Kumbukumbu la Torati
25 “Wakati mabishano yanatokea katikati ya watu, wanaweza kuenda mbele ya waamuzi,+ na waamuzi watawaamua na kumutangaza mwenye haki kwamba hana hatia na mutu muovu kwamba iko* na hatia.+ 2 Kama mutu muovu anastahili kupigwa,+ muamuzi atamufanya alale uso chini, na atapigwa mbele yake. Hesabu ya viboko inapaswa kulingana na uovu wa jambo lenye alifanya. 3 Anaweza kumupiga kufikia viboko makumi ine (40),+ lakini hapana zaidi. Kama anaendelea kumupiga viboko zaidi kuliko viboko hivyo, ndugu yako atapata haya mbele ya macho yako.
4 “Haupaswe kufunga kinywa cha ngombe-dume wakati anakanyanga-kanyanga nafaka.+
5 “Kama ndugu wanaishi pamoja na mumoja wao anakufa bila kupata mwana, bibi ya ule mwenye alikufa hataolewa na mutu fulani inje ya familia hiyo. Shemeki yake ataenda kwake, atamuchukua akuwe bibi yake, na kufunga naye ndoa ya mutu na shemeki yake.+ 6 Muzaliwa wa kwanza mwenye bibi huyo atazaa ataendeleza jina la ndugu yake mwenye alikufa,+ ili jina lake lisifutwe katikati ya Israeli.+
7 “Sasa kama mwanaume huyo hataki kuoa mujane wa ndugu yake, basi mujane wa ndugu yake ataenda kwa wazee kwenye mulango mukubwa wa muji na kusema, ‘Ndugu ya bwana yangu amekataa kulinda jina la ndugu yake katika Israeli. Amekataa kufunga na mimi ndoa ya mutu na shemeki yake.’ 8 Wazee wa muji wake wanapaswa kumuita na kuzungumuza naye. Kama anakazana na kusema, ‘Sitaki kumuoa,’ 9 basi mujane wa ndugu yake atamukaribia mbele ya wazee, atatosha kiatu cha mwanaume huyo kwenye muguu wake,+ atamutemea mate katika uso wake, na kusema, ‘Ni vile anapaswa kutendewa mwanaume mwenye hatajenga nyumba ya ndugu yake.’ 10 Kisha mambo hayo jina la familia yake* katika Israeli litakuwa ‘Nyumba ya mutu mwenye alitoshwa kiatu.’
11 “Kama wanaume wawili wanapigana na bibi ya mumoja wao anaingilia kati ili kumulinda bwana yake kutokana na ule mwenye kumupiga na ananyoosha mukono wake na kukamata sehemu za siri za ule mwenye kupiga bwana yake, 12 unapaswa kumukata mukono mwanamuke huyo. Haupaswe* kusikia huruma.
13 “Haupaswe kuwa na namna mbili ya majiwe ya kupimia katika mufuko wako,+ jiwe la mukubwa na jiwe la kidogo. 14 Haupaswe kuwa na namna mbili ya vyombo vya kupimia* katika nyumba yako,+ kikubwa na kidogo. 15 Unapaswa kuwa na jiwe la kupimia lenye kuwa sawa na la haki na kipimo chenye kuwa sawa na cha haki, ili uishi wakati murefu katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia.+ 16 Kwa maana kila mutu mwenye hatende haki mwenye anafanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova Mungu wako.+
17 “Kumbuka mambo yenye Amaleki alikutendea katika njia wakati ulikuwa unatoka Misri,+ 18 namna alikutana na wewe katika njia na kushambulia wale wote wenye walikuwa wanajikokota nyuma yako wakati ulikuwa umechoka na kuishiwa nguvu. Hakumuogopa Mungu. 19 Wakati Yehova Mungu wako atakuwa amekupatia pumuziko kutokana na maadui wako wote wenye kukuzunguka katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia kuwa uriti ili uikamate,+ unapaswa kufuta jina la Amaleki chini ya mbingu.+ Haupaswe kusahau.