Esta
6 Usiku huo mufalme hakupata usingizi.* Kwa hiyo, akasema walete kitabu cha historia ya nyakati,+ na wakakisomea mufalme. 2 Wakapata imeandikwa ndani ya kitabu hicho habari yenye Mordekai alikuwa ametoa juu ya Bigtana na Tereshi, maofisa wawili wa makao ya mufalme, walinzi wa milango, wenye walifanya mupango wa kumuua* Mufalme Ahasuero.+ 3 Mufalme akauliza: “Mordekai amepewa heshima na shukrani gani kwa sababu ya mambo hayo?” Watumishi wa mufalme wakasema: “Hajafanyiwa jambo lolote.”
4 Kisha wakati fulani mufalme akasema: “Ni nani mwenye iko* katika kiwanja?” Sasa Hamani alikuwa amekuja katika kiwanja cha inje+ cha nyumba ya mufalme ili azungumuze na mufalme kwamba Mordekai atundikwe kwenye muti wenye alikuwa amemutayarishia.+ 5 Watumishi wa mufalme wakamuambia: “Ni Hamani+ ndiye anasimama katika kiwanja.” Kwa hiyo mufalme akasema: “Mumuingize ndani.”
6 Wakati Hamani aliingia, mufalme akamuambia: “Mutu mwenye mufalme anataka kumuonyesha heshima afanyiwe nini?” Hamani akasema ndani ya moyo wake: “Mufalme angetaka kumuonyesha nani heshima kuliko mimi?”+ 7 Basi Hamani akamuambia mufalme: “Mutu mwenye mufalme anataka kumuonyesha heshima, 8 wamuletee nguo za kifalme+ zenye mufalme anazoea kuvaa na farasi mwenye mufalme anazoea kupanda, mwenye kuwa na taji la kifalme juu ya kichwa chake. 9 Kisha mumoja wa wakubwa wenye vyeo wa mufalme apewe nguo hizo na ule farasi; na wamuvalishe mutu mwenye mufalme anataka kumuonyesha heshima na wamutembeze katika kiwanja cha watu wote cha muji akiwa juu ya farasi. Watangaze kwa sauti kubwa mbele yake: ‘Ni hivi wanamufanyia mutu mwenye mufalme anataka kumuonyesha heshima!’”+ 10 Mara moja mufalme akamuambia Hamani: “Haraka! Kamata nguo hizo na ule farasi, na ufanyie Mordekai ule Muyahudi mwenye kukaa kwenye mulango mukubwa wa mufalme kama vile ulisema. Usiache jambo lolote lenye umesema.”
11 Kwa hiyo Hamani akakamata nguo hizo na ule farasi, akavalisha Mordekai+ na kumutembeza katika kiwanja cha watu wote cha muji akiwa juu ya farasi na kutangaza kwa sauti kubwa mbele yake: “‘Ni hivi wanamufanyia mutu mwenye mufalme anataka kumuonyesha heshima!” 12 Kisha Mordekai akarudia kwenye mulango mukubwa wa mufalme, lakini Hamani akaenda haraka katika nyumba yake, akiomboleza akiwa mwenye kufunika kichwa chake. 13 Wakati Hamani alimuelezea Zereshi+ bibi yake na marafiki wake wote kila jambo lenye lilimupata, wanaume wake wenye hekima na Zereshi bibi yake wakamuambia: “Kama Mordekai, mwenye umeanza kuanguka mbele yake ni muzao wa Wayahudi,* wewe hautamuweza, hakika utaanguka mbele yake.”
14 Wakati walikuwa wangali wanazungumuza naye, maofisa wa makao ya mufalme wakafika na kumupeleka haraka Hamani kwenye karamu yenye Esta alikuwa ametayarisha.+