Isaya
24 Angalia! Yehova anafanya inchi* ibakie bila kitu na ikuwe ukiwa.+
Anaipindua*+ na kusambaza wakaaji wake.+
2 Itakuwa sawasawa kwa kila mutu:
Watu na pia kuhani,
Mutumishi na bwana wake,
Mutumishi na bimukubwa wake,
Mwenye kuuza na mwenye kuuzisha,
Mwenye kukopesha na mwenye kukopa,
Mwenye kupana deni na mwenye kuwa na deni.+
3 Inchi itafanywa kuwa bila kitu kabisa,
Vitu vyenye kuwa ndani vitanyanganywa kabisa,+
Kwa maana Yehova amesema neno hilo.
4 Inchi inaomboleza;*+ inakuwa zaifu.
Inchi yenye kuzaa inakauka; inafifia.
Watu wa maana wa inchi wanakauka.
Ndiyo sababu wakaaji wa inchi wamepunguka,
Na wanadamu kidogo sana ndio wamebakia.+
7 Divai mupya inaomboleza,* muzabibu unakauka,+
Na wale wote wenye kuwa na furaha katika moyo wanalia kwa maumivu.+
8 Furaha ya ngoma za kidogo* imeisha;
Makelele ya watu wenye kushangilia yameisha;
Sauti ya furaha ya kinubi imeisha.+
9 Wanakunywa divai bila wimbo;
Na pombe ni yenye uchungu kwa wale wenye kuikunywa.
11 Wanalilia divai katika barabara.
Kushangilia kote kumeisha;
Furaha ya inchi imeisha.+
13 Kwa maana itakuwa hivi katika inchi, kati ya vikundi vya watu:
Kama vile wakati muzeituni unapigwa-pigwa,+
Kama vile kukusanya masalio wakati mavuno ya zabibu yanafikia mwisho.+
14 Watapandisha sauti zao,
Watapiga vigelegele vya shangwe.
Kutoka katika bahari* watatangaza ukubwa wa Yehova.+
15 Ndiyo sababu watamutukuza Yehova katika eneo la mwangaza;*+
Katika visiwa vya bahari watatukuza jina la Yehova Mungu wa Israeli.+
16 Kutoka miisho ya dunia tunasikia nyimbo:
Lakini ninasema: “Ninakuwa muzaifu, ninakuwa muzaifu!
Ole wangu! Wadanganyifu wametenda kwa udanganyifu;
Kwa udanganyifu wadanganyifu wametenda kwa udanganyifu.”+
17 Woga mukubwa na mashimo na mitego vinakungojea, mukaaji wa inchi.+
18 Mutu yeyote mwenye kukimbia sauti yenye kuogopesha sana ataanguka katika shimo,
Na mutu yeyote mwenye kupanda kutoka katika shimo atanaswa katika mutego.+
Kwa maana milango mikubwa ya maji mengi yenye kuwa juu itafunguliwa,
Na misingi ya inchi itatikisika.
20 Inchi inayumba-yumba kama mulevi,
Na inaenda huku na huku kama nyumba ya kidogo katika upepo.
Na makosa yake yameilemea sana,+
Na itaanguka, na hivyo haitasimama tena.
21 Siku hiyo Yehova ataelekeza uangalifu wake kwenye jeshi la nafasi za juu
Na kwa wafalme wa dunia juu ya dunia.
22 Na watakusanywa pamoja,
Kama wafungwa wenye kukusanywa katika shimo
Na watafungiwa katika gereza la chini ya udongo;
Kisha siku nyingi watakaziwa uangalifu.