayari kwa ajili ya taabu kubwa. Kwa hiyo, wakati taabu kubwa itaanza utakuwa tayari umejifunza namna ya kuonyesha uvumilivu na utaazimia kabisa kuendelea kuvumilia. w23.07 3 fu. 4, 8
Siku ya Yenga, 6 Mwezi wa 7
Kutakuwa njia kubwa kule, . . . Njia ya Utakatifu.—Isa. 35:8.
Ikuwe tuko watiwa-mafuta ao “kondoo wengine,” tunapaswa kubakia mu “Njia ya Utakatifu.” Ile njia itatusaidia tuendelee kumuabudu Yehova sasa na wakati wenye kuya, wakati Ufalme wa Mungu utafanya dunia ikuwe muzuri sana. (Yoh. 10:16) Kuanzia 1919 K.K.Y., mamilioni ya wanaume, wanamuke, na watoto wametoka mu Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uongo, na wameanza kutembea mu ile barabara ya mufano. Wakati Wayahudi walitoka mu Babiloni, Yehova alitosha vizuizi. (Isa. 57:14) Tuseme nini kuhusu “Njia ya Utakatifu” leo? Mamia ya miaka mbele ya 1919, Yehova alianza kutumia wanaume wenye kumuogopa juu wasaidie watu wengine watoke mu Babiloni Mukubwa. (Linganisha na Isaya 40:3.) Wale wanaume walifanya kazi ya maana ya kutayarisha barabara, ni kusema, barabara ya kiroho juu ya kusaidia watu wenye kuwa na mioyo ya muzuri watoke mu Babiloni Mukubwa na waingie mu paradiso ya kiroho ili kumuabudu Yehova pamoya na watu wake. w23.05 15-16 fu. 8-9
Siku ya Kwanza, 7 Mwezi wa 7
Mumutumikie Yehova kwa furaha. Muingie mbele yake kwa vigelegele vya shangwe.—Zb. 100:2.
Yehova anapenda tumutumikie kwa furaha na kwa kupenda. (2 Ko. 9:7) Sasa, tunapaswa kujikaza kufikia muradi wetu hata kama hatujisikie kufanya vile? Fikiria mufano wa mutume Paulo. Alisema hivi: “Ninapiga-piga mwili wangu na kuuongoza kama mutumwa.” (1 Ko. 9:25-27) Hata kama wakati fulani Paulo hakukuwa na hamu ya kufanya mambo yenye Yehova alimuomba, alijikaza kuifanya. Yehova alikubali utumishi wake? Ndiyo! Na alimupatia zawabu juu ya bidii yake. (2 Ti. 4:7, 8) Vilevile, Yehova anafurahiaka wakati tunajikaza kufikia muradi wetu hata kama hatuna hamu ya kufanya vile. Juu anajua kama kila mara hatufanyake mambo fulani juu tunaipenda, anafurahiaka wakati anaona tunaifanya juu tunamupenda. Sawa vile tu alimubariki Paulo, atatubariki pia juu ya bidii yetu. (Zb. 126:5) Na wakati tunaona namna Yehova iko natubariki, ile inaweza kufanya tuanze hata kupenda sana kufikia miradi yetu. w23.05 29 fu. 9-10
Siku ya Pili, 8 Mwezi wa 7
Siku ya Yehova inakuja.—1 Te. 5:2.
Mutume Paulo alilinganisha wale wenye hawataokoka siku ya Yehova na watu wenye wanalala. Hawajue mambo yenye iko nafanyika pembeni yao ao kama wakati iko napita. Kwa hiyo, hawawezi kujua wakati jambo fulani ya maana inatokea na hawawezi kufanya kitu. Watu wengi sana leo wanalala mu maana ya kiroho. (Ro. 11:8) Hawaamini mambo yenye kuonyesha kama tuko naishi mu “siku za mwisho” na yenye kuonyesha kama taabu kubwa itakuya hivi karibuni. (2 Pe. 3:3, 4) Kwa hiyo, ni jambo ya maana sana kwetu kuwa macho kila siku. (1 Te. 5:6) Kwa hiyo, tunapaswa kuwa wenye kutulia. Juu ya nini? Juu tusijiingize mu mambo ya politike ao mu mambo ya maisha. Kadiri siku ya Yehova iko nakaribia ni vile mukazo wa kuunga mukono mu ile mambo uko naongezeka. Njo maana, hatupaswe kuhangaika sana juu ya mambo yenye tutafanya. Roho takatifu ya Mungu inaweza kutusaidia ili tukuwe wenye kutulia, tusiogope, na tukamate maamuzi ya muzuri.—Lu. 12:11, 12. w23.06 10 fu. 6-7
Siku ya Tatu, 9 Mwezi wa 7
Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, unikumbuke, tafazali, na kunitia nguvu.—Amu. 16:28.
Nini inakuyaka mu akili yako ukisikia jina Samsoni? Pengine unakumbukaka mwanaume mwenye alikuwa na nguvu ya ajabu. Ni kweli. Lakini Samsoni alikamata uamuzi wa mubaya wenye ulikuwa na matokeo ya kuumiza. Hata vile, Yehova alikazia uangalifu maisha ya uaminifu ya Samsoni na aliiandikisha mu Biblia ili ituletee faida. Yehova alimutumia Samsoni ili kufanya mambo ya ajabu juu ya kusaidia watu wake wenye alikuwa amechagua, ni kusema Waisraeli. Miaka mingi kisha kifo ya Samsoni, Yehova alimuongoza mutume Paulo atie jina ya Samsoni mu liste ya watu wenye walikuwa na imani ya ajabu. (Ebr. 11:32-34) Mufano wa Samsoni unaweza kututia moyo. Alimutegemea Yehova hata wakati hali ilikuwa nguvu. Mufano wake unaweza kututia moyo na mambo ingine yenye unaweza kutufundisha. w23.09 2 fu. 1-2
Siku ya Ine, 10 Mwezi wa 7
Maombi yenu yajulishwe Mungu.—Flp. 4:6.
Tunaweza kukomalisha sifa ya uvumilivu kwa kumuambia Yehova kwa ukawaida mambo yenye iko natuhangaisha. (1 Te. 5:17) Pengine kwa sasa hauna magumu ya nguvu sana. Hata vile, Je, unamuombaka Yehova akuongoze kila mara wakati unapata magumu, unahangaika, na haujue ufanye nini? Kama unamuombaka Yehova akusaidie saa unapata magumu ya kidogo-kidogo leo, itakuwa mwepesi kwako kufanya vile wakati utapata magumu ya nguvu wakati wenye kuya. Kisha, utakuwa hakika kama anajua kabisa wakati na namna ya kukusaidia. (Zb. 27:1, 3) Itakuwa mwepesi sana kwetu kuvumilia taabu kubwa kama tuko navumilia magumu leo. (Ro. 5:3) Juu ya nini tunasema vile? Ndugu na dada wengi wanasemaka kama kila wakati wenye wanavumilia hali ya nguvu, ile inawasaidiaka wakuwe tayari kuvumilia magumu ingine yenye wanaweza kupata. Wakati wanavumilia magumu kwa musaada wa Yehova, ile inafanya wakuwe na imani kama anapenda kuwasaidia. Na ile imani ya nguvu itawasaidia wavumilie magumu ingine yenye wanaweza kupata.—Yak. 1:2-4. w23.07 3 fu. 7-8
Siku ya Tano, 11 Mwezi wa 7
Nitakuonyesha ufikirio.—Mwa. 19:21.
Unyenyekevu na huruma inafanyaka Yehova akuwe na usawaziko. Kwa mufano, Yehova alionyesha kama ni munyenyekevu wakati alikuwa karibu kuharibu watu waovu wenye waliishi mu Sodoma. Alituma malaika wamuambie Loti mwenye haki akimbilie mu maeneo ya milima. Loti aliogopa kuenda kule. Njo maana alimuomba sana Yehova aruhusu yeye na familia yake wakimbilie Soari, muji mudogo wenye Yehova alipangaka pia kuharibu. Yehova angemuambia tu Loti aende kule kwenye alikuwa namuambia aende. Lakini, alimuruhusu aende Soari, na hakuharibu tena ule muji. (Mwa. 19:18-22) Karne mingi kisha, Yehova aliwasikilia huruma wakaaji wa Ninawi. Alituma nabii Yona aambie watu waovu wa mu Ninawi kama atawaharibu na kama ataharibu pia muji wao. Lakini wakati watu wa Ninawi walitubu, Yehova aliwasikilia huruma na hakuharibu tena ule muji.—Yon. 3:1, 10; 4:10, 11. w23.07 21 fu. 5
Siku ya Posho, 12 Mwezi wa 7
Wakamuua [Yehoashi] . . . , lakini hawakumuzika katika makaburi ya wafalme.—2 Ny. 24:25.
Mufano wa Yehoashi unaweza kutufundisha nini? Alikuwa sawa vile muti wenye ulitegemezwa na muti ingine juu mizizi yake haikukuwa nakamata muzuri mu udongo. Wakati Yehoyada, ni kusema, muti wenye ulimutegemeza alikufa, Yehoashi alianza kusikiliza waasi-imani na hakuendelea kuwa muaminifu kwa Yehova. Ile mufano inaonyesha kama hatupaswe kumutii Mungu juu tu watu wa familia yetu na wengine mu kutaniko wanatuwekea mufano muzuri wa kufuata. Juu tuendelee kuwa nguvu kiroho, tunapaswa kujikaza kumupenda na kumuheshimia Yehova kwa kujifunza kwa ukawaida, kufikiri sana, na kusali. (Yer. 17:7, 8; Kol. 2:6, 7) Yehova hatuombe mambo mingi kupita uwezo wetu. Andiko ya Muhubiri 12:13 inaonyesha kwa kifupi mambo yenye anatuomba, inasema hivi: “Ogopa Mungu wa kweli na ushike amri zake, kwa maana hilo ndilo jambo lote lenye mwanadamu anapaswa kufanya.” Ikiwa tunamuogopa Mungu, tutaendelea kuwa washikamanifu kwake. Hata kutokee nini, hakuna jambo yoyote yenye inaweza kuharibisha urafiki wetu pamoya naye. w23.06 19 fu. 17-19
Siku ya Yenga, 13 Mwezi wa 7
Angalia! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.—Ufu. 21:5.
Mustari wa 5 unaanza na hii maneno: “Ule mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme akasema.” (Ufu. 21:5a) Ile ni maneno ya pekee juu inatanguliza maneno ya Yehova. Mu kitabu ya Ufunuo Yehova anazungumuza tu mara tatu na ile ni moja kati ya ile mara tatu. Kwa hiyo, haiko malaika mwenye nguvu ao hata Yesu mwenye kufufuliwa lakini Yehova mwenyewe njo anatoa ule uhakikisho! Ile inaonyesha kama tunaweza kutumainia kabisa maneno yenye kufuata. Juu ya nini? Juu Yehova “hawezi kusema uongo.” (Tit. 1:2) Ile inafanya maneno yenye tunasoma mu Ufunuo 21:5, 6 ikuwe yenye kutumainika kabisa. Tuzungumuzie neno “Angalia!” (Ufu. 21:5) Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “angalia!” inarudiliwa mara mingi mu kitabu ya Ufunuo. Ni mambo gani yenye inafuata kisha ile neno ya mushangao? Maneno yenye Mungu anasema: “Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Bila shaka Yehova iko nazungumuzia mabadiliko ya wakati wenye kuya. Kwake ile ahadi ni ya hakika kabisa, kwa hiyo anazungumuzia ile mabadiliko sawa vile iko nafanyika tayari.—Isa. 46:10. w23.11 3-4 fu. 7-8
Siku ya Kwanza, 14 Mwezi wa 7
Akaenda inje na kulia kwa uchungu.—Mt. 26:75.
Mutume Petro alipambana na uzaifu mbalimbali. Tuone mifano fulani. Wakati Yesu alikuwa anafasiria namna angeteseka na kufa ili kutimiza unabii wa Biblia, Petro alimukaripia. (Mk. 8:31-33) Mara kwa mara Petro na mitume wengine walibishana ili kujua ni nani njo alikuwa mukubwa zaidi kati yao. (Mk. 9:33, 34) Usiku wa mwisho mbele Yesu akufe, Petro alitenda bila kufikiri na kukata sikio ya mwanaume fulani. (Yoh. 18:10) Uleule usiku, Petro aliogopa na akamukana rafiki yake Yesu mara tatu. (Mk. 14:66-72) Ile ilifanya Petro alie kwa uchungu. Yesu hakuacha ule mutume wake mwenye alikuwa amevunjika moyo sana. Kisha Yesu kufufuliwa, alimupatia Petro nafasi ya kuonyesha kama anamupenda. Alimupatia nafasi ya kuchunga kondoo wake kwa unyenyekevu. (Yoh. 21:15-17) Petro alikubali kabisa ule mugao. Petro alikuwa Yerusalemu siku ya Pentekoste na akakuwa kati ya watu wa kwanza wenye walitiwa mafuta na roho takatifu. w23.09 22 fu. 6-7
Siku ya Pili, 15 Mwezi wa 7
Chunga kondoo wangu wadogo.—Yoh. 21:16.
Mutume Petro aliambia hivi wazee wenzake “Muchunge kundi la Mungu.” (1 Pe. 5:1-4.) Kama uko muzee, tunajua kama unapenda ndugu na dada zako na unapenda kuwahangaikia. Lakini, wakati fulani unaweza kuona kama uko na mambo mingi ya kufanya ao unachoka sana na hautaweza kutimiza ile daraka. Unaweza kufanya nini? Ambia Yehova mahangaiko yako. Petro aliandika hivi: “Kama mutu yeyote anatumikia, afanye hivyo kama vile anategemea nguvu zenye Mungu anatoa.” (1 Pe. 4:11) Pengine ndugu na dada zako wako napambana na magumu yenye haiwezi kumalizika kabisa mu hii ulimwengu. Lakini kumbuka kama “muchungaji mukubwa,” Yesu Kristo, anaweza kuwasaidia zaidi kuliko weye. Anaweza kufanya vile leo na pia mu dunia mupya. Mungu haombe wazee mambo mingi; anawaomba tu wapende ndugu zao, wahangaikie ndugu zao, na wakuwe “mifano kwa kundi.” w23.09 29-30 fu. 13-14
Siku ya Tatu, 16 Mwezi wa 7
Yehova anajua kama kufikiri kwa watu wenye hekima ni kwa bure.—1 Ko. 3:20.
Tunapaswa kuepuka kuwa na mawazo ya wanadamu wenye hawatii sheria za Yehova. Kama tunakuwa na mawazo sawa ya watu wenye hawamutii Yehova, siye pia tunaweza kumuacha Yehova na kuacha kutii sheria zake. (1 Ko. 3:19) Mara mingi “hekima ya ulimwengu huu” inachocheaka watu wasimutii Mungu. Wakristo fulani wa Pergamamu na Tiatira walichochewa na watu wenye waliishi nao wenye walikuwa waasherati na waabudu sanamu. Juu wale Wakristo waliachilia uasherati uendelee, Yesu aliwapatia mashauri mazito. (Ufu. 2:14, 20) Leo, watu wanaweza kufanya tukuwe na mawazo ya mubaya. Watu wa familia na marafiki wanaweza kutuambia kama tuko wenye kushikamana kupita kiasi na mambo yenye tunaamini na wanaweza kutuambia tuvunje sheria za Yehova. Kwa mufano, wanaweza kusema kama haiko jambo ya maana kuendelea kuwa na mwenedo safi na kama kanuni zenye kuwa mu Biblia kuhusu mwenendo ni mambo ya zamani. Wakati fulani tunaweza kuwaza kama maagizo yenye Yehova anatupatiaka haieleweke. Tunaweza hata kujaribiwa kuongeza mambo yenye “kupita mambo yenye yaliandikwa.”—1 Ko. 4:6. w23.07 16 fu. 10-11
Siku ya Ine, 17 Mwezi wa 7
Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote Naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.—Mez. 17:17.
Maria, mama ya Yesu, alikuwa na lazima ya kutiwa nguvu. Hakukuwa na bwana lakini alipaswa kupata mimba. Hakukuwa alishakomalisha mutoto yeyote, lakini sasa alipaswa kuhangaikia mutoto mwenye angefikia kuwa Masiya. Na juu alikuwaka hayafanya ngono, namna gani angefasiria Yosefu, muchumba wake, ile mambo yote? (Lu. 1:26-33) Maria alipata wapi nguvu? Alitafuta musaada kwa Yehova. Kwa mufano, alimuomba Gabrieli amupatie mafasirio zaidi kuhusu mugao wake. (Lu. 1:34) Kisha wakati kidogo alisafiri kuenda mu eneo ya “inchi ya milima” ya Yuda ili kutembelea Elizabeti, mutu wa jamaa yake. Elizabeti alimupongeza Maria na aliongozwa na Yehova ili kutoa unabii wenye kutia moyo kuhusu mwana wa Maria mwenye alikuwa hayazaliwa. (Lu. 1:39-45) Maria alisema kama Yehova alikuwa “ametenda kwa nguvu kwa mukono wake.” (Lu. 1:46-51) Yehova alimutia nguvu Maria kupitia Gabrieli na Elizabeti. w23.10 14-15 fu. 10-12
Siku ya Tano, 18 Mwezi wa 7
Alitufanya tukuwe ufalme, makuhani kwa Mungu na Baba yake.—Ufu. 1:6.
Hesabu kidogo ya wanafunzi wa Kristo wametiwa mafuta na roho takatifu, na wanafurahia uhusiano wa pekee pamoya na Yehova. Wale wanafunzi 144000 watatumika kama makuhani mbinguni pamoya na Yesu. (Ufu. 14:1) Mahali Patakatifu yenye ilikuwa mu tabenakulo inafananisha hali yao ya kufanywa kuwa wana wa Mungu wakati wangali ku dunia. (Ro. 8:15-17) Mahali Patakatifu Zaidi ya mu tabenakulo inafananisha mbinguni, kwenye Yehova anakuwaka. “Pazia” yenye ilitenganisha Patakatifu na Patakatifu Zaidi ilifananisha mwili wa kibinadamu wa Yesu wenye ulimuzuia kuingia mbinguni akiwa Kuhani Mukubwa zaidi wa hekalu ya kiroho. Kwa kutoa mwili wake wa kibinadamu kuwa zabihu kwa ajili ya wanadamu, Yesu alifanya iwezekane kwa Wakristo wote watiwa-mafuta kuenda mbinguni. Wanapaswa pia kuacha miili yao ya kibinadamu ili wapate zawabu ya kuishi mbinguni.—Ebr. 10:19, 20; 1 Ko. 15:50. w23.10 28 fu. 13
Siku ya Posho, 19 Mwezi wa 7
Nitakosa wakati kama ninaendelea kueleza juu ya Gideoni.—Ebr. 11:32.
Gideoni hakukasirika wakati watu wa Efraimu walimulaumu. (Amu. 8: 1-3) Hakuwajibia kwa kasirani. Alionyesha unyenyekevu kwa kusikiliza mambo yenye walikuwa nasema, na aliwajibia kwa upole; na ile ilifanya watulie. Wazee wenye kuwa na hekima wanaiga Gideoni kwa kusikiliza kwa uangalifu na kujibia kwa upole wakati wengine wanawalaumu. (Yak. 3:13) Kama wanafanya vile, kutaniko itaendelea kuwa na amani. Wakati watu walianza kumusifu Gideoni juu alishinda Wamidiani, alimupatia Yehova sifa. (Amu. 8:22, 23) Wazee wanaweza kufanya nini ili kumuiga Gideoni? Wanapaswa kumusifu Yehova juu ya mambo yote yenye wako natimiza. (1 Ko. 4:6, 7) Kwa mufano, kama watu fulani wanaanza kumusifu muzee fulani juu iko na uwezo wa kufundisha, anaweza kusema kama mambo yote yenye tuko najifunza inatoka mu Neno ya Mungu na kama siye wote tuko tu nazoezwa na tengenezo yake. Wakati fulani wazee wanaweza kufikiria ikiwa wako nafundisha mu njia yenye inamuletea Yehova sifa ao mu njia yenye itawaletea wao wenyewe sifa. w23.06 4 fu. 7-8
Siku ya Yenga, 20 Mwezi wa 7
Mawazo yangu hayako mawazo yenu.—Isa. 55:8.
Kama hatupate mambo yenye tuliomba mu sala yetu, tunaweza kujiuliza ‘Jambo yenye niko naombo njo yenye inafaa kabisa?’ Mara mingi tunawazaka kama tunajua jambo yenye inatufaa kabisa. Lakini pengine mambo yenye tuko naomba haiko njo yenye itatusaidia kabisa. Kwa mufano, kama tuko nasali juu ya tatizo fulani, kunaweza kuwa njia ya muzuri zaidi ya kuishugulikia kuliko ile yenye tuko naomba. Na inawezekana mambo fulani yenye tunaomba haipatane na mapenzi ya Yehova. (1 Yo. 5:14) Fikiria mufano wa wazazi. wenye walimuomba Yehova ahakikishe kama mutoto wao anabakia katika kweli. Ile inaweza kuonekana kuwa ombi yenye kufaa. Lakini Yehova hakazake mutu yeyote amutumikie. Anapenda siye wote, kutia ndani watoto wetu, tuchague kumutumikia. (Kum. 10:12, 13; 30:19, 20) Kwa hiyo, wazazi walipaswa njo kumuomba Yehova awasaidie waguse moyo wa mutoto wao ili mutoto wao achochewe kumupenda na kuwa rafiki yake.—Mez. 22:6; Efe. 6:4. w23.11 21 fu. 5; 23 fu. 12
Siku ya Kwanza, 21 Mwezi wa 7
Muendelee kufarijiana.—1 Te. 4:18.
Juu ya nini kufariji wengine ni njia ya maana ya kuonyesha kama tunawapenda? Kulingana na kitabu fulani yenye kuzungumuzia mambo ya Biblia, neno “kufariji” yenye Paulo alitumia maana yake kusimama pembeni ya mutu ili kumutia moyo wakati iko napambana na majaribu ya nguvu. Kwa hiyo wakati tunafariji muamini mwenzetu mwenye iko mu magumu, tunamusaidia asimame na aendelee kutembea mu barabara ya uzima. Kwa hiyo, kila wakati wenye tunafariji ndugu ao dada yetu, tunaonyesha kama tunamupenda. (2 Ko. 7:6, 7, 13.) Kuko uhusiano wa karibu sana kati ya kusikilia mutu huruma na kumufariji. Namna gani? Kama tunasikilia mutu huruma tutachochewa kumufariji na kujikaza kumusaidia. Kwa hiyo, kwanza tunasikia huruma na kisha tunafariji. Ona namna Paulo anaonyesha uhusiano wenye kuwa kati ya huruma ya Yehova na faraja yenye anatoa. Paulo anasema kama Yehova ni “Baba wa rehema nyingi na Mungu wa faraja yote.”—2 Ko. 1:3. w23.11 9-10 fu. 8-10
Siku ya Pili, 22 Mwezi wa 7
Tufurahi basi hata kama tuko katika taabu.—Ro. 5:3.
Wafuasi wote wa Yesu wanaweza kutazamia kama watapata mateso. Tuone mufano wa mutume Paulo. Aliambia hivi Watesalonike: “Wakati tulikuwa pamoja na ninyi, tulikuwa tunawaambia mbele ya wakati kwamba tutapata taabu, na ni vile mambo yametokea.” (1 Te. 3:4) Na aliandikia hivi Wakorinto: “Hatutaki mukose kujua, ndugu, juu ya taabu yenye tulipata . . . Hatukukuwa na uhakika kabisa hata juu ya uzima wetu.” (2 Ko. 1:8; 11:23-27) Leo pia Wakristo wanaweza kutazamia kama watapata aina fulani ya taabu. (2 Ti. 3:12) Kadiri unamuamini Yesu na kuendelea kumufuata, pengine marafiki na watu wa familia wamekutendea mubaya. Je, umepata matatizo ku kazi juu unaazimia kuendelea kuwa munyoofu mu mambo yote? (Ebr. 13:18) Umepata upinzani kutoka kwa wakubwa wa serikali juu unahubiria wengine kuhusu tumaini yako? Ikuwe unapambana na taabu ya namna gani, kumbuka kama Paulo alisema kwamba tunapaswa kufurahi. w23.12 10-11 fu. 9-10
Siku ya Tatu, 23 Mwezi wa 7
Mumeniletea shida kubwa.—Mwa. 34:30.
Yakobo alipata magumu mingi. Watoto wawili wa Yakobo, Simeoni na Lawi, hawakuheshimisha familia yao na jina ya Yehova. Tena, Raheli, bibi mupendwa wa Yakobo alikufa wakati alikuwa nazala mutoto wao wa pili. Zaidi ya ile, wakati kulikuwa njala kali, Yakobo mwenye alikuwa alishazeeka, alilazimika kuenda mu inchi ya Misri. (Mwa. 35:16-19; 37:28; 45:9-11, 28) Yakobo hakuacha kumutumainia Yehova na ahadi zake hata kama alipata ile magumu yote; na Yehova hakumuacha. Kwa mufano, aliendelea kumubariki kwa kumupatia vitu mingi. Pima tena kuwazia namna Yakobo alipaswa kumushukuru Yehova wakati alionana tena na Yosefu, mwenye alikuwa nawazia kama alikufaka zamani! Urafiki wenye Yakobo alikuwa nao pamoya na Yehova ulimusaidia avumilie ile magumu yote. (Mwa. 30:43; 32:9, 10; 46:28-30) Kama tunaendelea kuwa na urafiki wa karibu pamoya na Yehova, tunaweza pia kuvumilia magumu yenye haitazamiwe. w23.04 15 fu. 6-7
Siku ya Ine, 24 Mwezi wa 7
Yehova ni Muchungaji wangu. Sitakosa kitu.—Zb. 23:1.
Zaburi ya 23 ni wimbo wenye kuonyesha kabisa kama Yehova iko na upendo na anatuhangaikia. Daudi, muandikaji wa ile zaburi, anazungumuzia uhusiano wenye nguvu wenye kuwa kati yake na Muchungaji wake Yehova. Daudi alijisikia kuwa salama juu aliacha Yehova amuongoze na alimutegemea kabisa. Daudi alijua kama upendo wa Yehova utaendelea kumufuata siku zote za maisha yake. Ni nini ilimuhakikishia vile? Daudi aliona kuwa Yehova anamuhangaikia kwa sababu sikuzote alimupatia mambo yenye alikuwa nayo lazima. Daudi alijua pia kama Yehova ni Rafiki yake na kama alimukubali. Njo maana alikuwa hakika kama hata nini itokee, Yehova angeendelea kumupatia mambo yenye alikuwa nayo lazima. Juu Daudi alikuwa hakika kama Yehova alimupenda sana na kama angemuhangaikia, ile ilifanya asilemewe na mahangaiko, lakini akuwe na furaha na akuwe mwenye kutosheka.—Zb. 16:11. w24.01 29 fu. 12-13
Siku ya Tano, 25 Mwezi wa 7
Niko pamoja na ninyi sikuzote mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.—Mt. 28:20.
Tangu Vita ya Pili ya Ulimwengu, watu wa Yehova mu inchi za mingi, wanafurahia amani na uhuru kwa kiasi fulani, na ile inawasaidia waendelee kufanya kazi ya kuhubiri. Kwa kweli, kazi ya kuhubiri imekuwa na matokeo ya muzuri kabisa. Leo ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza wanaendelea kufuata muongozo wa Kristo. Wanapenda muongozo wenye wanatolea ndugu na dada upatane na mawazo ya Yehova. Na wanatumia waangalizi wa muzunguko na wazee ili kutolea makutaniko ule muongozo. Wazee watiwa-mafuta wako katika “mukono [wa Kristo ] wa kuume.” (Ufu. 2:1) Kwa kweli, wale wazee ni watu wenye hawakamilike na wanafanyaka makosa. Musa na Yoshua na hata mitume, walifanya pia makosa wakati fulani. (Hes. 20:12; Yos. 9:14, 15; Ro. 3:23) Lakini, Yesu anaendelea kuongoza mutumwa muaminifu na mwenye busara, na wazee wenye wamewekwa, na ataendelea kufanya vile. Kwa hiyo, tuko na sababu za muzuri sana za kutegemea muongozo wenye anatupatia kupitia wale wenye ameweka ili watuongoze. w24.02 23-24 fu. 13-14
Siku ya Posho, 26 Mwezi wa 7
Mukuwe waigaji wa Mungu, kama watoto wapendwa.—Efe. 5:1.
Leo, tunaweza kumusifu Yehova kwa kuzungumuza kwa upendo, kwa shukrani, na kwa uchangamufu kumuhusu. Wakati tuko mu mahubiri, tunakumbuka kama kusudi yetu kubwa ni kusaidia watu wamukaribie Yehova, na kuwasaidia waone Baba yetu mwenye upendo vile siye tunamuona. (Yak. 4:8) Tunafurahia kuonyesha watu mambo yenye Biblia inasema juu ya Yehova, namna inafunua upendo wake, haki, hekima, nguvu, na sifa zake zingine za muzuri. Pia tunamusifu Yehova na kumufurahisha wakati tunajikaza kumuiga. Wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tuko tofauti na watu wa mu huu ulimwengu. Watu wanaweza kuona namna tuko tofauti na wanaweza kutuuliza ni juu ya nini tuko vile. (Mt. 5:14-16) Na wakati tuko nao mu maisha yetu ya kila siku, tunaweza kuwafasiria juu ya nini tunatendaka vile. Matokeo ni kwamba, watu wenye moyo muzuri wanachochewa kumukaribia Yehova. Wakati tunasifu Yehova mu zile njia, tunafurahisha sana moyo wake.—1 Ti. 2:3, 4. w24.02 10 fu. 7
Siku ya Yenga, 27 Mwezi wa 7
Uweze kutia moyo . . . na kukaripia.—Tit. 1:9.
Ili kuwa mwanaume Mukristo mwenye kukomaa kiroho, uko na lazima ya kujifunza ufundi fulani wa maana. Ile itakusaidia kutimiza migao yako mu kutaniko, kupata kazi ya kukutegemeza weye na familia yako, na kuwa na uhusiano wa muzuri pamoja na wengine. Kwa mufano, ujifunze kusoma na kuandika muzuri. Biblia inasema kama mutu mwenye furaha na mwenye anapata matokeo ya muzuri anapitisha wakati kila siku na iko anasoma na kufikiri sana juu ya Neno ya Mungu. (Zb. 1:1-3) Kwa kusoma Biblia kila siku, atafikia kujua namna ya Yehova ya kuona mambo, na ile inaweza kumusaidia kufikiri muzuri. (Mez. 1:3, 4) Ndugu na dada wako na lazima ya wanaume wenye uzoefu wa kuwapatie maagizo na mashauri yenye kutegemea Biblia. Kujua kusoma na kuandika muzuri kunaweza kukusaidia utayarishe hotuba na maelezo yenye kujenga. Ile inaweza pia kukusaidia kuandika maelezo fulani ya maana wakati uko unajifunza Biblia, ile mambo yenye uliandika inaweza kukusaidia kujenga imani yako na kutia wengine moyo. w23.12 26-27 fu. 9-11
Siku ya Kwanza, 28 Mwezi wa 7
Ule mwenye kuwa katika umoja na ninyi ni mukubwa kuliko ule mwenye kuwa katika umoja na ulimwengu.—1 Yo. 4:4.
Wakati unaogopa, utafakari juu ya mambo yenye Yehova atafanya wakati wenye kuya wakati Shetani hatakuwa tena. Onyesho fulani ku mukusanyiko wa eneo wa 2014, ulionyesha baba fulani mwenye alikuwa nazungumuza na familia yake juu ya namna 2 Timoteo 3:1-5 inaweza kusomwa ikiwa ilikuwa inatabiri namna mambo itakuwa mu Paradiso: “Mu ulimwengu mupya mutakuwa nyakati za furaha. Kwa maana watu watakuwa wenye kupendana, wenye kupenda mambo ya kiroho, wenye kiasi, wanyenyekevu, wenye kumusifu Mungu, wenye kutii wazazi, wenye shukrani, washikamanifu, wenye kupenda sana watu wa familia yao, wenye kupenda makubaliano, wenye kusema mambo ya muzuri juu ya wengine, wenye kujizuia, wapole, wenye kupenda wema, wenye kutumainika, wenye kuwa tayari kusikia, wenye kujishusha, wenye kumupenda Mungu kuliko kupenda raha, wenye wanachochewa na ushikamanifu kwa Mungu; na weye ushikamane na watu wa namna ile.” Unazungumuzaka na watu wa familia yako ao waamini wenzako juu ya namna maisha itakuwa mu ulimwengu mupya? w24.01 6 fu. 13-14
Siku ya Pili, 29 Mwezi wa 7
Nimekukubali.—Lu. 3:22.
Inatia moyo sana kujua kama Yehova anakubali watu wake wakiwa kikundi! Biblia inasema: “Yehova anafurahia watu wake.” (Zb. 149:4) Lakini, wakati fulani kuko Wakristo wenye wanaweza kuvunjika moyo na kujiuliza hivi: ‘Yehova ananikubali na miye?’ Watumishi fulani waaminifu wa Yehova wa zamani walijiuliza pia vile wakati fulani. (1 Sa. 1:6-10; Yob. 29:2, 4; Zb. 51:11) Biblia inaonyesha wazi kama wanadamu wenye hawakamilike wanaweza kukubaliwa na Yehova. Namna gani? Tunapaswa kukubali Yesu Kristo na kubatizwa. (Yoh. 3:16) Kwa kufanya vile tunaonyesha waziwazi kama tumetubu zambi zetu na tumemuahidi Mungu kama tutafanya mapenzi yake. (Mdo. 2:38; 3:19) Yehova anafurahi sana wakati tunafanya ile mambo ili kuwa marafiki wake wa karibu. Wakati tunaendelea kufanya yetu yote ili kuheshimia naziri yetu ya kujitoa kwake, Yehova anatukubali na kutuona kuwa marafiki wake.—Zb. 25:14. w24.03 26 fu. 1-2
Siku ya Tatu, 30 Mwezi wa 7
Hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.—Mdo. 4:20.
Tunaweza pia kuiga wanafunzi wa Yesu kwa kuendelea kuhubiri hata kama wenye mamlaka wanatukataza kufanya vile.Tuko hakika kama Yehova atatusaidia kutimiza utumishi wetu. Kwa hiyo, umuombe Yehova uhodari na hekima na akusaidie ili uvumilie magumu. Wengi kati yetu wako napambana na magumu ya kimwili ao ya kihisia, magumu ya kupoteza mupendwa wao, magumu fulani mu familia, mateso, ao magumu ingine. Na mambo sawa vile, magonjwa ya kuambukiza na vita imefanya ikuwe nguvu kuvumilia magumu mingi kati ya ile. Umufungulie Yehova moyo wako. Umuambie hali yako sawa vile tu unaweza kumuambia rafiki yako wa karibu sana. Ukuwe hakika kama Yehova “atatenda kwa ajili yako. (Zb. 37:3, 5) Kuendelea kusali kutakusaidia “uvumilie chini ya taabu.” (Ro. 12:12) Yehova anajua mambo yenye watumishi wake wako napambana nayo. “Anasikia kilio chao cha kuomba musaada.”—Zb. 145:18, 19. w23.05 5-6 fu. 12-15
Siku ya Ine, 31 Mwezi wa 7
Muendelee kuhakikisha ni nini yenye kukubaliwa kwa Bwana.—Efe. 5:10.
Wakati tunataka kukamata maamuzi ya maana, ni muzuri tutafute kujua “mapenzi ya Yehova” na kisha tutende kulingana nayo. (Efe. 5: 17) Wakati tunapata kanuni ya Biblia yenye inahusu hali yetu, ni sawa vile tuko natafuta mawazo ya Yehova kuhusu ile jambo. Na wakati tunatumikisha ile kanuni, tutaweza kukamata maamuzi ya muzuri. “Ule muovu,” adui yetu Shetani, anapenda tutumie wakati wetu wote ili kufuatilia mambo ya huu ulimwengu na tukose wakati wa kumutumikia Mungu. (1 Yo. 5:19) Inaweza kuwa mwepesi kwa Mukristo kutia pa nafasi ya kwanza vitu vya kimwili, elimu ya huu ulimwengu, ao kazi kuliko kutia utumishi wake kwa Yehova pa nafasi ya kwanza. Kama ile inatokea, inaweza kuonyesha kama ule Mukristo iko nachochewa na mawazo ya ulimwengu. Kusema kweli, ile mambo haiko ya mubaya, lakini haipaswe kuwa pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu. w24.03 24 fu. 16-17