-
Hesabu 28:3-8Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
3 “Na uwaambie, ‘Hili ndilo toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto lenye mutamutolea Yehova: wana-kondoo dume wawili wa mwaka mumoja wenye hawana kasoro kuwa toleo la kawaida la kuteketezwa.+ 4 Utatoa mwana-kondoo dume mumoja asubui, na mwana-kondoo dume mwingine utamutoa mangaribi wakati giza linaanza,*+ 5 pamoja na sehemu moja ya kumi (1/10) ya efa* ya unga muzuri wenye kuchanganywa na sehemu moja ya ine (1/4) ya hini* ya mafuta ya zeituni zenye kupondwa-pondwa kuwa toleo la nafaka.+ 6 Ni toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida,+ lenye lilianzishwa kwenye Mulima Sinai kuwa harufu ya muzuri,* toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, 7 pamoja na toleo lake la kinywaji, sehemu moja ya ine (1/4) ya hini kwa ajili ya kila mwana-kondoo dume.+ Umwange pombe katika mahali patakatifu kuwa toleo la kinywaji kwa ajili ya Yehova. 8 Na utatoa mwana-kondoo dume mwingine mangaribi wakati giza linaanza.* Pamoja na toleo la nafaka kama lile lenye lilitolewa asubui pamoja na toleo lilelile la kinywaji, utalitoa kuwa toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova.+
-