Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
23 Wakati Daudi alikuwa amezeeka na kukaribia mwisho wa maisha yake,* alimufanya Sulemani mwana wake kuwa mufalme juu ya Israeli.+ 2 Kisha akakusanya wakubwa wote wa Israeli, makuhani,+ na Walawi.+ 3 Walawi wenye walikuwa na miaka makumi tatu (30) na zaidi walihesabiwa;+ hesabu yao, kichwa kwa kichwa, mwanaume kwa mwanaume, ilikuwa elfu makumi tatu na munane (38 000). 4 Kati yao, watu elfu makumi mbili na ine (24 000) walitumika wakiwa viongozi wa kazi ya nyumba ya Yehova, na kulikuwa maofisa na waamuzi elfu sita (6 000),+ 5 na kulikuwa walinzi elfu ine (4 000) wa milango mikubwa,+ na watu elfu ine walimusifu+ Yehova kwa vyombo vyenye Daudi alisema hivi juu yavyo: “Nilivitengeneza kwa ajili ya kutoa sifa.”
6 Kisha Daudi akawapanga* katika vikundi+ kulingana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohati, na Merari.+ 7 Kati ya Wagershoni kulikuwa Ladani na Shimei. 8 Wana wa Ladani walikuwa Yehieli kichwa, Zetamu, na Yoeli,+ watatu (3). 9 Wana wa Shimei walikuwa Shelomoti, Hazieli, na Harani, watatu (3). Hao ndio walikuwa vichwa vya jamaa za upande wa baba kwa ajili ya Ladani. 10 Na wana wa Shimei walikuwa Yahati, Zina, Yeushi, na Beria. Hao ine (4) walikuwa wana wa Shimei. 11 Yahati alikuwa kichwa, na Ziza alikuwa wa pili. Lakini kwa kuwa Yeushi na Beria hawakukuwa na wana wengi, walihesabiwa kama jamaa moja ya upande wa baba wakiwa na daraka lilelile.
12 Wana wa Kohati walikuwa Amramu, Ishari,+ Hebroni, na Uzieli,+ ine (4). 13 Wana wa Amramu walikuwa Haruni+ na Musa.+ Lakini Haruni aliwekwa pembeni wakati wote+ ili atakase Patakatifu Zaidi, yeye na wana wake, ili watoe zabihu mbele ya Yehova, wamutolee utumishi, na kutangaza baraka katika jina lake sikuzote.+ 14 Na kuhusu Musa, mutu wa Mungu wa kweli, wana wake walihesabiwa kati ya kabila la Walawi. 15 Wana wa Musa walikuwa Gershomu+ na Eliezeri.+ 16 Kati ya wana wa Gershomu, Shebueli+ alikuwa kichwa. 17 Kati ya wazao* wa Eliezeri, Rehabia+ alikuwa kichwa; Eliezeri hakukuwa na wana wengine, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana. 18 Kati ya wana wa Ishari,+ Shelomiti+ alikuwa kichwa. 19 Wana wa Hebroni walikuwa Yeria kichwa, wa pili Amaria, wa tatu (3) Yahazieli, na wa ine (4) Yekameamu.+ 20 Wana wa Uzieli+ walikuwa Mika kichwa, na wa pili Ishia.
21 Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi.+ Wana wa Mali walikuwa Eleazari na Kishi. 22 Eleazari alikufa, lakini hakukuwa na watoto wanaume, alikuwa na watoto wanamuke tu. Basi wana wa Kishi, watu wa jamaa yao,* waliwachukua wakuwe bibi zao. 23 Wana wa Mushi walikuwa Mali, Ederi, na Yeremoti, watatu (3).
24 Hao ndio walikuwa wana wa Lawi kulingana na jamaa zao za upande wa baba, vichwa vya jamaa za upande wa baba, kupitia wale wenye waliandikishwa wenye walihesabiwa na kupangwa kulingana na majina yao na wenye walitimiza kazi kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Yehova, kuanzia miaka makumi mbili (20) kuenda juu. 25 Kwa maana Daudi alikuwa amesema: “Yehova Mungu wa Israeli amepatia watu wake pumuziko,+ na atakaa katika Yerusalemu milele. + 26 Pia Walawi hawatalazimika kubeba tabenakulo ao kifaa chake chochote chenye kinatumiwa kwa ajili ya utumishi wake.”+ 27 Kwa maana kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi wenye miaka kuanzia makumi mbili (20) kuenda juu walihesabiwa. 28 Kazi yao ilikuwa kusaidia wana wa Haruni+ kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Yehova, kusimamia viwanja,+ vyumba vya kukulia chakula, kutakaswa kwa kila kitu kitakatifu, na kazi yoyote yenye ilihitajiwa kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli. 29 Walisaidia katika kazi ya mikate yenye kupangwa moja juu ya ingine,*+ unga muzuri wa toleo la nafaka, mikate myembamba yenye haina chachu,+ keki zenye ziliokwa, donge lenye lilichanganywa,+ na vipimo vyote vya wingi na ukubwa. 30 Walipaswa kusimama kila asubui+ ili kumushukuru na kumusifu Yehova na walipaswa kufanya vilevile mangaribi.+ 31 Walisaidia wakati wowote wenye zabihu za kuteketezwa zilitolewa kwa Yehova katika siku za Sabato,+ miezi mipya,+ na wakati wa vipindi vya sikukuu,+ kulingana na hesabu yenye iliombwa na sheria kuzihusu, walifanya vile kwa ukawaida mbele ya Yehova. 32 Walitimiza pia madaraka yao kuelekea hema ya mukutano, kuelekea mahali patakatifu, na kuelekea ndugu zao wana wa Haruni kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Yehova.