Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
1 Sulemani mwana wa Daudi akaendelea kuwa na nguvu katika ufalme wake, na Yehova Mungu wake alikuwa pamoja naye na akamufanya kuwa mukubwa sana.+
2 Sulemani akaagiza Israeli wote wakusanywe, wakubwa wa maelfu na wa mamia, waamuzi, na wakubwa wote wa Israeli yote, vichwa vya jamaa za upande wa baba. 3 Kisha Sulemani na kutaniko lote wakaenda mahali pa juu kule Gibeoni,+ kwa maana kule ndiko kulikuwa hema ya mukutano ya Mungu wa kweli, hema yenye Musa mutumishi wa Yehova alikuwa ametengeneza katika jangwa. 4 Hata hivyo, Daudi alikuwa amepandisha Sanduku la Mungu wa kweli kutoka Kiriat-yearimu+ na kulileta mahali kwenye Daudi alikuwa ametayarisha kwa ajili yake; alikuwa amejenga hema kwa ajili ya Sanduku hilo katika Yerusalemu.+ 5 Na ile mazabahu ya shaba+ yenye Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru alikuwa ametengeneza ilikuwa imewekwa mbele ya tabenakulo ya Yehova; na Sulemani na kutaniko walikuwa wanasali mbele ya mazabahu hiyo.* 6 Sasa Sulemani akatoa matoleo pale mbele ya Yehova, na akatoa matoleo elfu moja (1 000) ya kuteketezwa kwenye mazabahu ya shaba+ ya hema ya mukutano.
7 Usiku huo Mungu akamutokea Sulemani na kumuambia: “Omba kile unataka nikupatie.”+ 8 Halafu Sulemani akamuambia Mungu: “Umemuonyesha baba yangu Daudi upendo mwingi mushikamanifu,+ na umenifanya kuwa mufalme pa nafasi yake.+ 9 Sasa, Ee Yehova Mungu, ahadi yako yenye ulimutolea Daudi baba yangu ikuwe ya uaminifu,+ kwa maana umenifanya kuwa mufalme juu ya watu wengi sana kama chembe za mavumbi ya dunia.+ 10 Sasa unipatie hekima na ujuzi+ ili niongoze watu hawa,* kwa maana ni nani mwenye anaweza kuhukumu watu wako hawa wenye ni wengi?”+
11 Kisha Mungu akaambia Sulemani: “Kwa sababu hii ndiyo tamaa ya moyo wako na haukuomba mali, utajiri, na heshima ao kifo cha* wale wenye wanakuchukia, ao haukuomba maisha ya murefu,* lakini umeomba hekima na ujuzi ili uhukumu watu wangu wenye nimekufanya kuwa mufalme juu yao,+ 12 utapewa hekima na ujuzi; lakini nitakupatia pia mali na utajiri na heshima vyenye hakuna mufalme yeyote mwenye amevipata mbele yako na hakuna mufalme yeyote kisha wewe mwenye atavipata.”+
13 Basi Sulemani akatoka mahali pa juu kule Gibeoni,+ akatoka mbele ya hema ya mukutano, akakuja Yerusalemu; na akatawala juu ya Israeli. 14 Sulemani akaendelea kukusanya magari na farasi;* alikuwa na magari elfu moja mia ine (1 400) na farasi* elfu kumi na mbili (12 000),+ na aliviweka katika miji ya magari+ na karibu na mufalme katika Yerusalemu.+ 15 Mufalme alifanya feza na zahabu katika Yerusalemu ikuwe nyingi kama majiwe,+ na mierezi kuwa mingi kama mikuyu katika Shefela.+ 16 Farasi wa Sulemani waliletwa kutoka Misri,+ na wafanyabiashara wa mufalme walikuwa wanapata makundi ya farasi* kwa bei moja.+ 17 Kila gari lenye lililetwa kutoka Misri lilinunuliwa kwa vipande mia sita (600) vya feza, na farasi mumoja alinunuliwa kwa vipande mia moja makumi tano (150); kisha walikuwa wanaviuzisha kwa wafalme wote wa Wahiti na wafalme wa Siria.