-
2 Wafalme 24:12, 13Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
12 Mufalme Yehoyakini wa Yuda akatoka inje kuenda kwa mufalme wa Babiloni,+ pamoja na mama yake, watumishi wake, wakubwa wake, na watu wenye cheo kwenye makao yake;+ na mufalme wa Babiloni akamukamata mateka katika mwaka wa munane (8) wa utawala wake.+ 13 Kisha akakamata kutoka pale hazina zote za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mufalme.+ Akakata vipande-vipande vyombo vyote vya zahabu vyenye Sulemani mufalme wa Israeli alikuwa ametengeneza katika hekalu la Yehova.+ Jambo hilo lilitokea kama vile Yehova alikuwa ametabiri.
-
-
Zaburi 74:7Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
7 Waliunguza patakatifu pako.+
Walichafua tabenakulo yenye kubeba jina lako, wakaiangusha chini.
-