Esta
9 Katika siku ya kumi na tatu (13) ya mwezi wa kumi na mbili (12), ni kusema, mwezi wa Adari,*+ wakati neno la mufalme na sheria yake ilipaswa kutimizwa,+ siku yenye maadui wa Wayahudi walitumaini kuwashinda, mambo yaligeuka, na Wayahudi wakashinda wale wenye kuwachukia.+ 2 Wayahudi walikusanyika pamoja katika miji yao katika majimbo yote ya* Mufalme Ahasuero+ ili kushambulia wale wenye walitafuta kuwaumiza, na hakuna mutu mwenye aliweza kusimama mbele ya Wayahudi, kwa sababu woga wao ulikuwa umeanguka juu ya vikundi vyote vya watu.+ 3 Na wakubwa wote wa majimbo,* maliwali,+ magavana, na watu wenye walifanya kazi za mufalme waliunga mukono Wayahudi, kwa sababu walimuogopa Mordekai. 4 Mordekai alikuwa amepata mamlaka makubwa+ katika nyumba ya mufalme, na sifa yake iliendelea kuenea katika majimbo yote,* kwa sababu Mordekai aliendelea kuwa na mamlaka makubwa.
5 Wayahudi walipiga na kuua maadui wao wote kwa upanga, waliwaua na kuwaharibu; walitendea wale wenye kuwachukia kama vile walitaka.+ 6 Katika ngome* ya Shushani*+ Wayahudi waliua watu mia tano (500). 7 Pia, walimuua Parshandata, Dalfoni, Aspata, 8 Porata, Adalia, Aridata, 9 Parmashta, Arisai, Aridai, na Vaizata, 10 wana kumi (10) wa Hamani mwana wa Hamedata, adui ya Wayahudi.+ Lakini kisha kuwaua, hawakunyanganya kitu chochote.+
11 Siku hiyo mufalme alijulishwa hesabu ya wale wenye waliuawa katika ngome* ya Shushani.*
12 Mufalme akamuambia Malkia Esta: “Katika ngome* ya Shushani* Wayahudi wameua na kuharibu watu mia tano (500) na wana kumi (10) wa Hamani. Sasa, wamefanya nini katika majimbo mengine ya* mufalme?+ Unataka nini sasa? Utapewa. Na uko na ombi gani lingine? Litafanywa.” 13 Esta akajibu: “Kama inamupendeza mufalme,+ Wayahudi wenye kuwa katika Shushani* wapewe ruhusa ya kufanya pia kulingana na sheria ya leo;+ na wana kumi (10) wa Hamani watundikwe kwenye muti.”+ 14 Kwa hiyo mufalme akatoa amri ili jambo hilo lifanywe. Sheria ikatolewa katika Shushani,* na wana kumi (10) wa Hamani wakatundikwa.
15 Wayahudi wenye walikuwa katika Shushani* wakakusanyika tena pamoja siku ya kumi na ine (14) ya mwezi wa Adari,+ na wakaua watu mia tatu (300) katika Shushani,* lakini hawakunyanganya kitu chochote.
16 Wayahudi wengine wenye walikuwa katika majimbo ya* mufalme, wakakusanyika pamoja na kupigania uzima wao.+ Wakaangamiza maadui wao,+ wakaua watu elfu makumi saba na tano (75 000) kati ya wale wenye kuwachukia; lakini hawakunyanganya kitu chochote. 17 Mambo hayo yalifanyika siku ya kumi na tatu (13) ya mwezi wa Adari, na walipumuzika siku ya kumi na ine (14) na waliifanya kuwa siku ya karamu na kushangilia.
18 Wayahudi wenye walikuwa katika Shushani,* walikusanyika pamoja siku ya kumi na tatu (13)+ na ya kumi na ine (14),+ na walipumuzika siku ya kumi na tano (15) na waliifanya kuwa siku ya karamu na kushangilia. 19 Ndiyo sababu Wayahudi wa maeneo ya mashamba wenye walikaa katika miji ya wilaya za pembeni-pembeni walifanya siku ya kumi na ine (14) ya mwezi wa Adari kuwa siku ya kushangilia na ya karamu, siku ya sherehe,+ na wakati wa kutumiana mafungu ya chakula.+
20 Mordekai+ akaandika matukio hayo na akatuma barua kwa Wayahudi wote wenye walikuwa katika majimbo yote ya* Mufalme Ahasuero, ya karibu na ya mbali. 21 Akawaagiza wakuwe wanakumbuka siku ya kumi na ine (14) ya mwezi wa Adari, na pia siku ya kumi na tano (15), ya kila mwaka, 22 kwa maana katika siku hizo Wayahudi waliacha kusumbuliwa na maadui wao na katika mwezi huo huzuni yao iligeuka kuwa shangwe na maombolezo yao+ kuwa siku ya sherehe. Walipaswa kufanya siku hizo kuwa siku za karamu na shangwe na wakati wa kutumiana mafungu ya chakula na kupatia maskini zawadi.
23 Na Wayahudi wakakubali kuendelea kufanya sherehe yenye walikuwa wameanza na kufanya mambo yenye Mordekai aliwaandikia. 24 Kwa maana Hamani+ mwana wa Hamedata Mwagagi,+ adui ya Wayahudi wote, alikuwa amefanya mupango wa kuharibu Wayahudi,+ na alikuwa amepiga Puri,+ ni kusema, Kura, ili kuwaogopesha na kuwaharibu. 25 Lakini wakati Esta aliingia mbele ya mufalme, mufalme alitoa amri zenye ziliandikwa:+ “Mupango wake mubaya juu ya Wayahudi+ urudie juu ya kichwa chake mwenyewe”; na walimutundika Hamani na wana wake kwenye muti.+ 26 Ndiyo sababu waliita siku hizo Purimu, kutokana na jina la Puri.*+ Basi, kwa sababu ya mambo yote yenye yaliandikwa katika barua hiyo na mambo yenye walijionea kuhusu jambo hilo na mambo yenye yalikuwa yamewapata, 27 Wayahudi wenyewe na wazao wao na wote wenye walijiunga nao+ wakajiwekea sheria ya kuwa wanakumbuka siku hizo mbili bila kukosea na kufanya mambo yenye yaliandikwa kuwahusu kwa wakati wenye uliwekwa kila mwaka. 28 Siku hizo zilipaswa kukumbukwa na kufanywa katika kila kizazi, kila familia, kila jimbo,* na kila muji; na siku hizo za Purimu hazikupaswa kusahauliwa kati ya Wayahudi, na ukumbusho wa siku hizo haukupaswa kuisha kati ya wazao wao.
29 Kisha Malkia Esta, binti ya Abihaili, na Mordekai ule Muyahudi wakaandika kwa mamlaka yote ili kutoa uhakikisho kuhusu barua ya pili juu ya Purimu. 30 Mordekai akatuma barua kwa Wayahudi wote katika majimbo* mia moja makumi mbili na saba (127)+ ya utawala wa Ahasuero,+ kwa maneno ya amani na kweli 31 ili kutoa uhakikisho kuhusu kukumbuka siku za Purimu wakati wenye uliwekwa, kama vile Mordekai ule Muyahudi na Malkia Esta walikuwa wamewaagiza wafanye+ na kama vile walikuwa wamejiwekea sheria wenyewe* na wazao wao ili kutimiza,+ na pia kufunga+ na kutoa sala ya kumulilia Mungu.*+ 32 Na amri ya Esta ikatoa uhakikisho kuhusu mambo hayo ya Purimu,+ na yakaandikwa katika kitabu.