Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Leo

Siku ya Tatu, 16 Mwezi wa 7

Yehova anajua kama kufikiri kwa watu wenye hekima ni kwa bure.​—1 Ko. 3:20.

Tunapaswa kuepuka kuwa na mawazo ya wanadamu wenye hawatii sheria za Yehova. Kama tunakuwa na mawazo sawa ya watu wenye hawamutii Yehova, siye pia tunaweza kumuacha Yehova na kuacha kutii sheria zake. (1 Ko. 3:19) Mara mingi “hekima ya ulimwengu huu” inachocheaka watu wasimutii Mungu. Wakristo fulani wa Pergamamu na Tiatira walichochewa na watu wenye waliishi nao wenye walikuwa waasherati na waabudu sanamu. Juu wale Wakristo waliachilia uasherati uendelee, Yesu aliwapatia mashauri mazito. (Ufu. 2:14, 20) Leo, watu wanaweza kufanya tukuwe na mawazo ya mubaya. Watu wa familia na marafiki wanaweza kutuambia kama tuko wenye kushikamana kupita kiasi na mambo yenye tunaamini na wanaweza kutuambia tuvunje sheria za Yehova. Kwa mufano, wanaweza kusema kama haiko jambo ya maana kuendelea kuwa na mwenedo safi na kama kanuni zenye kuwa mu Biblia kuhusu mwenendo ni mambo ya zamani. Wakati fulani tunaweza kuwaza kama maagizo yenye Yehova anatupatiaka haieleweke. Tunaweza hata kujaribiwa kuongeza mambo yenye “kupita mambo yenye yaliandikwa.”​—1 Ko. 4:6. w23.07 16 fu. 10-11

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Ine, 17 Mwezi wa 7

Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote Naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.​—Mez. 17:17.

Maria, mama ya Yesu, alikuwa na lazima ya kutiwa nguvu. Hakukuwa na bwana lakini alipaswa kupata mimba. Hakukuwa alishakomalisha mutoto yeyote, lakini sasa alipaswa kuhangaikia mutoto mwenye angefikia kuwa Masiya. Na juu alikuwaka hayafanya ngono, namna gani angefasiria Yosefu, muchumba wake, ile mambo yote? (Lu. 1:26-33) Maria alipata wapi nguvu? Alitafuta musaada kwa Yehova. Kwa mufano, alimuomba Gabrieli amupatie mafasirio zaidi kuhusu mugao wake. (Lu. 1:34) Kisha wakati kidogo alisafiri kuenda mu eneo ya “inchi ya milima” ya Yuda ili kutembelea Elizabeti, mutu wa jamaa yake. Elizabeti alimupongeza Maria na aliongozwa na Yehova ili kutoa unabii wenye kutia moyo kuhusu mwana wa Maria mwenye alikuwa hayazaliwa. (Lu. 1:39-45) Maria alisema kama Yehova alikuwa “ametenda kwa nguvu kwa mukono wake.” (Lu. 1:46-51) Yehova alimutia nguvu Maria kupitia Gabrieli na Elizabeti. w23.10 14-15 fu. 10-12

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Tano, 18 Mwezi wa 7

Alitufanya tukuwe ufalme, makuhani kwa Mungu na Baba yake.​—Ufu. 1:6.

Hesabu kidogo ya wanafunzi wa Kristo wametiwa mafuta na roho takatifu, na wanafurahia uhusiano wa pekee pamoya na Yehova. Wale wanafunzi 144000 watatumika kama makuhani mbinguni pamoya na Yesu. (Ufu. 14:1) Mahali Patakatifu yenye ilikuwa mu tabenakulo inafananisha hali yao ya kufanywa kuwa wana wa Mungu wakati wangali ku dunia. (Ro. 8:15-17) Mahali Patakatifu Zaidi ya mu tabenakulo inafananisha mbinguni, kwenye Yehova anakuwaka. “Pazia” yenye ilitenganisha Patakatifu na Patakatifu Zaidi ilifananisha mwili wa kibinadamu wa Yesu wenye ulimuzuia kuingia mbinguni akiwa Kuhani Mukubwa zaidi wa hekalu ya kiroho. Kwa kutoa mwili wake wa kibinadamu kuwa zabihu kwa ajili ya wanadamu, Yesu alifanya iwezekane kwa Wakristo wote watiwa-mafuta kuenda mbinguni. Wanapaswa pia kuacha miili yao ya kibinadamu ili wapate zawabu ya kuishi mbinguni.​—Ebr. 10:19, 20; 1 Ko. 15:50. w23.10 28 fu. 13

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine