Wimbo wa Sulemani
6 “Mupenzi wako ameenda wapi,
Ee mwenye sura na umbo ya muzuri sana kuliko wanamuke wote?
Mupenzi wako amefuata njia gani?
Acha tumutafute pamoja.”
2 “Mupenzi wangu ameenda kwenye bustani yake,
Kwenye bustani yenye mimea yenye kutoa harufu ya muzuri,
Ili kuchunga kondoo kati ya mabustani
Na kuchuma maua ya mayungiyungi.+
3 Mimi ni wa mupenzi wangu,
Na mupenzi wangu ni wangu.+
Anachunga wanyama kati ya maua ya mayungiyungi.”+
4 “Uko mwenye sura na umbo ya muzuri kama Tirza,*+ mupendwa wangu,+
Unapendeza kama Yerusalemu,+
Unashangaza kama majeshi yenye kukusanyika kuzunguka bendera zao.+
Nywele zako ziko kama kundi la mbuzi
Wenye kushuka kwenye milima ya Gileadi.+
6 Meno yako ni kama kundi la kondoo
Wenye wametoka kunawishwa,
Wote wamezaa mapacha,
Na hakuna mwenye amepoteza kitoto chake.
7 Kama kipande cha tunda la komamanga
Ni vile mashavu yako yanaonekana nyuma ya kitambaa chako cha kufunika kichwa.
8 Kunaweza kuwa malkia makumi sita (60)
Na masuria* makumi munane (80)
Na vijana wanamuke wenye hawana hesabu,+
9 Lakini mumoja tu ndiye njiwa wangu,+ wangu mwenye hana kasoro.
Mutoto wa pekee wa mama yake.
Anapendwa sana na* ule mwenye alimuzaa.
Mabinti wanamuona, na wanamutangaza kuwa mwenye furaha;
Malkia na masuria,* na wanamusifu.
10 ‘Ni mwanamuke gani mwenye kungaa* kama mapambazuko,*
Mwenye sura na umbo ya muzuri kama mwezi wenye kuenea,
Mwenye kutakata kama mwangaza wa jua,
Mwenye kushangaza kama majeshi yenye kukusanyika kuzunguka bendera zao?’”+
11 “Nilishuka kwenye bustani ya miti ya lozi+
Ili nione machipukizi katika bonde,*
Ili nione kama muzabibu umechipuka*
Kama miti ya mikomamanga imetoa maua.
13 “Rudia, rudia, Ee Mushulami!
Rudia, rudia,
Ili tukuone!”
“Sababu gani munamuangalia Mushulami?”+
“Yeye ni kama dansi ya vikundi mbili!”*