Ezekieli
42 Kisha akanipeleka kwenye kiwanja cha inje kuelekea kaskazini.+ Na akanileta kwenye jengo la vyumba vya kukulia chakula lenye lilikuwa karibu na eneo lenye kuwa wazi,+ upande wa kaskazini wa jengo lenye kufuata.+ 2 Urefu wake katika muingilio wa kaskazini ulikuwa mikono* mia moja (100), na upana wake mikono makumi tano (50). 3 Jengo hilo lilikuwa kati ya kiwanja cha ndani, chenye kilikuwa na upana wa mikono makumi mbili (20),+ na sakafu* ya kiwanja cha inje. Veranda zake ziliangaliana na zilikuwa na urefu wa gorofa tatu (3). 4 Mbele ya vyumba vya kukulia chakula* kulikuwa njia ya ndani+ yenye upana wa mikono kumi (10) na urefu wa mikono mia moja (100),* na miingilio yake ilielekea kaskazini. 5 Vyumba vya kukulia chakula vyenye vilikuwa juu katika jengo vilikuwa vyembamba kuliko vile vya chini na gorofa za katikati, kwa sababu veranda zilikamata nafasi kubwa ya vyumba hivyo. 6 Kwa maana zilikuwa na urefu wa gorofa tatu (3), lakini hazikukuwa na nguzo kama nguzo za vile viwanja. Ndiyo sababu nafasi kubwa zaidi ya sakafu* ilikamatwa kwenye vyumba hivyo vya kukulia chakula kuliko kwenye gorofa za chini na za katikati.
7 Ukuta wa inje wa majiwe wenye ulikuwa karibu na vyumba vya kukulia chakula kuelekea kiwanja cha inje chenye kilielekea vile vyumba vingine vya kukulia chakula ulikuwa na urefu wa mikono makumi tano (50). 8 Kwa maana urefu wa vyumba vya kukulia chakula vyenye vilielekea kiwanja cha inje ulikuwa mikono makumi tano (50), lakini vile vyenye vilielekea patakatifu, urefu wake ulikuwa mikono mia moja (100). 9 Vyumba vya kukulia chakula vilikuwa na muingilio upande wa mashariki wenye ulipeleka kwenye vyumba hivyo kutoka kwenye kiwanja cha inje.
10 Kulikuwa pia vyumba vya kukulia chakula ndani ya* ukuta wa majiwe wa kiwanja kuelekea mashariki, karibu na eneo lenye kuwa wazi na jengo.+ 11 Mbele yake kulikuwa njia kama ile ya vyumba vya kukulia chakula vya kaskazini.+ Vilikuwa na urefu na upana uleule, na vilikuwa na milango ya kutokea yenye kufanana na ramani zenye kufanana. Miingilio yake 12 ilikuwa kama ile miingilio ya vyumba vya kukulia chakula vyenye vilielekea kusini. Kulikuwa muingilio mahali kwenye njia ilianzia mbele ya ukuta wa majiwe wenye ulikuwa karibu nayo kuelekea mashariki, kwenye mutu angeingilia.+
13 Kisha akaniambia: “Vyumba vya kukulia chakula vya kaskazini na vyumba vya kukulia chakula vya kusini vyenye kuwa karibu na eneo lenye kuwa wazi+ ndivyo vyumba vya kukulia chakula vyenye kuwa vitakatifu kwenye makuhani wenye wanamukaribia Yehova wanakula matoleo matakatifu zaidi.+ Ni pale wanatia matoleo matakatifu zaidi, toleo la nafaka, toleo la zambi, na toleo la hatia, kwa sababu mahali pale ni patakatifu.+ 14 Wakati makuhani wanaingia, hawapaswe kutoka mahali patakatifu na kuenda kwenye kiwanja cha inje bila kuvua kwanza nguo zenye wanavaa wakati wanafanya utumishi,+ kwa sababu hizo ni nguo takatifu. Watavaa nguo zingine ili kukaribia maeneo kwenye watu wanaruhusiwa kuingia.”
15 Wakati alimaliza kupima eneo la ndani la hekalu,* akanipeleka inje kupitia mulango mukubwa wenye unaelekea mashariki,+ na akapima eneo hilo lote.
16 Akapima upande wa mashariki kwa ule utete wa kupimia.* Ulikuwa na urefu wa matete mia tano (500) kutoka upande mumoja mupaka upande mwingine, kulingana na utete wa kupimia.
17 Akapima upande wa kaskazini, na ulikuwa na urefu wa matete mia tano (500), kulingana na utete wa kupimia.
18 Akapima upande wa kusini, na ulikuwa na urefu wa matete mia tano (500), kulingana na utete wa kupimia.
19 Akazunguka upande wa mangaribi. Akapima matete mia tano (500) kwa utete wa kupimia.
20 Akapima eneo hilo kwenye pande ine (4). Lilikuwa na ukuta kuzunguka pande zote+ wenye ulikuwa na urefu wa matete mia tano (500) na upana wa matete mia tano,+ ili kutenganisha kitu kitakatifu na kitu cha matumizi ya kawaida.+