-
Matendo 4:25-28Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
25 na ulisema kupitia roho takatifu kwa kinywa cha babu yetu Daudi,+ mutumishi wako: ‘Sababu gani mataifa yalikuwa na musukosuko na watu walifikiri juu ya mambo yenye hayana maana? 26 Wafalme wa dunia walijipanga na watawala wakakusanyika pamoja kama mutu mumoja ili kumupinga Yehova* na ili kumupinga mutiwa-mafuta wake.’*+ 27 Kwa maana kwa kweli Herode na Pontio Pilato+ pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli walikusanyika pamoja katika muji huu ili kumupinga mutumishi wako mutakatifu Yesu, mwenye ulitia mafuta,+ 28 ili kufanya mambo yenye mukono wako na shauri lako vilionyesha mbele ya wakati kuwa yatatokea.+
-