Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 28:53-57
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 53 Halafu utalazimika kula watoto wako* mwenyewe, nyama ya watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke+ wenye Yehova Mungu wako amekupatia, kwa sababu ya kuzungukwa sana kwa ajili ya vita na kwa sababu ya taabu yenye adui yako atakuletea.

      54 “Hata mwanaume mupole* sana na mwenye hisia nyingi kati yako hatamusikilia huruma ndugu yake ao bibi yake mupendwa ao wana wake wenye wanabakia, 55 na hatawapatia hata kidogo sehemu yoyote ya nyama ya wana wake yenye atakula, kwa maana hana kitu kingine chochote cha kula kwa sababu ya kuzungukwa sana kwa ajili ya vita na kwa sababu ya taabu yenye adui yako ataleta katika miji yako.+ 56 Na mwanamuke mupole* sana na mwenye hisia nyingi kati yako mwenye hawezi hata kufikiria kutia kikanyangio cha muguu wake chini kwa sababu ni mupole sana+ hatakuwa na huruma kuelekea bwana yake mupendwa wala mutoto wake mwanaume wala mutoto wake mwanamuke, 57 hata kuelekea vitu vyenye kutoka katikati ya miguu yake kisha kuzaa na kuelekea wana wenye anazaa, kwa maana atawakula kwa uficho kwa sababu ya kuzungukwa sana kwa ajili ya vita na kwa sababu ya taabu yenye adui yako ataleta katika miji yako.

  • 2 Wafalme 25:3-7
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 3 Katika siku ya kenda (9) ya mwezi wa ine (4) njaa ikakuwa kali+ katika muji, na hapakukuwa chakula kwa ajili ya watu wa inchi.+ 4 Ukuta wa muji ulitobolewa tundu kubwa,+ na maaskari wote wakakimbia usiku kupitia mulango mukubwa wenye kuwa kati ya zile kuta mbili karibu na bustani ya mufalme, wakati Wakaldayo walikuwa wanazunguka muji; na mufalme akaenda kupitia njia ya Araba.+ 5 Lakini jeshi la Wakaldayo likamufuatilia mufalme, na wakamufikia katika maeneo tambarare ya jangwa la Yeriko, na maaskari wake wote wakatawanyika na kutoka pembeni yake. 6 Kisha wakamukamata mufalme+ na kumuleta mupaka kwa mufalme wa Babiloni kule Ribla, na wakamuhukumu. 7 Wakaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake; kisha Nebukadneza akapofusha macho ya Sedekia, akamufunga kwa pingu za shaba, na akamupeleka Babiloni.+

  • Isaya 3:1
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 3 Kwa maana angalia! Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,

      Anaondoa katika Yerusalemu na katika Yuda kila namna ya tegemeo na akiba,

      Tegemeo lote la mukate na maji,+

  • Ezekieli 4:16
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 16 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, angalia, nitaondoa akiba ya chakula* katika Yerusalemu,+ na kwa wasiwasi mwingi watakula kipimo chao cha mukate kwa kupima,+ na kwa woga mukubwa watakunywa kipimo chao cha maji kwa kupima.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine