Kumbukumbu la Torati
5 Kisha Musa akaita Israeli wote na kuwaambia: “Sikia, Ee Israeli, masharti na maamuzi ya hukumu yenye ninakutangazia leo, na unapaswa kujifunza na kushika kwa uangalifu masharti na maamuzi hayo ya hukumu. 2 Yehova Mungu wetu alifanya agano pamoja na sisi katika Horebu.+ 3 Yehova hakufanya agano hilo pamoja na mababu zetu, lakini pamoja na sisi, sisi wote wenye kuwa wazima hapa leo. 4 Yehova alisema na ninyi uso kwa uso katika mulima, kutoka katika moto.+ 5 Nilisimama katikati yenu na Yehova wakati huo+ ili niwaambie neno la Yehova, kwa maana muliogopa kwa sababu ya moto na hamukupanda katika mulima.+ Alisema:
6 “‘Mimi ni Yehova Mungu wako, mwenye alikutosha katika inchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.+ 7 Haupaswe hata kidogo kuwa na miungu mingine isipokuwa mimi.*+
8 “‘Haupaswe kujifanyia sanamu ya kuchongwa+ wala umbo ya* kitu chochote chenye kuwa juu mbinguni ao chenye kuwa hapa chini juu ya dunia ao chenye kuwa ndani ya maji chini ya dunia. 9 Haupaswe kuviinamia wala kushawishiwa kuvitumikia,+ kwa sababu mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu,+ mwenye analeta azabu juu ya wana kwa sababu ya kosa la baba, juu ya kizazi cha tatu (3) na juu ya kizazi cha ine (4) cha wale wenye kunichukia,+ 10 lakini mwenye kuonyesha upendo mushikamanifu* kwa kizazi cha elfu (1 000) cha wale wenye kunipenda na kushika amri zangu.
11 “‘Haupaswe kutumia jina la Yehova Mungu wako kwa njia yenye haifae,+ kwa maana Yehova hatakosa kumupatia azabu mutu yeyote mwenye anatumia jina lake kwa njia yenye haifae.+
12 “‘Shika siku ya Sabato ili uione kuwa takatifu, kama vile Yehova Mungu wako alikuamuru.+ 13 Utatumika na kufanya kazi zako zote kwa siku sita (6),+ 14 lakini siku ya saba (7) ni sabato kwa ajili ya Yehova Mungu wako.+ Haupaswe kufanya kazi yoyote,+ wewe, wala mutoto wako mwanaume wala mutoto wako mwanamuke wala mutumwa wako mwanaume wala mutumwa wako mwanamuke wala ngombe-dume wako wala punda wako wala munyama yeyote katikati ya wanyama wako wa kufugwa wala mukaaji mugeni mwenye kuwa katika miji yako,*+ ili mutumwa wako mwanaume na mutumwa wako mwanamuke wapumuzike kama wewe.+ 15 Kumbuka kwamba ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri na kwamba Yehova Mungu wako alikutosha kule kwa mukono wenye nguvu na mukono wenye kunyooshwa.+ Ndiyo sababu Yehova Mungu wako alikuamuru ushike siku ya Sabato.
16 “‘Heshimia baba yako na mama yako,+ kama vile Yehova Mungu wako amekuamuru, ili uishi wakati murefu na kufanikiwa* katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia.+
17 “‘Haupaswe kuua.+
18 “‘Wala haupaswe kufanya uzinifu.+
19 “‘Wala haupaswe kuiba.+
20 “‘Wala haupaswe kutoa ushahidi wa uongo juu ya mwenzako.+
21 “‘Wala haupaswe kutamani bibi ya mwenzako.+ Wala haupaswe kutamani kwa uchoyo nyumba ya mwenzako wala shamba lake wala mutumwa wake mwanaume wala mutumwa wake mwanamuke wala ngombe-dume wake wala punda wake wala kitu chochote cha mwenzako.’+
22 “Yehova aliambia kutaniko lenu lote amri* hizo kwenye mulima, kutoka katika moto, wingu, na giza nzito,+ kwa sauti kubwa, na hakuongeza jambo lolote; kisha akaziandika kwenye mabamba mbili ya majiwe na kunipatia.+
23 “Lakini wakati tu mulisikia sauti kutoka katika lile giza, wakati mulima ulikuwa unawaka moto,+ vichwa vyote vya makabila yenu na wazee wakanikaribia. 24 Kisha mukasema, ‘Angalia, Yehova Mungu wetu ametuonyesha utukufu wake na ukubwa wake, na tumesikia sauti yake kutoka katika moto.+ Leo tumeona kwamba Mungu anaweza kuongea na mwanadamu na mwanadamu huyo anaweza kuendelea kuishi.+ 25 Sasa, sababu gani tukufe? Kwa maana moto huu mukubwa unaweza kututeketeza. Kama tunaendelea kusikia sauti ya Yehova Mungu wetu, hakika tutakufa. 26 Kwa maana ni nani kati ya miili yote* mwenye amesikia sauti ya Mungu mwenye kuishi ikiongea kutoka katika moto kama vile tulisikia na bado anaendelea kuishi? 27 Wewe mwenyewe unapaswa kuenda karibu ili usikie mambo yote yenye Yehova Mungu wetu atasema, na ni wewe utatuambia mambo yote yenye Yehova Mungu wetu anakuambia, na sisi tutasikiliza na kuyatenda.’+
28 “Kwa hiyo Yehova alisikia maneno yenye muliniambia, na Yehova akaniambia, ‘Nimesikia maneno yenye watu hawa wamekuambia. Mambo yote yenye wamesema ni sawa.+ 29 Kama tu wangekuwa sikuzote na moyo wenye muelekeo wa kuniogopa+ na kushika amri zangu zote,+ basi mambo yangewaendea muzuri wao na wana wao milele!+ 30 Uende uwaambie: “Murudie kwenye mahema yenu.” 31 Lakini unapaswa kubakia hapa pamoja na mimi, na uache nikuambie amri zote, masharti, na maamuzi ya hukumu yenye unapaswa kuwafundisha na yenye wanapaswa kushika katika inchi yenye ninawapatia ili wairiti.’ 32 Sasa ninyi watu munapaswa kuwa waangalifu kufanya kama vile Yehova Mungu wenu amewaamuru.+ Musigeuke kuenda kuume wala kushoto.+ 33 Munapaswa kutembea katika njia yote yenye Yehova Mungu wenu amewaamuru,+ ili muishi na kufanikiwa na kurefusha siku zenu katika inchi yenye mutariti.+