-
Kutoka 23:31-33Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
31 “Nitaweka mupaka wako kuanzia Bahari Nyekundu kufikia bahari ya Wafilisti na kuanzia jangwa kufikia ule Muto;*+ kwa maana nitatia wakaaji wa inchi hiyo katika mukono wako, na utawafukuza watoke mbele yako.+ 32 Haupaswe kufanya agano pamoja nao wala pamoja na miungu yao.+ 33 Hawapaswe kuishi katika inchi yako, ili wasikufanye unitendee zambi. Kama unatumikia miungu yao, hakika jambo hilo litakuwa mutego kwako.”+
-
-
Kumbukumbu la Torati 7:3, 4Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
3 Haupaswe kufanya mapatano yoyote ya ndoa pamoja* nao. Watoto wako wanamuke usiwapatie watoto wao wanaume wala usikamate watoto wao wanamuke kwa ajili ya watoto wako wanaume.+ 4 Kwa maana watageuza watoto wenu wanaume waache kunifuata ili kutumikia miungu mingine;+ kisha kasirani ya Yehova itawaka juu yenu, na atawaharibu haraka.+
-
-
Yoshua 23:12, 13Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
12 “Lakini kama munageuka na kushikamana na watu wa mataifa haya yenye yanabakia,+ wenye wangali pamoja na ninyi na kama munafanya maagano ya ndoa+ pamoja* nao na kujiunga nao na wao kujiunga na ninyi, 13 munapaswa kujua kwa uhakika kwamba Yehova Mungu wenu hataendelea kufukuza* mataifa haya kwa ajili yenu.+ Yatakuwa mutego kwenu na kitu cha kunasa na yatakuwa fimbo kwenye mbavu zenu+ na miiba katika macho yenu mupaka wakati mutaangamia musikuwe tena katika inchi hii ya muzuri yenye Yehova Mungu wenu amewapatia.
-