-
Kumbukumbu la Torati 12:31Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
31 Haupaswe kumufanyia vile Yehova Mungu wako, kwa sababu mataifa hayo yanafanyia miungu yao kila jambo lenye kuchukiza lenye Yehova anachukia, hata yanateketeza watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke ndani ya moto kwa ajili ya miungu yao.+
-
-
2 Wafalme 16:1Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
16 Katika mwaka wa kumi na saba (17) wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi+ mwana wa Mufalme Yotamu wa Yuda akakuwa mufalme.
-
-
2 Wafalme 17:17, 18Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
17 Pia walipitisha watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke katika moto,+ walifanya uaguzi na walitafuta alama za mambo yenye yatatokea,+ na waliendelea kujitoa* wenyewe ili kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova, ili kumukasirisha.
18 Basi Yehova akakasirikia sana Israeli, na hivyo akawaondoa mbele ya macho yake.+ Hakuacha mutu yeyote abakie isipokuwa kabila la Yuda tu.
-
-
Yeremia 7:30, 31Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
30 ‘Kwa maana watu wa Yuda wamefanya mambo ya mubaya mbele ya macho yangu,’ ni vile Yehova anasema. ‘Wameweka sanamu zao zenye kuchukiza katika nyumba yenye inabeba jina langu, ili kuichafua.+ 31 Wamejenga mahali pa juu pa Tofeti, kwenye kuwa katika Bonde la Mwana wa Hinomu,*+ ili kuteketeza watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke katika moto,+ jambo lenye sikukuwa nimeamuru na halijaingia katika moyo wangu* hata kidogo.’+
-