Esta
10 Mufalme Ahasuero akatumikisha watu wa inchi na visiwa vya bahari kazi ya kulazimishwa.
2 Na matendo yake yote yenye nguvu na ya uwezo, na pia habari zote za ukubwa wa Mordekai+ wenye mufalme alimutukuza,+ je, haziandikwe katika kitabu cha historia ya nyakati+ ya wafalme wa Umedi na Uajemi?+ 3 Kwa maana Mordekai ule Muyahudi alikuwa wa pili kwa cheo kisha tu Mufalme Ahasuero. Alikuwa mukubwa* kati ya Wayahudi na aliheshimiwa na ndugu zake wengi, alitumika kwa faida ya watu wake na alitetea hali njema ya* wazao wao wote.