Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • es25 uku. 77-87
  • Mwezi wa 8

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mwezi wa 8
  • Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Siku ya Tano, 1 Mwezi wa 8
  • Siku ya Posho, 2 Mwezi wa 8
  • Siku ya Yenga, 3 Mwezi wa 8
  • Siku ya Kwanza, 4 Mwezi wa 8
  • Siku ya Pili, 5 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tatu, 6 Mwezi wa 8
  • Siku ya Ine, 7 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tano, 8 Mwezi wa 8
  • Siku ya Posho, 9 Mwezi wa 8
  • Siku ya Yenga, 10 Mwezi wa 8
  • Siku ya Kwanza, 11 Mwezi wa 8
  • Siku ya Pili, 12 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tatu, 13 Mwezi wa 8
  • Siku ya Ine, 14 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tano, 15 Mwezi wa 8
  • Siku ya Posho, 16 Mwezi wa 8
  • Siku ya Yenga, 17 Mwezi wa 8
  • Siku ya Kwanza, 18 Mwezi wa 8
  • Siku ya Pili, 19 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tatu, 20 Mwezi wa 8
  • Siku ya Ine, 21 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tano, 22 Mwezi wa 8
  • Siku ya Posho, 23 Mwezi wa 8
  • Siku ya Yenga, 24 Mwezi wa 8
  • Siku ya Kwanza, 25 Mwezi wa 8
  • Siku ya Pili, 26 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tatu, 27 Mwezi wa 8
  • Siku ya Ine, 28 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tano, 29 Mwezi wa 8
  • Siku ya Posho, 30 Mwezi wa 8
  • Siku ya Yenga, 31 Mwezi wa 8
Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025
es25 uku. 77-87

Mwezi wa 8

Siku ya Tano, 1 Mwezi wa 8

Magumu ya mwenye haki ni mengi, lakini Yehova anamuokoa katika magumu hayo yote.​—Zb. 34:19.

Ona mambo mbili ya maana yenye kupatikana mu ile zaburi: (1) Mwenye haki anapataka magumu. (2) Yehova anatuokoaka wakati tunapata magumu. Yehova anafanyaka nini ili kutuokoa? Anatusaidiaka tukuwe na mutazamo wenye kufaa juu ya maisha. Yehova anatutolea ahadi ya kama tutakuwa na maisha yenye furaha wakati tuko namutumikia, lakini ile haimaanishe kama hatutapata magumu leo. (Isa. 66:14) Anatuambia tukaze akili yetu juu ya wakati yenye kuya, ni kusema, wakati yenye tutakuwa na maisha yenye anapenda tufurahie milele. (2 Ko. 4:16-18) Kwa sasa, iko natusaidia ili tuendelee kumutumikia kila siku. (Omb. 3:22-24) Mifano ya waabudu waaminifu wa Yehova wa zamani na wa leo inaweza kutufundisha nini? Tunaweza kupata magumu fulani yenye haitazamiwe. Lakini kama tunamutegemea Yehova, bila shaka, ataendelea kutusaidia.​—Zb. 55:22. w23.04 14-15 fu. 3-4

Siku ya Posho, 2 Mwezi wa 8

Kwa mamlaka zenye kuwa kubwa.​—Ro. 13:1.

Mufano wa Yosefu na Maria unaweza kutufundisha mambo mingi. Walikuwa tayari kutii wenye mamlaka hata wakati haikukuwa mwepesi kwao kufanya vile. (Lu. 2:1-6) Wakati Maria alikuwa na mimba ya karibu miezi kenda, walikutana na hali yenye ilijaribu utii wao. Mutawala wa Roma Mwezi wa 80, aliamuru watu wote waandikishwe. Yosefu na Maria walipaswa kuenda kujiandikisha Betlehemu, safari ya kilometre 150 mu njia ya milima-milima. Ile safari haingekuwa mwepesi, zaidi sana kwa Maria. Pengine wangekuwa na wasiwasi juu ya usalama wa Maria na wa mutoto wao mwenye alikuwa angali mu tumbo. Mambo ingekuwa namna gani kama maumivu ya kuzala ingeanza na wako? Mu tumbo ya Maria mulikuwa mutoto mwenye angefikia kuwa Masiya. Ile ingekuwa sababu yenye ingefanya wasitii serikali? Yosefu na Maria hawakuruhusu ile mambo yenye ilikuwa nawahangaisha iwazuie kutii ile sheria. Yehova alibariki utii wao. Maria alifika salama Betlehemu, akazaa mutoto mwenye afya ya muzuri, na hata akasaidia kutimiza unabii wa Biblia!​—Mik. 5:2. w23.10 8 fu. 9; 9 fu. 11-12

Siku ya Yenga, 3 Mwezi wa 8

[Tutuiane] moyo.​—Ebr. 10:25.

Tuseme nini kama unaogopaka kutoa maelezo ku mikutano? Inaweza kuwa muzuri ujitayarishe muzuri. (Mez. 21:5) Kama unaelewa muzuri habari, itakuwa mwepesi kwako kutoa maelezo. Tena, utayarishe maelezo ya mufupi. (Mez. 15:23; 17:27) Maelezo ya mufupi itakusaidia usiogope sana wakati uko naitoa. Wakati unatoa maelezo ya mufupi mu maneno yako, utaonyesha kama ulijitayarisha muzuri na kama ulielewa habari muzuri. Tuseme nini kama ungali naogopa kutoa maelezo mara mingi kisha kutumikisha mapendekezo fulani kati ya ile mapendekezo? Ukuwe hakika kama Yehova atasamini bidii yako ya kutoa maelezo. (Lu. 21:1-4) Yehova hatuombe kufanya mambo yenye kupita uwezo wetu. (Flp. 4:5) Ujue mambo yenye unaweza kufanya, ujiwekee muradi wa kuifanya, na usali juu ya kuwa na moyo wenye kutulia. Ku mwanzo, unaweza kujiwekea muradi wa kutoa tu jibu moya ya mufupi. w23.04 21 fu. 6-8

Siku ya Kwanza, 4 Mwezi wa 8

Kuvaa bamba la kifua . . . na . . . kofia ya chuma.​—1 Te. 5:8.

Mutume Paulo anatulinganisha na maaskari wenye kuwa macho na wenye kuvala muzuri kwa ajili ya vita. Askari anapaswa kuwa tayari kupigana kila wakati kama vita inaanza. Ni vile pia kwetu. Tunaendelea kuwa tayari kwa ajili ya siku ya Yehova kwa kuvala bamba ya kifua ya imani, upendo, na kofia ya chuma ya tumaini. Bamba ya kifua ilikuwa nalinda moyo wa askari. Imani na upendo inalindaka moyo wetu wa mufano. Njo sifa zenye zitatusaidia tuendelee kumutumikia Mungu na kumufuata Yesu. Juu tuko na imani, tuko hakika kama Yehova atatupatia zawabu kama tunaendelea kumutafuta kwa moyo wote. (Ebr. 11:6) Imani itatusaidia tuendelee kuwa washikamanifu kwa Kiongozi wetu, Yesu, hata kama inaomba tuvumilie magumu. Tunaweza kufanya imani yetu ikuwe nguvu ili tuweze kuvumilia kwa kujifunza mambo fulani kupitia mifano ya watu wa leo wenye waliendelea kuwa washikamanifu ijapokuwa mateso ao magumu ya kupata makuta. Na tunaweza kuepuka hatari ya kupenda sana makuta na vitu vya kimwili kama tunaiga wale wenye walifanya maisha yao ikuwe mwepesi ili kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza. w23.06 10 fu. 8-9

Siku ya Pili, 5 Mwezi wa 8

Mwenye anaangalia mawingu hatavuna.​—Muh. 11:4.

Mutu mwenye kuwa na sifa ya kujizuia anakuwaka na uwezo wa kuongoza hisia na matendo yake. Inaomba kuwa na ile sifa ili kufikia miradi yetu, zaidi sana kama muradi wetu ni wa nguvu ao kama hatuna hamu ya kuufikia. Tusisahau kama kujizuia ni sifa ya maana na ni sehemu ya tunda ya roho. Kwa hiyo, umuombe Yehova akupatie roho yake takatifu ili uikomalishe. (Lu. 11:13; Gal. 5:22, 23) Usichunge mupaka hali ikuwe muzuri sana. Mu hii dunia, pengine ile haitawezekana. Kwa hiyo, kama tuko nachunga hali ikuwe muzuri sana, pengine hatutawezaka kufikia miradi yetu. Wakati fulani, tunaweza kukosa hamu ya kufikia muradi kama unaonekana sawa vile ni wa nguvu sana. Kama ile njo hali yako, unawaza nini kama unagawanya ule muradi mu sehemu kidogo-kidogo? Kama muradi wako ni wa kukomalisha sifa fulani, hauone kama ni muzuri uionyeshe mu njia za kidogo-kidogo? Na kama muradi wako ni wa kusoma Biblia yote, unawaza namna gani kama unapanga kuisoma mu wakati kidogo-kidogo? w23.05 29 fu. 11-13

Siku ya Tatu, 6 Mwezi wa 8

Njia ya wenye haki iko kama mwangaza wenye kungaa wa asubuiwenye kungaa zaidi na zaidi mupaka muchana kamili.​—Mez. 4:18.

Mu hizi siku za mwisho, Yehova anaendelea kutumia tengenezo yake ili kutupatia maagizo yenye kutoka mu Neno yake juu tuendelee kutembea mu “Njia ya Utakatifu.” (Isa. 35:8; 48:17; 60:17) Tunaweza kusema kama wakati mutu anakubali kujifunza Biblia, anapata nafasi ya kuanza kutembea mu “Njia ya Utakatifu.” Watu fulani wanatembeaka kidogo tu mu ile njia kubwa kisha wanaiacha. Wengine wanaazimia kuendelea kutembea mule mupaka wafike ku mwisho wa safari yao. Njo wapi? Kwa wale wenye kuwa na tumaini ya kuenda mbinguni, “Njia ya Utakatifu” itawafikisha mu “paradiso ya Mungu” mbinguni. (Ufu. 2:7) Kwa wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi ku dunia, ile njia kubwa itawafikisha ku mwisho wa utawala wa miaka 1000 wa Kristo, wakati watu wote watakuwa wakamilifu. Leo kama uko natembea mu ile njia, tafazali, usiangalie nyuma na usiiache mupaka ufike ku mwisho wa safari yako, ni kusema, mu dunia mupya. w23.05 17 fu. 15; 19 fu. 16-18

Siku ya Ine, 7 Mwezi wa 8

Sisi tunapenda, kwa sababu alitupenda kwanza.​—1 Yo. 4:19.

Wakati unafikiria mambo yote yenye Yehova alishafanya kwa ajili yako, unajisikia tu ujitoe kwake. (Zb. 116:12-14) Bila shaka Biblia haikosee wakati inamuita Yehova Mupaji wa “kila zawadi ya muzuri na kila zawadi kamilifu.” (Yak. 1:17) Zawadi kubwa zaidi kati ya zawadi zenye Yehova ametutolea ni zabihu ya Mwana wake Yesu. Waza kidogo! Bei ya ukombozi imefanya iwezekane ukuwe na urafiki wa karibu pamoya na Yehova. Na inafanya ukuwe na tumaini ya kuishi milele. (1 Yo. 4:9, 10) Kujitoa kwa Yehova ni njia ya kuonyesha shukrani juu ya ile tendo kubwa zaidi ya upendo, na juu ya baraka zingine za mingi zenye amekupatia.​—Kum. 16:17; 2 Ko. 5:15. w24.03 5 fu. 8

Siku ya Tano, 8 Mwezi wa 8

Mutu mwenye kutembea katika unyoofu wake anamuogopa Yehova.​—Mez. 14:2.

Tuko najisikia sawa vile Loti wakati tunaona mwenendo mubaya wa watu leo. “Alihuzunishwa sana na mwenendo mupotovu wa bila haya wa watu wenye kuvunja sheria” juu alijua kama Baba yetu wa mbinguni anachukia mwenendo mubaya. (2 Pe. 2:7, 8) Juu alimuogopa Mungu na kumupenda, Loti alichukia mwenendo mubaya wa watu wenye aliishi nao. Siye pia, tuko naishi na watu wenye kuwa na mwenendo mubaya. Hata vile, tunaweza kuendelea kuwa na mwenendo safi kama tunamupenda Mungu na kumuogopa mu njia yenye kufaa. Yehova anatusaidia kufanya vile kupitia kitia-moyo yenye tunapata mu kitabu ya Mezali. Wakristo wote, ni kusema, wanaume na wanamuke, vijana na wazee, wanaweza kabisa kupata faida kwa kuchunguza mashauri ya hekima yenye kuwa mu ile kitabu. Wakati tunamuogopa Yehova tunakuwa waangalifu juu tusiachlie tabia fulani ya mubaya. w23.06 20 fu. 1-2; 21 fu. 5

Siku ya Posho, 9 Mwezi wa 8

Kama mutu yeyote anataka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe, achukue muti wake wa mateso kila siku na aendelee kunifuata.​—Lu. 9:23.

Pengine umepambana na upinzani wa watu wa familia, ao pengine umeacha vitu fulani vya kimwili ili kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza. (Mt. 6:33) Kama ni vile, unaweza kuwa hakika kama Yehova anaona matendo yako ya uaminifu. (Ebr. 6:10) Na inawezekana kabisa umejionea utimizo wa hii maneno ya Yesu: “Hakuna mutu mwenye ameacha nyumba ao ndugu ao dada ao mama ao baba ao watoto ao mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya habari njema mwenye hatapata mara mia moja (100) sasa katika kipindi hiki—nyumba, ndugu, dada, mama, watoto, mashamba, pamoja na mateso—na katika mupangilio wa mambo wenye unakuja, uzima wa milele.” (Mk. 10:29, 30) Baraka zenye umepata ni za mingi sana kupita jambo yoyote yenye umejiima.​—Zb. 37:4. w24.03 9 fu. 5

Siku ya Yenga, 10 Mwezi wa 8

Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote Naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.​—Mez. 17:17.

Wakati Wakristo wa mu Yudea walipigwa na njala kali. wandugu wa mu kutaniko ya Antiokia ya Siria. “Wakaamua, kila mumoja kulingana na uwezo wake, kutuma misaada kwa ndugu wenye kuishi Yudea.” (Mdo. 11:27-30) Hata kama wale ndugu na dada wenye walipigwa na njala walikuwa naishi mbali, Wakristo wa Antiokia waliazimia kuwasaidia. (1 Yo. 3:17, 18) Leo, siye pia tunaweza kuonyesha huruma wakati tunasikia kama waabudu wenzetu wamepatwa na misiba. Tunaweza kuonyesha kama tuko tayari kufanya vile kwa kuambia wazee kama tunapenda kusaidia mu kazi fulani, kwa kutoa michango juu ya kutegemeza kazi ya mu dunia yote, ao kwa kusali kwa ajili ya wale ndugu wenye wamepatwa na misiba. Pengine ndugu na dada zetu watakuwa na lazima ya musaada ili kupata mambo yenye wako nayo lazima juu waokoke. Wakati Kristo Yesu, Mufalme wetu, atakuya kuhukumu watu, ni muzuri atukute tayari tuko naonyesha huruma na atuambie hivi: Mukuye “muriti Ufalme.”​—Mt. 25:34-40. w23.07 4 fu. 9-10; 6 fu. 12

Siku ya Kwanza, 11 Mwezi wa 8

Usawaziko wenu ujulikane kwa watu wote.​—Flp. 4:5.

Yesu alimuiga Yehova kwa kuwa na usawaziko. Alitumwa hapa ku dunia ili kuhubiria “kondoo wenye kupotea wa nyumba ya Israeli.” Lakini, alionyesha kama alikuwa na usawaziko wakati alikuwa natimiza ule mugao. Siku moya, mwanamuke fulani mwenye hakukuwa Mwisraeli alimuomba aponyeshe mutoto wake mwanamuke mwenye alikuwa “anasumbuliwa sana na pepo muchafu.” Yesu alimusikilia huruma ule mwanamuke na aliponyesha mutoto wake. (Mt. 15:21-28) Fikiria mufano ingine. Ku mwanzo wa utumishi wake, Yesu alisema hivi: “Kila mutu mwenye ananikana . . . , mimi pia nitamukana.” (Mt. 10:33) Je, Yesu alimukana Petro, mwenye alimukanaka mara tatu? Hapana. Alijua kama Petro alitubu kikweli na alikuwa muaminifu. Kisha kufufuliwa, Yesu alimutokea Petro na inawezakana kabisa alimuhakikishia kama alikuwa alishamusamehe na kama alimupenda (Lu. 24:33, 34) Yehova na Yesu wako na usawaziko. Alafu siye? Yehova anatazamia tukuwe na usawaziko. w23.07 21 fu. 6-7

Siku ya Pili, 12 Mwezi wa 8

Kifo hakitakuwa tena.​—Ufu. 21:4.

Namna gani unaweza kuhakikishia wale wenye kuwa na mashaka kama ahadi ya Mungu ya kuleta Paradiso itatimia? Kwanza, ni Yehova mwenyewe njo ametoa ile ahadi. Kitabu ya Ufunuo inasema hivi: “Ule mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme akasema: “Angalia! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’” Iko na hekima, iko na nguvu, na anapenda kabisa kutimiza ile ahadi. Pili, iko hakika kabisa kama ahadi yake itatimia njo maana anaizungumuzia mu njia yenye kuonyesha kama ilishatimia. Njo maana anasema hivi: “Maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli. . . . Yamefanyika!” Tatu, wakati Yehova anaanza kufanya kitu fulani anaendelea mupaka kifikie mwisho, sawa vile maneno “mimi ndiye Alfa na Omega” inaonyesha. (Ufu. 21:6) Yehova ataonyesha kama Shetani ni muongo na ameshidwa. Kwa hiyo wakati mutu anasema, “Ile ni ndoto tu,” umusomee na kumufasiria Ufunuo 21:5, 6. Umuonyeshe namna Yehova amehakikisha kuwa ahadi yake itatimia kwa kuitilia yeye wenyewe sinyatire ya mufano.​—Isa. 65:16. w23.11 7 fu. 18-19

Siku ya Tatu, 13 Mwezi wa 8

Nitakufanya kuwa taifa kubwa.​—Mwa. 12:2.

Yehova alimupatia Abrahamu ile ahadi wakati alikuwa na miaka 75 na hakukuwa na mutoto. Abrahamu alijionea utimizo wa ile ahadi? Hapana yote. Kisha kutambuka Muto Efrati na kisha kungoya miaka 25, Abrahamu alijionea muujiza wa kuzaliwa kwa mutoto yake Isaka, na kisha miaka ingine 60, wajukuu wake, Esau na Yakobo walizaliwa. (Ebr. 6:15) Lakini, Abrahamu hakujioneaka namna wazao wake walifikia kuwa taifa kubwa na kuriti Inchi ya Ahadi. Hata vile, ule mwanaume muaminifu alikuwa na urafiki wa karibu pamoya na Muumbaji wake. (Yak. 2:23) Wazia furaha yenye Abrahamu atakuwa nayo wakati atafufuliwa na kujua kama imani yake na uvumilivu wake njo ilifanya Yehova abariki mataifa yote! (Mwa. 22:18) Ile inatufundisha nini? Pengine leo hatutajionea kutimizwa kwa ahadi zote za Yehova. Lakini, kama tuko na uvumilivu sawa vile wa Abrahamu, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatubariki sasa na atatubariki hata zaidi mu dunia mupya yenye anaahidi.​—Mk. 10:29, 30. w23.08 24 fu. 14

Siku ya Ine, 14 Mwezi wa 8

Katika ule wakati wenye alikuwa anamutafuta Yehova, Mungu wa kweli alimufanya apate matokeo ya muzuri.​—2 Ny. 26:5.

Mufalme Uzia alikuwa munyenyekevu wakati alikuwa kijana. Alijifunza “kumuogopa Mungu wa kweli.” Aliishi miaka 68 na Yehova alimubariki mu sehemu kubwa ya maisha yake. (2 Ny. 26:1-4) Uzia alishinda maadui wengi na alihakikisha kama muji wa Yerusalemu unalindwa muzuri zaidi. (2 Ny. 26:6-15) Bila shaka, Uzia alifurahia mambo yote yenye Mungu alimusaidia kufanya. (Muh. 3:12, 13) Mufalme Uzia alizoea kupatia wengine maagizo. Je, ile ilimufanya awaze kama anaweza kufanya jambo yoyote yenye anapenda? Siku moja Uzia aliamua kuingia mu hekalu ya Yehova, na kwa kimbelembele alijaribu kuchoma uvumba ku mazabahu, jambo yenye wafalme hawakuruhusiwa kufanya. (2 Ny. 26:16-18) Kuhani Mukubwa Azaria alijaribu kumukataza, lakini Uzia alikasirika sana. Jambo ya kuhuzunisha ni kama Uzia hakuendelea kuwa muaminifu, na Yehova alimupatia malipizi kwa kumupiga ugonjwa wa ukoma. (2 Ny. 26:19-21) Bila shaka, maisha yake ingekuwa tofauti kabisa kama angeendelea kuwa munyenyekevu! w23.09 10 fu. 9-10

Siku ya Tano, 15 Mwezi wa 8

Akajitenga, kwa kuogopa wale wa kikundi cha wenye kutahiriwa.​—Gal. 2:12.

Hata kisha kuwa Mukristo mutiwa-mafuta, mutume Petro aliendelea kupambana na uzaifu wake. Mu mwaka wa 36 K.K.Y., Petro alikuwa pale wakati Kornelio, Mutu wa Mataifa mwenye hatahiriwe, alitiwa mafuta na roho takatifu. Ile ilionyesha wazi kama “Mungu hana ubaguzi” na kama Watu wa Mataifa wanaweza kuingia mu kutaniko ya Kikristo. (Mdo. 10:34, 44, 45) Kisha pale, Petro alijisikia huru kula pamoya na Watu wa Mataifa, jambo yenye hangefanyaka zamani. Lakini, Wakristo fulani Wayahudi waliona kama Wayahudi hawapaswe kula pamoya na Watu wa Mataifa. Wakati Wakristo fulani Wayahudi wenye walikuwa na ile mawazo walikuya Antiokia, Petro aliacha kula pamoya na ndugu zake wenye hawakukuwa Wayahudi. Pengine alifanya vile juu aliogopa kukwaza Wakristo Wayahudi. Mutume Paulo aliona ule unafiki na alimukaripia Petro mbele ya watu wote. (Gal. 2:13, 14) Hata kama Petro aliangukia tena mu uzaifu wake, hakuvunjika moyo na aliendelea kujikaza. w23.09 22 fu. 8

Siku ya Posho, 16 Mwezi wa 8

Atawafanya ninyi musitikisike.​—1 Pe. 5:10.

Wakati unajichunguza muzuri, unaweza kuona mambo yenye pengine unapaswa kufanyia kazi. Lakini usivunjike moyo. “Bwana ni mwenye fazili,” na atakusaidia kufanya maendeleo. (1 Pe. 2:3) Mutume Petro anatuhakikishia hivi: “Mungu . . . yeye mwenyewe atamaliza mazoezi yenu. Atawafanya kuwa imara.” Ku mwanzo Petro aliona kama hastahili kuwa pamoya na Mwana wa Mungu. (Lu. 5:8) Lakini, juu Yehova na Yesu walimutegemeza kwa upendo, Petro aliendelea kuwa mufuasi wa Kristo. Na kwa hiyo, Petro alikubaliwa “kuingia katika Ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.” (2 Pe. 1:11) Ile ilikuwa baraka kubwa! Kama unaendelea kujikaza kumutumikia Yehova kama vile Petro alifanya na unaacha Yehova akuzoeze, weye pia utapata baraka ya uzima wa milele. “Utafikia kusudi la imani yako, wokovu wako.”​—1 Pe. 1:9. w23.09 31 fu. 16-17

Siku ya Yenga, 17 Mwezi wa 8

Mumuabudu Ule mwenye alifanya mbingu na dunia.​—Ufu. 14:7.

Tabenakulo ya zamani ilikuwa na kiwanja moya, ni kusema fasi kubwa yenye kuzungukwa na lupango kwenye makuhani walikuwa nafanyia kazi zao. Mazabahu kubwa ya shaba ya toleo ya kuteketezwa ilkuwa pia mu ile kiwanja, mulikuwa pia beseni ya shaba ya maji yenye makuhani walitumia ili kujisafisha mbele ya kufanya utumishi wao mutakatifu. (Kut. 30:17-20; 40:6-8) Leo, mbele ya kuenda mbinguni ili kuwa makuhani pamoya na Yesu, mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta wanatumika kwa uaminifu ku dunia mu kiwanja cha ndani cha hekalu ya kiroho. Ile beseni kubwa ya maji inakumbusha Wakristo watiwa-mafuta na Wakristo wengine wote kama ni jambo ya maana waendelee kuwa safi kiroho na waendelee kuwa na mwenendo safi. Sasa ni wapi njo “kundi kubwa” wanamutumikia Yehova? Mutume Yohana aliwaona “wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme,” chenye ku dunia kinalingana na kiwanja cha inje, kwenye “wanamutolea [Mungu] utumishi mutakatifu muchana na usiku katika hekalu lake.” (Ufu. 7:9, 13-15) Tunafurahi sana juu tuko na fasi yetu mu mupango wa Yehova wa ibada safi! w23.10 28 fu. 15-16

Siku ya Kwanza, 18 Mwezi wa 8

Kwa sababu ya ahadi ya Mungu, . . . [akakuwa] mwenye nguvu kwa imani yake.​—Ro. 4:20.

Njia ingine yenye Yehova anatumia ili kututia nguvu ni kupitia wazee. (Isa. 32:1, 2) Kwa hiyo, wakati uko na mahangaiko, elezea wazee kuhusu mahangaiko yako. Wakati wanakutolea musaada, ukuwe tayari kuukubali. Kupitia wazee Yehova anaweza kukutia nguvu. Tumaini yenye kuzungumuziwa mu Biblia yenye tuko nayo ya kuishi milele, ikuwe mu dunia yenye kuwa paradiso ao mbinguni mu Ufalme wa Mungu inaweza pia kutupatia nguvu. (Ro. 4:3, 18, 19) Inatupatia nguvu ya kuvumilia magumu, ya kuhubiri habari njema, na ya kutimiza migao mbalimbali mu kutaniko. (1 Te. 1:3) Ile tumaini njo ilipatiaka mutume Paulo nguvu. “Alikazwa,” “alivurugika,” “aliteswa,”“aliangushwa chini,” na hata maisha yake ilikuwa mu hatari. (2 Ko. 4:8-10) Paulo alipata nguvu ya kuvumilia kwa kukazia akili tunaini yake. (2 Ko. 4:16-18) Paulo alikazia akili tumaini yake ya kuishi milele mbinguni. Paulo alitafakari juu ya tunaini yake, na ile ilifanya ajisikie kuwa “anafanywa upya siku kwa siku.” w23.10 15-16 fu. 14-17

Siku ya Pili, 19 Mwezi wa 8

Yehova atapatia watu wake nguvu. Yehova atabariki watu wake kwa amani.​—Zb. 29:11.

Wakati ukonasali, fikiria kama huu njo wakati wa Yehova wa kujibia ombi yako. Tunaweza kuona kama ni lazima sala zetu zijibiwe palepale. Lakini, Yehova njo anajua wakati wenye kufaa zaidi wa kutusaidia. (Ebr. 4:16) Wakati hatupate palepale kitu yenye tuko naomba tunaweza kuwaza kama jibu ya Yehova ni ‘Hapana.’ Lakini jibu inaweza kuwa ni ‘Hapana kwa sasa.’ Kwa mufano ndugu kijana alisali ili apone. But his health did not improve.Yehova angemuponyesha kwa muujiza, Shetani angeweza kusema kama ule ndugu anaendelea kumutumikia Yehova juu tu alimuponyesha. (Yob. 1:9-11; 2:4) Zaidi ya ile, Yehova alishaweka wakati wenye ataponyesha magonjwa yote. (Isa. 33:24; Ufu. 21:3, 4) Mbele ile wakati ifike, hatuwezi kutazamia kama tutaponyeshwa kwa muujiza. Kwa hiyo, ule ndugu anaweza kumuomba Yehova amupatie nguvu na amupatie amani ya akili ili avumilie ugonjwa wake na aendelee kumutumikia kwa uaminifu. w23.11 24 fu. 13

Siku ya Tatu, 20 Mwezi wa 8

Hajatutendea kulingana na zambi zetu, Wala hajatulipa malipo yenye makosa yetu yanastahili.​—Zb. 103:10.

Samsoni alikuwa amefanya kosa kubwa, lakini hakuacha kufanya mapenzi ya Yehova. Alitafuta nafasi ya kutimiza mugao wenye Mungu alimupatia wa kupiganisha Wafilisti. (Amu. 16:28-30) Samsoni alimuomba hivi Yehova: “Uache nilipize kisasi juu ya Wafilisti.” Mungu wa kweli alijibia sala ya Samsoni, na kwa muujiza alimurudishia nguvu ya pekee yenye alikuwaka nayo. Matokeo ilikuwa nini? Ku ile tukio, Samsoni aliua Wafilisti wengi zaidi kuliko wenye alikuwa ameua mbele ya pale. Hata kama Samsoni alipata matokeo ya mubaya kwa sababu ya kosa yake, hakuacha kujikaza kufanya mapenzi ya Yehova. Na siye, hata kama tunafanya makosa na inaomba tukaripiwe ao tupoteze mapendeleo, hatupaswe kuacha kujikaza ili kufanya mapenzi ya Yehova. Kumbuka kama Yehova iko tayari kusamehe. (Zb. 103:8, 9) Hata kama tumefanya makosa, Yehova anaweza kuendelea kututumikisha sawa vile alitumikisha tena Samsoni. w23.09 6 fu. 15-16

Siku ya Ine, 21 Mwezi wa 8

Uvumilivu unatokeza hali ya kukubaliwa; na hali ya kukubaliwa inatokeza tumaini.​—Ro. 5:4.

Uvumilivu wako unafanya Yehova akukubali. Ile haimaanishe kama Yehova anafurahi wakati unapata majaribu ao magumu. Lakini ni weye njo Yehova anafurahia. Uvumilivu wako unatokeza hali ya kukubaliwa. Ile ni baraka ya ajabu! (Zb. 5:12) Kumbuka kama Abrahamu alivumilia majaribu na ile ilifanya Yehova amukubali. Yehova alimuona kuwa rafiki yake na alimuona kuwa mwenye haki. (Mwa. 15:6; Ro. 4:13, 22) Na siye anaweza kutuona vile. Haiko juu ya kazi mingi yenye tunafanya mu utumishi wake, ao juu tuko na madaraka ya mingi njo Yehova anatukubali. Yehova anatukubali juu tunavumilia kwa uaminifu. Siye wote tunaweza kuvumilia ikuwe tuko na miaka ngapi, tuko mu hali gani, ao tuko na uwezo gani. Je, kwa sasa kuko jaribu fulani yenye uko unavumilia kwa uaminifu? Kama ni vile, usisahau kama Yehova anakukubali. Kujua vile kunaweza kuwa na matokeo ya muzuri sana. Kunaweza kutia nguvu tumaini yetu. w23.12 11 fu. 13-14

Siku ya Tano, 22 Mwezi wa 8

Ujionyeshe kuwa mwanaume.​—1 Fa. 2:2.

Mwanaume Mukristo anapaswa kujifunza kuzungumuza muzuri. Mwanaume mwenye anajua kuzungumuza muzuri anasikiliza na anaelewa mawazo ya wengine na namna wengine wanajisikia. (Mez. 20:5) Anaweza kujifunza kutambua maoni ya mutu kupitia sauti ya ule mutu, sura yake, ao ishara zake za mwili. Hauwezi kujifunza kufanya mambo hayo kama haupitishe wakati pamoya na watu. Kama unazoea zaidi kuongea na watu kwa kuwatumia ujumbe ku telefone ao ku ordinatere, ile itakufanya usijue kuzungumuza muzuri na watu uso kwa uso. Kwa hiyo, ujikaze kutafuta nafasi za kuongea na watu uso kwa uso. (2 Yo. 12) Mwanaume Mukristo mwenye kukomaa kiroho anapaswa kuwa na uwezo wa kuhangaikia mahitaji yake na ya familia yake. (1 Ti. 5:8) Ni jambo ya maana ujifunze ufundi fulani wenye unaweza kukusaidia kupata kazi. (Mdo. 18:2, 3; 20:34; Efe. 4:28) Ujulikane kuwa mutu mwenye anatumikaka sana na mwenye anatumika mupaka amalize kazi yenye alianza. Ukifanya vile, inaweza kuwa mwepesi kwako kupata kazi na kuilinda. w23.12 27 fu. 12-13

Siku ya Posho, 23 Mwezi wa 8

Siku ya Yehova inakuja sawasawa kabisa na vile mwizi anakuja usiku.​—1 Te. 5:2.

Wakati Biblia inasema kuhusu “siku ya Yehova,” inazungumuzia wakati wenye Yehova ataharibu maadui wake na kuokoa watu wake. Zamani, wakati fulani Yehova alihukumu mataifa fulani. (Isa. 13:1, 6; Eze. 13:5; Sef. 1:8) “Siku ya Yehova” itaanza na uharibifu wa Babiloni Mukubwa na itaishia ku vita ya Armagedoni. Juu ya kuokoka ile “siku,” tunapaswa kujitayarisha kuanzia sasa. Kwa kweli, Yesu alifundisha kama tunapaswa “kuendelea kuwa tayari” kwa ajili ya “taabu kubwa.” Alisema ile maneno ili kuonyesha kama tunapaswa kufanya vile bila kuacha. (Mt. 24:21; Lu. 12:40) Mutume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandikia Watesalonike barua yake ya kwanza. Mu ile barua, alizungumuzia mifano mingi ili kusaidia Wakristo waendelee kuwa tayari kwa ajili ya siku ya Yehova ya hukumu. Mutume Paulo alijua kama siku ya Yehova haingekuya ile wakati. (2 Te. 2:1-3) Lakini, aliambia ndugu zake wajitayarishe kwa ajili ya ile siku sawa vile tu ingekuya kesho. Na siye pia tunapaswa kutumikisha ile shauri. w23.06 8 fu. 1-2

Siku ya Yenga, 24 Mwezi wa 8

Ndugu zangu wapendwa, mukuwe imara, bila kutikisika.​—1 Ko. 15:58.

Mu Tokyo, Japani, mulijengwa jengo moya ya murefu sana mu 1970. Juu mu ule muji mulikuwa natokea matetemeko mingi ya inchi, watu walikuwa najiuliza ikiwa ile jengo itabakia kabisa imara ao hapana. Juu ibakie imara, siri ilikuwa nini? Wajenzi walitumia vifaa vyenye viliifanya ikuwe nguvu sana, na waliijenga mu njia yenye ingeifanya ibakie imara hata kama kunatokea matetemeko ya inchi. Wakristo wako sawa vile ile jengo. Mu njia gani? Mukristo anapaswa kujua ni wakati gani anapaswa kuwa imara na ni wakati gani anapaswa kuwa na usawaziko. Anapaswa kuwa nguvu na imara wakati inaomba kutii sheria na kanuni za Yehova. Anakuwaka “tayari kutii.” Lakini anapaswa kuwa na usawaziko kama inawezekana ao kama ni lazima. (Yak. 3:17) Mukristo mwenye kuwa vile, ataepuka kuwa imara kupita kiasi ao kuachilia mambo kupita kiasi. w23.07 14 fu. 1-2

Siku ya Kwanza, 25 Mwezi wa 8

Hata kama hamujamuona hata siku moja, munamupenda.​—1 Pe. 1:8.

Yesu alipaswa kubakia muaminifu wakati Shetani Ibilisi alimujaribu, na hata wakati alimushawishi moja kwa moja avunje ushikamanifu wake kwa Mungu. (Mt. 4:1-11) Shetani aliazimia kabisa kumuchochea Yesu afanye zambi juu asiweze kulipa bei ya ukombozi. Wakati wa utumishi wake ku dunia, Yesu alivumilia majaribu ingine. Maadui wake walimutesa na hata walitafuta kumuua. (Lu. 4:28, 29; 13:31) Alipaswa kupambana na uzaifu wa wafuasi wake. (Mk. 9:33, 34) Wakati alikuwa nasambishwa alitendewa mubaya na kuchekelewa. Kisha aliuawa mu njia yenye kuzaraulisha na yenye maumivu mingi sana. (Ebr. 12:1-3) Alipaswa kuvumilia yeye mwenyewe majaribu ya mwisho-mwisho ya mu maisha yake bila ulinzi wa Yehova. (Mt. 27:46) Kwa kweli, Yesu alijizabihu sana juu ya kutoa bei ya ukombozi. Wakati tunafikiri sana juu ya namna Yesu alikuwa tayari kujitoa sana kwa ajili yetu, ile haifanye tumupende hata zaidi? w24.01 10-11 fu. 7-9

Siku ya Pili, 26 Mwezi wa 8

Wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.​—Mez. 21:5.

Kama tuko na uvumilivu, tunaweza kuwa na uhusiano wa muzuri pamoya na wengine, tutasikiliza wengine kwa uangalifu wakati wako nasema. (Yak. 1:19) Na kama tuko na uvumilivu, tutaendeleza amani. Ile sifa itatuzuia tusitende haraka sana ao kusema jambo fulani yenye haifae wakati tuko na mahangaiko. Tena, kama tuko na uvumilivu, hatutakasirika haraka wakati mutu fulani anatukwaza. Kuliko kulipiza kisasi, “tutaendelea kuvumiliana na kusameheana kwa kupenda.” (Kol. 3:12, 13) Tena, kama tuko na uvumilivu, tutakamata maamuzi ya muzuri zaidi. Kuliko kukamata maamuzi haraka-haraka, tutafanya utafiti juu ya kuchunguza ni uamuzi gani njo wa muzuri sana. Kwa mufano, kama tuko natafuta kazi, pengine tunaweza kuitika kazi yoyote yenye tunapata Lakini, kama tuko na uvumilivu, tutakamata wakati wa kuchunguza matokeo yenye ile kazi inaweza kuwa nayo juu ya familia yetu na juu ya hali yetu ya kiroho. Tena, ile sifa itatusaidia tuepuke kukamata uamuzi wa mubaya. w23.08 22 fu. 8-9

Siku ya Tatu, 27 Mwezi wa 8

Ninaona ndani ya mwili wangu sheria ingine ikipigana na sheria ya akili yangu na kunipeleka nikiwa nimetekwa kwa sheria ya zambi yenye kuwa ndani ya mwili wangu.​—Ro. 7:23.

Ikiwa umevunjika moyo kwa sababu ya muelekeo wako wa kufanya zambi, kufikiria ahadi yenye ulimutolea Yehova kunaweza kukusaidia upambane na majaribu. Kusema kweli, kufikiria naziri yako ya kujitoa kwa Yehova kutafanya mambo ikuwe mwepesi zaidi wakati unapambana na majaribu. Namna gani? Wakati unajitoa kwa Yehova, unajikana mwenyewe. Ile inamaanisha kama unatia pembeni tamaa na miradi yenye haimufurahishe Yehova. (Mt. 16:24) Kwa hiyo wakati unapambana na majaribu, hautapitisha wakati mingi na uko najiuliza utafanya nini. Kati ya njia zote utakuwa ulishachagua njia moya tu ya kufuata: kubakia muaminifu kwa Yehova. Utaazimia kabisa kuendelea kumufurahisha Yehova. Mu njia fulani utakuwa sawa vile Yobu. Hata kama alipambana na magumu ya nguvu sana, alisema hivi kwa uhakika: “Sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!”​—Yob. 27:5. w24.03 9 fu. 6-7

Siku ya Ine, 28 Mwezi wa 8

Yehova iko karibu na wale wote wenye kumuitia, wote wenye kumuitia katika ukweli.​—Zb. 145:18.

Yehova, “Mungu wa upendo,” iko pamoja na siye! (2 Ko. 13:11) Anahangaikia kila mumoja wetu kipekee. Tuko hakika kama “tunazungukwa na upendo wake mushikamanifu.” (Zb. 32:10) Kadiri tunaendelea kutafakari juu ya namna Yehova ametuonyesha upendo, ni vile tutamuona kuwa mutu kweli kabisa, na tutamukaribia zaidi. Tujisikie huru kusali kwake na kumuambia namna tuko na lazima kabisa ya upendo wake. Tunaweza kumuambia mambo yote yenye inatuhangaisha, juu tuko hakika kama anatuelewa na anapenda kabisa kutusaidia. (Zb. 145: 19) Sawa vile tu tunapendaka kukaribia moto wakati wa baridi, tunapenda kumukaribia Yehova kwa sababu ya upendo wake mwingi. Upendo wa Yehova ni wenye nguvu sana, lakini pia ni mwororo. Kwa hiyo, karibisha upendo wa Yehova mu maisha yako. Basi, siye wote upendo wake utuchochee kusema: “Ninamupenda Yehova”!​—Zb. 116:1. w24.01 31 fu. 19-20

Siku ya Tano, 29 Mwezi wa 8

Nimewajulisha jina lako.​—Yoh. 17:26.

Yesu hakuambia tu watu kama jina ya Mungu ni Yehova. Wayahudi wenye Yesu alifundisha, tayari walikuwa najua jina ya Mungu. Lakini Yesu alikuwa ule “mwenye . . . alieleza juu Yake.” (Yoh. 1:17, 18) Kwa mufano, Maandiko ya Kiebrania inaonyesha kama Yehova iko na rehema na huruma. (Kut. 34:5-7) Yesu alisaidia watu waelewe zaidi ile kweli wakati alieleza mufano wa mwana mupotevu na baba yake. Wakati tunasoma namna ule baba aliona mutoto wake “wakati alikuwa angali mbali,” namna alikimbia ili kukutana naye, namna alimukumbatia, na kumusamehe kwa moyo wote, tunaelewa muzuri zaidi rehema na huruma ya Yehova. (Lu. 15:11-32) Yesu alionyesha waziwazi Baba yake ni mutu wa namna gani. w24.02 10 fu. 8-9

Siku ya Posho, 30 Mwezi wa 8

Kufariji wengine . . . namna yoyote kupitia faraja yenye tunapokea kutoka kwa Mungu.​—2 Ko. 1:4.

Yehova anafanyaka wale wenye kuwa na huzuni wajisikie muzuri na wafarijike. Kama Yehova, namna gani na siye tunaweza kusikilia wengine huruma na kuwafariji? Njia moja ya kufanya vile ni kukomalisha katika moyo wetu sifa zenye zinaweza kutusaidia tufariji wengine. Ni sifa gani? Ni nini itatusaidia tuendelee kuwa na upendo wenye utatuchochea “tuendelee kufarijiana” kila siku? (1 Te. 4:18) Tunapaswa kukomalisha sifa sawa vile kujitia pa nafasi ya wengine, kuwa na upendo wa kindugu, na fazili. (Kol. 3:12; 1 Pe. 3:8) Zile sifa zitatusaidia namna gani? Wakati tunakuwa na huruma na hizi sifa zingine, tutakuwa na hamu sana ya kufariji wale wenye kuwa mu magumu. Sawa vile Yesu alisema “kinywa kinasema mambo yenye kujaa katika moyo. Mutu muzuri anatosha mambo ya muzuri katika hazina yake ya muzuri.” (Mt. 12:34, 35) Kufariji ndugu na dada wakati wako na lazima kabisa ya faraja ni njia ya muzuri sana ya kuonyesha kama tunawapenda. w23.11 10 fu. 10-11

Siku ya Yenga, 31 Mwezi wa 8

Wale wenye kuwa na ufahamu wataelewa.​—Da. 12:10.

Tunapaswa kuomba musaada kama tunapenda kuelewa maunabii yenye kuwa mu Biblia. Fikiria hii mufano. Wazia weye na rafiki yako muko naenda fasi fulani yenye haujue, lakini ule rafiki yako anajua ile fasi muzuri. Anajua muzuri kabisa kwenye muko na anajua muzuri fasi kwenye kila barabara inaishia. Bila shaka, utafurahi juu ule rafiki yako aliitika uende naye! Vilevile, Yehova anajua muzuri kipindi yenye tuko naishi na kwenye tuko naenda. Kwa hiyo, juu tuelewe maunabii yenye kuwa mu Biblia, tunapaswa kumuomba Yehova kwa unyenyekevu ili atusaidie. (Da. 2:28; 2 Pe. 1:19, 20) Sawa vile muzazi yeyote muzuri, Yehova anapenda watoto wake wakuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuya. (Yer. 29:11) Lakini, tofauti na muzazi yeyote, Yehova anaweza kutuambia bila kukosea mambo yenye itafanyika wakati wenye kuya. Aliandikisha maunabii mu Neno yake ili itusaidie kujua matukio makubwa mbele hata itokee.​—Isa. 46:10. w23.08 8 fu. 3-4

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine