Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Isaya 28:16
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 16 Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:

      “Angalia, ninaweka katika Sayuni jiwe lenye limejaribiwa ili likuwe musingi,+

      Jiwe la pembe lenye samani+ la musingi imara.+

      Kila mutu mwenye anaonyesha imani hataogopa.+

  • Luka 20:17
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 17 Lakini akawaangalia moja kwa moja na kusema: “Basi, andiko hili maana yake nini: ‘Jiwe lenye wajenzi walikataa ndilo limekuwa jiwe kubwa la pembe’?*+

  • Matendo 4:11
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 11 Hili ndilo ‘jiwe lenye ninyi wajenzi mulitendea kama vile halina maana lenye limekuwa jiwe kubwa la pembe.’*+

  • 1 Wakorinto 3:11
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 11 Kwa maana hakuna mutu mwenye anaweza kuweka musingi mwingine wowote juu ya ule wenye uliwekwa, ambao ni Yesu Kristo.+

  • Waefeso 2:19, 20
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 19 Basi ninyi hamuko tena wageni na watu wa mataifa ya kigeni,+ lakini ninyi muko wanainchi+ pamoja na watakatifu na muko washiriki wa nyumba ya Mungu,+ 20 na mumejengwa juu ya musingi wa mitume na manabii,+ na Kristo Yesu mwenyewe ndiye jiwe la musingi la pembe.+

  • 1 Petro 2:4-7
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 4 Wakati munakuja kwake, jiwe lenye uzima lenye lilikataliwa na wanadamu+ lakini lenye lilichaguliwa, lenye samani kwa Mungu,+ 5 ninyi wenyewe pia kama majiwe yenye uzima munajengwa kuwa nyumba ya kiroho+ kusudi mukuwe ukuhani mutakatifu, ili kutoa zabihu za kiroho+ zenye kukubalika kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.+ 6 Kwa maana Andiko linasema: “Angalia! Ninaweka katika Sayuni jiwe lenye lilichaguliwa, jiwe la musingi la pembe lenye samani, na mutu yeyote mwenye anaonyesha imani katika jiwe hilo hatakata tamaa* hata kidogo.”+

      7 Kwa hiyo, yeye ni mwenye samani kwenu, kwa sababu ninyi ni waamini; lakini kwa wale wenye hawaamini, “jiwe lenye wajenzi walikataa+ ndilo limekuwa jiwe kubwa la pembe,”*+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine