Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 31
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Kuanguka kwa Misri, mwerezi murefu sana (1-18)

Ezekieli 31:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 46:2; Eze 29:2

Ezekieli 31:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kichaka chenye.”

Ezekieli 31:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Kiota ni nyumba ya ndege.

Ezekieli 31:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 2:8; Eze 28:12, 13

Ezekieli 31:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wewe ulikuwa.”

Ezekieli 31:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 30:10, 11; Hab 1:6

Ezekieli 31:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 32:5, 6

Ezekieli 31:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 29:5; 32:4

Ezekieli 31:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kaburi.”

Ezekieli 31:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ezekieli 31:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

  • *

    Ao “kaburi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 31:9

Ezekieli 31:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

  • *

    Tnn., “mukono wake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 32:18, 20
  • +Eze 30:6; 32:31

Ezekieli 31:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 31:9; 32:19

Maandiko ingine

Eze. 31:2Yer 46:2; Eze 29:2
Eze. 31:8Mwa 2:8; Eze 28:12, 13
Eze. 31:11Eze 30:10, 11; Hab 1:6
Eze. 31:12Eze 32:5, 6
Eze. 31:13Eze 29:5; 32:4
Eze. 31:16Eze 31:9
Eze. 31:17Eze 32:18, 20
Eze. 31:17Eze 30:6; 32:31
Eze. 31:18Eze 31:9; 32:19
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 31:1-18

Ezekieli

31 Katika mwaka wa kumi na moja (11), mwezi wa tatu (3), siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, ambia Farao mufalme wa Misri na vikundi vyake vya watu,+

“‘Unafanana na nani katika ukubwa wako?

 3 Kulikuwa Mwashuru, mwerezi katika Lebanoni,

Ulikuwa na matawi ya muzuri kama vile miti midogo-midogo yenye* kivuli, yenye urefu mukubwa,

Sehemu yake ya juu ilikuwa kati ya mawingu.

 4 Maji yaliufanya ukuwe mukubwa, chemchemi za maji zenye kuenda chini sana ziliufanya kuwa murefu.

Mito midogo ilizunguka pande zote mahali kwenye ulipandwa;

Mifereji yake ilitia maji miti yote ya shamba.

 5 Ndiyo sababu ulikuwa murefu kuliko miti ingine yote ya shamba.

“‘Na matawi yake ya mukubwa yaliongezeka, na matawi yake ya kidogo yakakuwa ya murefu

Kwa sababu ya maji mengi katika mito yake midogo.

 6 Ndege wote wa anga walitengeneza viota* kwenye matawi yake ya mukubwa,

Wanyama wote wa pori walizaa chini ya matawi yake ya kidogo,

Na mataifa yote yenye watu wengi yalikuwa yanakaa chini ya kivuli chake.

 7 Ukakuwa mukubwa kwa uzuri na kwa urefu wa matawi yake,

Kwa maana mizizi yake ilishuka katika maji mengi.

 8 Hakuna muti mwingine wa mwerezi katika bustani ya Mungu+ wenye ungeweza kulinganishwa nao.

Hakuna muti wa muberoshi wenye ulikuwa na matawi ya mukubwa kama yake,

Na hakuna muti wa mwaramoni wenye ulikuwa na matawi ya kidogo yenye kufanana na yake.

Hakuna muti mwingine katika bustani ya Mungu wenye ungeweza kukaribia uzuri wake.

 9 Niliufanya upendeze, kwa majani mengi,

Na miti ingine yote ya Edeni, katika bustani ya Mungu wa kweli, iliusikilia wivu.’

10 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ulikuwa* murefu sana, ukainua sehemu yake ya juu kati ya mawingu, na moyo wake ukakuwa na majivuno kwa sababu ya urefu wake, 11 nitautia katika mukono wa mutawala mwenye nguvu wa mataifa.+ Hakika ataukamatia hatua, na mimi nitaukataa kwa sababu ya uovu wake. 12 Nao wageni, wenye hawana huruma kabisa kati ya mataifa, wataukata, nao watauacha kwenye milima, na majani yake yataanguka katika mabonde yote, na matawi yake yatavunjika na kusambaa katika mito midogo ya inchi.+ Vikundi vyote vya watu wa dunia vitaondoka kwenye kivuli chake na kuuacha. 13 Ndege wote wa anga wataishi kwenye shina lake lenye lilianguka, na wanyama wote wa pori kwenye matawi yake;+ 14 Ni vile ili muti wowote wenye kuwa karibu na maji usikuwe murefu sana ao usiinue sehemu yake ya juu kati ya mawingu na muti wowote wenye ulitiwa maji mengi usifikie urefu wao. Kwa maana yote itatolewa ili ikufe, kwenye inchi ya chini, pamoja na wana wa binadamu, wenye kushuka katika shimo.’*

15 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Siku yenye utashuka kuingia katika Kaburi,* nitatokeza maombolezo. Kwa hiyo, nitafunika maji yenye kuenda chini sana na kuzuia mito yake midogo ili maji mengi yazuiwe. Nitatia giza katika Lebanoni kwa sababu yake, na miti yote ya shamba itakauka. 16 Wakati sauti ya kuanguka kwake itasikika, nitafanya mataifa yatetemeke wakati nitaushusha katika Kaburi* pamoja na wote wenye kushuka katika shimo,* na miti yote ya Edeni,+ yenye kuwa bora na ya muzuri sana ya Lebanoni, yote yenye ilitiwa maji mengi, itafarijiwa katika inchi ya chini. 17 Wameshuka katika Kaburi* pamoja naye, kwa wale wenye waliuawa kwa upanga,+ pamoja na wale wenye walimuunga mukono* wenye waliishi katika kivuli chake kati ya mataifa.’+

18 “‘Ni muti gani katika Edeni ulifanana na wewe kwa utukufu na ukubwa?+ Lakini hakika utashushwa pamoja na miti ya Edeni mupaka katika inchi ya chini. Utalala kati ya wale wenye hawatahiriwe, pamoja na wale wenye waliuawa kwa upanga. Itakuwa vile kwa Farao na vikundi vyake vyote vya watu,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine