Yobu
7 “Katika dunia, je, maisha ya mwanadamu mwenye anaweza kufa hayako kama kazi ya kulazimishwa,
Na siku zake kama siku za mufanyakazi wa kulipwa?+
2 Kama vile mutumwa, yeye anatamani sana kivuli,
Na kama vile mufanyakazi wa kulipwa, yeye anangojea malipo yake.+
4 Wakati ninalala, ninajiuliza, ‘Nitaamuka wakati gani?’+
Lakini wakati usiku unakuwa murefu, ninaendelea kujigeuza-geuza mupaka wakati wa gizagiza la asubui.
6 Siku zangu zinapita mbio kuliko chombo cha kusuka cha musukaji wa nguo,+
Na zinaisha bila tumaini.+
8 Jicho lenye linaniona sasa halitaniona tena;
Macho yenu yatanitafuta, lakini sitakuwa tena.+
11 Kwa hiyo, sitazuia kinywa changu.
12 Je, mimi ni bahari ao munyama mukubwa wa bahari,
Ili uweke mulinzi juu yangu?
13 Wakati ninasema, ‘Kiti changu kitanifariji;
Kitanda changu kitapunguza mateso yangu,’
14 Kisha unaniogopesha sana na ndoto
Na kunitia woga kupitia maono,
15 Ili nichague* kufa kwa sababu ya kukosa pumuzi,
16 Ninachukia maisha yangu;+ sitaki kuendelea kuishi.
Uniache, kwa maana siku zangu ziko kama pumuzi.+
18 Sababu gani unamuchunguza kila asubui
Na kumujaribu kila wakati?+
19 Je, hautaacha kuniangalia
Na kuniacha kwa muda wa kutosha ili nimeze mate yangu?+
20 Kama nimefanya zambi, namna gani ninaweza kukuumiza wewe, Muchunguzaji wa wanadamu?+
Sababu gani umenifanya kuwa shabaha yako?
Je, nimekuwa muzigo kwako?
21 Sababu gani hausamehe zambi yangu
Na kusamehe kosa langu?
Kwa maana hivi karibuni nitalala katika mavumbi,+
Na utanitafuta, lakini sitakuwa tena.”