Isaya
10 Ole wao wale wenye wanatunga masharti yenye kuumiza+
Wenye kila wakati wanaandika amri za kukandamiza watu,
2 Ili kuima maskini haki zao za kisheria
Ili kunyanganya haki+ watu wa hali ya chini kati ya watu wangu,
Kuchukua vitu vya wajane,
4 Hakuna chenye kubakia isipokuwa kushutama kati ya wafungwa
Ao kuanguka kati ya watu wenye waliuawa.
Kwa sababu ya mambo hayo yote, kasirani yake haijarudia nyuma,
Lakini mukono wake ungali wenye kunyooshwa ili kupiga.+
Fimbo ya kuonyesha kasirani yangu,+
Na fimbo yenye kuwa katika mukono wao kwa ajili ya kuonyesha kemeo langu!
6 Nitamutuma ashambulie taifa lenye kuasi imani,+
Ashambulie watu wenye wamenikasirisha sana,
Nitamuamuru achukue vitu vingi na kunyanganya vitu vingi katika vita
Na kuvikanyanga-kanyanga kama matope katika barabara.+
7 Lakini hatataka kufanya vile
Na moyo wake hautapanga kufanya vile;
Kwa maana kuangamiza kuko katika moyo wake,
Kuondoa mataifa mengi yasikuwe tena, hapana mataifa kidogo.
9 Je, Kalno+ haiko kama vile Karkemishi?+
Je, Hamati+ haiko kama Arpadi?+
Je, Samaria+ haiko kama Damasko?+
10 Mukono wangu umekamata falme za miungu yenye haina mafaa yoyote,
Zenye sanamu zao za kuchongwa zilikuwa nyingi kuliko zile za Yerusalemu na Samaria!+
11 Je, sitatendea pia Yerusalemu na sanamu zake
Kama vile nilitendea Samaria na miungu yake yenye haina mafaa yoyote?’+
12 “Wakati Yehova atamaliza kazi yake yote kwenye Mulima Sayuni na katika Yerusalemu, Yeye atapatia* mufalme wa Ashuru azabu kwa sababu ya moyo wake wenye zarau na namna yake ya kuangalia yenye kiburi na majivuno.+ 13 Kwa maana anasema,
‘Nitafanya vile kwa nguvu za mukono wangu
Na kwa hekima yangu, kwa maana niko na hekima.
Nitaondoa mipaka ya vikundi vya watu,+
Na kunyanganya hazina zao,+
Na nitatiisha wakaaji kama mutu mwenye nguvu.+
14 Kama mutu mwenye anafika katika chicha,*
Mukono wangu utakamata mali za vikundi vya watu;
Na kama mutu mwenye anakusanya mayai yenye yameachwa,
Nitakusanya dunia yote!
Hakuna mwenye atapiga mabawa yake ao kufungua kinywa chake wala kusema kwa sauti ya chini.’”
15 Je, shoka litajiinua juu ya ule mwenye analitumia ili kukata?
Je, musumeno utajiinua juu ya ule mwenye anautumia ili kukata?
Je, fimbo+ inaweza kutikisa ule mwenye kuiinua?
Ao je, fimbo inaweza kuinua ule mwenye hatengenezwe na muti?
16 Kwa hiyo Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,
Atafanya watu wanene wakonde sana na kuwa wazaifu,+
Na chini ya utukufu wake atawasha moto wenye kuteketeza.+
17 Mwangaza wa Israeli+ utakuwa moto,+
Na Mutakatifu wake mwali wa moto;
Utawaka na kuteketeza magugu yake na miti yake midogo-midogo ya miiba kwa siku moja.
18 Ataondoa kabisa* utukufu wa pori lake na shamba lake la matunda,
Itakuwa kama wakati mutu mugonjwa anakuwa muzaifu.+
19 Miti yenye itabakia katika pori lake
Itakuwa kidogo sana kiasi ya kwamba kijana mudogo ataweza kuiandika kwenye oroza.
20 Siku hiyo wale wenye watabakia wa Israeli
Na wenye waliokoka wa nyumba ya Yakobo
Hawatamutegemea tena ule mwenye aliwapiga;+
Lakini watamutegemea Yehova,
Mutakatifu wa Israeli, kwa uaminifu.
22 Kwa maana hata kama watu wako, Ee Israeli,
Ni kama chembe za muchanga wa bahari,
Ni mabaki tu ndio watarudia.+
23 Ndiyo, uharibifu wenye uliamuliwa na Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi,
Utafanywa katika inchi yote.+
24 Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi, anasema: “Musiogope, watu wangu wenye kukaa katika Sayuni, kwa sababu ya Mwashuru, mwenye alikuwa anawapiga kwa fimbo+ na kuinua fimbo yake juu yenu kama vile Misri ilifanya.+ 25 Kwa maana katika wakati kidogo sana kemeo litafika mwisho; na kasirani yangu itaelekezwa kwenye uharibifu wao.+ 26 Yehova wa majeshi atatikisa mujeledi juu yake,+ kama vile wakati alishinda Midiani pembeni ya mwamba wa Orebu.+ Na fimbo yake itakuwa juu ya bahari, naye ataiinua kama vile alitendea Misri.+
27 “Siku hiyo muzigo wake utaondoka kwenye bega lako,+
Na nira yake itaondoka kwenye shingo yako,+
Na nira itavunjwa+ kwa sababu ya mafuta.”
29 Wamevuka nafasi ya kuvukia;
Wamekaa Geba usiku wote;+
30 Pandisha sauti na ulalamike, Ee binti ya Galimu!
Kaza uangalifu, Ee Laisha!
Ee maskini Anatoti!+
31 Madmena amekimbia.
Wakaaji wa Gebimu wametafuta mahali pa kujificha.
Anatikisa ngumi yake kwenye mulima wa binti ya Sayuni,
Kilima cha Yerusalemu.
33 Angalia! Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,
Anakata matawi kwa kishindo cha kuogopesha;+
Miti mirefu zaidi inakatwa,
Na wenye kuwa juu wanashushwa.