Kumbukumbu la Torati
11 “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako+ na kutimiza sikuzote mambo yenye anakuomba ufanye na sheria zake, maamuzi yake ya hukumu, na amri zake. 2 Munajua kama leo ninazungumuza na ninyi, sizungumuze na wana wenu wenye hawajajua wala kuona nizamu ya Yehova Mungu wenu,+ ukubwa wake,+ mukono wake wenye nguvu+ na mukono wake wenye kunyooshwa. 3 Hawakuona alama zake na matendo yake yenye alimutendea Farao mufalme wa Misri katika Misri na inchi yake yote;+ 4 wala mambo yenye alitendea majeshi ya Misri, farasi za Farao na magari yake ya vita, yenye yalifunikwa na maji ya Bahari Nyekundu wakati walikuwa wanawafuatilia ninyi, na Yehova akawaharibu milele.*+ 5 Hawakuona mambo yenye aliwatendea katika jangwa mupaka wakati mulifika mahali hapa, 6 wala mambo yenye alitendea Datani na Abiramu, wana wa Eliabu mwana wa Rubeni, wakati dunia ilifunguka na kuwameza, pamoja na watu wa nyumba zao na mahema yao na kila kiumbe chenye kuishi chenye kiliwafuata, mbele ya macho ya Israeli wote.+ 7 Macho yenu wenyewe yameona matendo yote makubwa yenye Yehova alifanya.
8 “Munapaswa kushika amri yote yenye ninawapatia leo, kusudi mukuwe na nguvu na kuvuka ili kuingia katika inchi hiyo kusudi muiriti, 9 na ili muishi wakati murefu+ katika inchi yenye Yehova aliapa kwamba atapatia mababu zenu na uzao wao,*+ inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+
10 “Inchi yenye unaenda kuriti haiko kama vile inchi ya Misri, kwenye mulitoka, kwenye ulikuwa unapanda mbegu zako na kuzimwangilia maji kwa muguu wako,* kama vile bustani ya mboga za majani. 11 Lakini inchi yenye munakaribia kuvuka kuingia ndani na kuiriti ni inchi ya milima na mabonde tambarare.+ Inakunywa maji ya mvua kutoka mbinguni;+ 12 ni inchi yenye Yehova Mungu wako anatunza. Macho ya Yehova Mungu wako yako juu ya inchi hiyo sikuzote, kuanzia mwanzo wa mwaka mupaka mwisho wa mwaka.
13 “Na kama mutatii kwa bidii amri zangu zenye ninawaamuru leo na kumupenda Yehova Mungu wenu na kumutumikia kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote,+ 14 nitawapatia pia mvua kwa ajili ya inchi yenu kwa wakati wake wenye uliwekwa, mvua ya kipindi cha mvua ya kwanza na mvua ya kipindi cha mvua ya mwisho, na utakusanya nafaka yako na divai yako mupya na mafuta yako.+ 15 Na nitaotesha majani katika mashamba yako kwa ajili ya mifugo yako, na utakula na kushiba.+ 16 Mukuwe waangalifu ili musiache mioyo yenu ishawishiwe kupotoka na kuabudu miungu mingine na kuiinamia.+ 17 Kama hamufanye vile, kasirani ya Yehova itawaka juu yenu, na atafunga mbingu ili mvua isinyeshe+ na udongo hautazaa mazao yake na mutaangamia haraka katika inchi ya muzuri yenye Yehova anawapatia.+
18 “Munapaswa kukazia maneno yangu haya katika moyo wenu na nafsi* yenu na kuyafunga kama kikumbusho kwenye mukono wenu, na yanapaswa kuwa kama utepe wa kichwa kwenye paji la uso wenu.*+ 19 Muyafundishe watoto wenu, na kuongea kuyahusu wakati unakaa katika nyumba yako na wakati unatembea katika barabara na wakati unalala na wakati unaamuka.+ 20 Uyaandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na kwenye milango yako mikubwa, 21 ili ninyi na wana wenu muishi wakati murefu+ katika inchi yenye Yehova aliapa kwamba atapatia mababu zenu,+ sikuzote zenye mbingu zitakuwa juu ya dunia.
22 “Kama munashika kabisa amri hii yenye ninawapatia na kuitenda, kumupenda Yehova Mungu wenu,+ kutembea katika njia zake zote na kushikamana naye,+ 23 Yehova atafukuza mataifa haya yote mbele yenu,+ na mutakamata inchi ya mataifa makubwa zaidi na yenye watu wengi zaidi kuliko ninyi.+ 24 Kila mahali kwenye mutakanyanga kwa muguu wenu patakuwa penu.+ Mupaka wenu utaanzia katika jangwa kufikia Lebanoni, kuanzia ule Muto, muto Efrati, kufikia kwenye bahari ya mangaribi.*+ 25 Hakuna mutu mwenye atasimama mbele yenu.+ Yehova Mungu wenu ataeneza hofu na woga wenu juu ya inchi yote yenye mutatembea juu yake,+ kama vile aliwaahidi.
26 “Angalia, ninatia mbele yenu leo baraka na laana:+ 27 baraka kama munatii amri za Yehova Mungu wenu zenye ninawaamuru leo,+ 28 na laana kama hamutii amri za Yehova Mungu wenu+ na munageuka kutoka katika njia yenye ninawaamuru mufuate leo na munafuata miungu yenye hamukujua.
29 “Wakati Yehova Mungu wako atakuingiza katika inchi yenye utariti, unapaswa kutangaza* baraka kwenye Mulima Gerizimu na laana kwenye Mulima Ebali.+ 30 Je, milima hiyo haiko ngambo ingine ya Yordani kuelekea mangaribi,* katika inchi ya Wakanaani wenye wanaishi Araba, mbele ya Gilgali, pembeni ya ile miti mikubwa ya More?+ 31 Kwa maana munavuka Yordani ili muingie na kuriti inchi yenye Yehova Mungu wenu anawapatia.+ Wakati mutairiti na kuishi ndani yake, 32 munapaswa kuwa waangalifu ili kushika masharti na maamuzi ya hukumu yenye ninatia mbele yenu leo.+