Yobu
35 Elihu akaendelea kujibu:
2 “Je, uko kabisa hakika kwamba uko na haki ya kusema,
‘Niko mwenye haki kuliko Mungu’?+
3 Kwa maana unasema, ‘Haki yangu iko na faida gani kwako?*
Je, hali yangu iko muzuri kuliko vile ingekuwa kama ningefanya zambi?+
4 Nitakujibu
Wewe pamoja na marafiki wako.+
5 Angalia juu mbinguni na uone,
Ona mawingu,+ yenye kuwa mbali juu yako.
6 Kama unatenda zambi, hilo linamuumiza namna gani?+
Kama makosa yako yanaongezeka, hilo linamufanya nini?+
8 Uovu wako uko na matokeo juu ya mwanadamu tu kama wewe,
Na haki yako juu ya mwana wa binadamu.
9 Watu wanalia wakati wanakandamizwa sana;
Wanalia ili wapate kitulizo kwa sababu ya utawala* wa watu wenye nguvu.+
10 Lakini hakuna mwenye kusema, ‘Iko* wapi Mungu, Mutengenezaji wangu Mukubwa,+
Yeye mwenye kufanya nyimbo ziimbwe usiku?’+
14 Namna gani basi, wakati unalalamika kwamba haumuone!+
Kesi yako ya hukumu iko mbele yake, kwa hiyo unapaswa kumungojea kwa hamu.+
15 Kwa maana hajakuomba kwa kasirani utoe hesabu;
Wala hajakazia uangalifu maneno yako makali sana.+
16 Yobu anafungua wazi kinywa chake bure;
Anasema maneno mengi bila ujuzi.”+