Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 36:20, 21
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 20 Akakamata mateka wale wenye waliponyoka upanga na kuwapeleka Babiloni,+ na wakakuwa watumishi wake+ na wa wana wake mupaka wakati ufalme wa Uajemi ulianza* kutawala,+ 21 ili kutimiza neno la Yehova lenye lilisemwa na Yeremia,+ mupaka wakati inchi ilikuwa imelipa sabato zake.+ Siku zote zenye iliachwa ukiwa ilishika sabato, ili kutimiza miaka makumi saba (70).+

  • Isaya 49:14
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 14 Lakini Sayuni aliendelea kusema:

      “Yehova ameniacha,+ na Yehova amenisahau.”+

  • Yeremia 30:17
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 17 “Lakini nitakurudishia afya ya muzuri na nitaponyesha vidonda vyako,”+ ni vile Yehova anasema.

      “Hata kama walikuita mwenye kutengwa:

      ‘Sayuni, mwenye hakuna mutu yeyote mwenye anamutafuta.’”+

  • Maombolezo 1:4
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    •  4 Barabara za kuenda Sayuni zinaomboleza, kwa sababu hakuna mutu yeyote mwenye anakuja kwenye sikukuu.+

      Milango yake yote mikubwa imekuwa ukiwa;+ makuhani wake wanalia kwa maumivu.

      Mabikira wake* wako na huzuni, na yeye iko* katika uchungu mukali.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine