Ezekieli
22 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Sasa wewe, mwana wa binadamu, je, uko tayari kutangaza hukumu juu ya* muji wenye hatia ya damu+ na kuujulisha mambo yake yote yenye kuchukiza?+ 3 Unapaswa kusema, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Ee muji wenye kumwanga damu+ ndani yake, wenye wakati wake unakuja,+ wenye kutengeneza sanamu zenye kuchukiza* ili kujichafua,+ 4 umekuwa na hatia kwa sababu ya kumwanga damu,+ na sanamu zako zenye kuchukiza zimekufanya usikuwe safi.+ Umeharakisha mwisho wa siku zako, na mwisho wa miaka yako umefika. Ndiyo sababu nitakufanya kuwa kitu cha haya kwa mataifa na kitu cha kuchekelewa katika inchi zote.+ 5 Inchi zenye kuwa karibu na wewe na zile zenye kuwa mbali na wewe zitakuchekelea,+ wewe mwenye jina lako haliko safi na mwenye kujaa musukosuko. 6 Angalia! Kila mumoja wa wakubwa wa Israeli kati yako anatumia mamlaka yake ili kumwanga damu.+ 7 Ndani yako wanamutendea baba yao na mama yao kwa zarau.+ Wanamupunja mukaaji mugeni, na wanamutendea mubaya mutoto mwenye hana baba* na mujane.”’”+
8 “‘Unazarau mahali pangu patakatifu, na unachafua sabato zangu.+ 9 Ndani yako muko wachongezi wenye wameazimia kumwanga damu.+ Ndani yako wanakula zabihu kwenye milima na kuendeleza mwenendo muchafu katikati yako.+ 10 Ndani yako wanakitendea bila heshima kitanda cha baba yao,*+ na wanamuchafua mwanamuke mwenye haiko safi katika siku zake za kuona mwezi.*+ 11 Ndani yako mwanaume mumoja anatenda kwa njia yenye kuchukiza pamoja na bibi ya jirani yake,+ mwingine anamuchafua binti-mukwe wake kupitia mwenendo muchafu,+ na mwingine anamuchafua dada yake, binti ya baba yake mwenyewe.+ 12 Ndani yako wanakamata rushwa* ili kumwanga damu.+ Unakopesha kwa faida+ ao kwa faida ya juu sana, na unapunja majirani wako feza.+ Ndiyo, umenisahau kabisa,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
13 “‘Angalia! Ninapiga mikono kwa sababu ya kuchukizwa na faida yenye haiko ya haki yenye umepata na kwa sababu ya matendo ya kumwanga damu yenye kuwa katikati yako. 14 Je, uhodari* wako utadumu na mikono yako itaendelea kuwa nguvu katika siku zenye nitakukamatia hatua?+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema, na nitakamata hatua. 15 Nitakusambaza kati ya mataifa na kukutawanya kati ya inchi hizo,+ na nitakomesha uchafu wako.+ 16 Na utazarauliwa mbele ya mataifa, na utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”+
17 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 18 “Mwana wa binadamu, nyumba ya Israeli imekuwa kama takataka yenye haina mafaa yoyote kwangu. Wote ni shaba na bati na chuma na risasi katika tanuru. Wamekuwa takataka ya feza.+
19 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ninyi wote mumekuwa kama takataka yenye haina mafaa yoyote, ninawakusanya pamoja ndani ya Yerusalemu.+ 20 Kama vile feza na shaba na chuma na risasi na bati zinakusanywa katika tanuru ili kuzipulizia moto na kuziyeyusha, ni vile nitawakusanya ninyi pamoja katika hasira yangu na katika kasirani yangu kali, na nitawapuliza na kuwayeyusha.+ 21 Nitawakusanya pamoja na kuwapulizia moto wa kasirani yangu kali,+ na ninyi mutayeyushwa ndani yake.+ 22 Kama vile feza inayeyushwa katika tanuru, ni vile mutayeyushwa ndani yake; na mutalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimemwanga kasirani yangu kali juu yenu.’”
23 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 24 “Mwana wa binadamu, ambia muji huo, ‘Wewe ni inchi yenye haitasafishwa wala kunyeshewa mvua katika siku ya kasirani kali. 25 Manabii wake wamefanya mupango mubaya ndani yake,+ kama vile simba mwenye kunguruma anapasua mawindo.+ Wanameza watu.* Wananyanganya hazina na vitu vyenye samani. Wamefanya wengi kuwa wajane ndani yake. 26 Makuhani wake wamevunja sheria yangu,+ nao wanaendelea kuchafua mahali pangu patakatifu.+ Hawafanye tofauti kati ya kitu kitakatifu na kitu cha kawaida,+ nao wamekosa kujulisha kitu chenye hakiko safi na kitu chenye kiko safi,+ nao wanakataa kushika sabato zangu, na mimi nimechafuliwa kati yao. 27 Wakubwa wake wenye kuwa katikati yake ni kama imbwa wa pori wenye kupasua mawindo; wanamwanga damu na kuua watu* ili kupata faida yenye haiko ya haki.+ 28 Lakini manabii wake wamepiga lipu matendo yao kwa chokaa. Wanaona maono ya uongo na kutoa uaguzi wa uongo,+ nao wanasema: “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi,” wakati Yehova mwenyewe hajasema. 29 Watu wa inchi wamepunja na kunyanganya,+ wamewatendea mubaya wenye uhitaji na maskini, nao wamemupunja mukaaji mugeni na kumuima haki.’
30 “‘Nilikuwa ninatafuta kati yao mutu mwenye angetengeneza nafasi zenye kuharibika za ukuta wa majiwe ao asimame mbele yangu katika tundu lenye kuwa katika ukuta kwa ajili ya inchi, ili isiharibiwe,+ lakini sikumupata mutu yeyote. 31 Kwa hiyo nitamwanga gazabu yangu juu yao na kuwamaliza kupitia moto wa kasirani yangu kali. Nitaleta matokeo ya njia yao juu ya kichwa chao wenyewe,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”