Isaya
38 Katika siku hizo Hezekia akakuwa mugonjwa na alikuwa karibu kufa.+ Nabii Isaya+ mwana wa Amozi akakuja na kumuambia, “Yehova anasema hivi: ‘Patia nyumba yako maagizo, kwa maana utakufa; hautapona.’”+ 2 Basi Hezekia akageuza uso wake kuelekea ukuta na kuanza kusali kwa Yehova: 3 “Ninakuomba, Ee Yehova, kumbuka,+ tafazali, namna nimetembea mbele yako kwa uaminifu na kwa moyo kamili,+ na nimetenda mambo mema mbele ya macho yako.” Na Hezekia akaanza kulia sana.
4 Kisha neno la Yehova likakuja kwa Isaya, na kusema: 5 “Rudia na umuambie Hezekia,+ ‘Yehova, Mungu wa Daudi babu yako anasema hivi: “Nimesikia sala yako.+ Nimeona machozi yako.+ Angalia, ninaongeza miaka kumi na tano (15) kwenye maisha yako,*+ 6 na nitakuokoa wewe na muji huu kutoka katika mukono wa mufalme wa Ashuru, na nitalinda muji huu.+ 7 Hii ndiyo alama kutoka kwa Yehova yenye itakuonyesha kwamba Yehova atatimiza neno lenye amesema:+ 8 Nitafanya kivuli cha jua chenye kushuka kwenye ngazi* ya Ahazi kirudie nyuma hatua kumi (10).”’”+ Basi jua likarudia nyuma hatua kumi kwenye ngazi zenye tayari lilikuwa limeshuka.
9 Haya ni maandishi ya* Mufalme Hezekia wa Yuda, wakati alishikwa na ugonjwa na kupona ugonjwa wake.
10 Nilisema: “Katikati ya maisha yangu
Lazima niingie katika milango mikubwa ya Kaburi.*
Nitaimwa miaka yangu yenye inabakia.”
11 Nilisema: “Sitamuona Yah,* Yah katika inchi ya wazima.+
Sitaona tena wanadamu
Wakati nitakuwa pamoja na wakaaji wa mahali kwenye kila kitu kinafikia mwisho.
12 Makao yangu yamengolewa na kupelekwa mbali na mimi+
Kama hema ya muchungaji.
Nimekunja uzima wangu kama musukaji wa nguo;
Ananikata kama nyuzi za murefu zenye kutoka juu kuenda chini.*
Kuanzia mapambazuko* mupaka wakati giza linaingia unaendelea kunileta kwenye mwisho.+
13 Nimejituliza mupaka asubui.
Kama simba, anaendelea kuvunja mifupa yangu yote;
Kuanzia mapambazuko* mupaka wakati giza linaingia unaendelea kunileta kwenye mwisho.+
Macho yangu yameangalia nafasi ya juu kwa uchovu:+
15 Niseme nini?
Amezungumuza na mimi na kutenda.
16 ‘Ee Yehova, kila mwanadamu anaishi kwa mambo hayo,*
Na uzima wa roho yangu uko katika mambo hayo.
Utanirudishia afya ya muzuri na kulinda uzima wangu.+
17 Angalia! Kuliko kuwa na amani, nilikuwa na uchungu mwingi;
Lakini kwa sababu ulinipenda sana*
Ulinilinda nisiingie katika shimo la uharibifu.+
Kwa maana umetupa zambi zangu zote nyuma ya mugongo wako.*+
Wale wenye kushuka katika shimo hawawezi kutumainia uaminifu wako.+
19 Wazima, wazima wanaweza kukusifu,
Kama vile ninaweza kukusifu leo hii.
Baba anaweza kupatia wana wake ujuzi kuhusu uaminifu wako.+
20 Ee Yehova, uniokoe
Na tutapiga nyimbo zangu kwa vyombo vya kamba+
Siku zote za maisha yetu katika nyumba ya Yehova.’”+
21 Kisha Isaya akasema: “Mulete keki ya tini zenye kukauka zenye zilifinywa-finywa na muitie kwenye jipu hilo, ili apone.”+ 22 Hezekia alikuwa ameuliza: “Ni nini alama ya kwamba nitapanda kuenda kwenye nyumba ya Yehova?”+