Rutu
2 Basi Naomi alikuwa na mutu mumoja wa jamaa ya upande wa bwana yake mwenye alikuwa tajiri sana; jina lake lilikuwa Boazi,+ na alikuwa wa familia ya Elimeleki.
2 Rutu Mumoabu akamuambia Naomi: “Tafazali, uniache niende katika mashamba ili niokote masalio+ kati ya masuke ya nafaka nyuma ya mutu yeyote mwenye atanikubali.” Basi Naomi akamuambia: “Uende, binti yangu.” 3 Kwa hiyo akaenda na kuanza kuokota masalio katika shamba nyuma ya wavunaji. Bila kujua akajikuta katika shamba la Boazi,+ mwenye alikuwa wa familia ya Elimeleki.+ 4 Kisha Boazi akafika kutoka Betlehemu na akasalimia wavunaji: “Yehova akuwe pamoja na ninyi.” Nao wakajibu: “Yehova akubariki.”
5 Kisha Boazi akamuuliza kijana mwanaume mwenye alikuwa musimamizi wa wavunaji: “Huyu kijana mwanamuke ni wa nani?” 6 Kijana huyo mwanaume mwenye alikuwa musimamizi wa wavunaji akamujibu: “Huyu kijana mwanamuke ni Mumoabu+ mwenye alikuja na Naomi kutoka katika maeneo ya mashamba ya Moabu.+ 7 Aliniuliza, ‘Tafazali, ninaweza kuokota+ na kukusanya masalio kati ya masuke* yenye kukatwa ya nafaka yenye wavunaji waliacha nyuma?’ Na hajakaa tangu wakati alifika asubui hii mupaka sasa, na ni sasa tu ndio amekaa katika kibanda ili kupumuzika kidogo.”
8 Kisha Boazi akamuambia Rutu: “Sikiliza, binti yangu. Usiende kuokota masalio katika shamba lingine, wala usiende mahali pengine popote; bakia karibu na vijana wangu wanamuke.+ 9 Endelea kuangalia shamba lenye wanavuna, na uwafuate. Nimeamuru vijana wanaume wasikuguse.* Ukisikia kiu, uende kwenye mitungi ukunywe maji yenye vijana hao wanaume wameshota.”
10 Kwa hiyo akaanguka uso chini na kuinama mupaka chini na kumuambia: “Namna gani nimekubaliwa mbele ya macho yako, na sababu gani umenitambua, ijapokuwa mimi ni mugeni?”+ 11 Boazi akamujibu: “Wameniambia mambo yote yenye ulimufanyia mama-mukwe wako kisha bwana yako kufa na namna uliacha baba yako na mama yako na inchi ya watu wa jamaa yako na ukakuja kwa watu wenye haukukuwa unajua zamani.+ 12 Yehova akupatie zawabu kwa sababu ya mambo yenye ulifanya,+ na upate malipo kamili* kutoka kwa Yehova Mungu wa Israeli, mwenye umekuja kutafuta ulinzi chini ya mabawa yake.”+ 13 Basi Rutu akasema: “Acha nikubaliwe mbele ya macho yako, bwana wangu. Umenifariji na kusema na mutumishi wako kwa njia yenye kutuliza,* ijapokuwa mimi siko mumoja wa watumishi wako.”
14 Basi wakati wa kula, Boazi akamuambia: “Kuja hapa, ukule mukate na kuutia katika siki.”* Basi akakaa pembeni ya wavunaji. Boazi akamupatia nafaka yenye kukaangwa. Akakula, akashiba, na akaacha zingine. 15 Wakati alisimama ili aokote masalio,+ Boazi akaamuru vijana wake wanaume: “Mumuache aokote pia kati ya masalio ya masuke* yenye kukatwa ya nafaka, na musimutendee mubaya.+ 16 Pia, muhakikishe kwamba mumeondoa masuke fulani ya nafaka katika mafungu-mafungu na muyaache nyuma ili ayaokote, na musiseme jambo lolote ili kumukataza.”
17 Basi akaendelea kuokota masalio katika shamba mupaka mangaribi.+ Kisha kupiga-piga masalio yenye alikuwa ameokota, akapata karibu efa* moja ya shayiri. 18 Halafu akayakamata na kuenda katika muji, na mama-mukwe wake akaona masalio yenye alikuwa ameokota. Na Rutu akakamata chakula chenye aliacha+ kisha kushiba, akamupatia mama-mukwe wake.
19 Basi mama-mukwe wake akamuuliza: “Leo uliokota masalio wapi? Ulifanya kazi wapi? Abarikiwe mutu mwenye alikuona.”+ Kwa hiyo akamuelezea mama-mukwe wake kuhusu mutu mwenye alitumika naye, akasema: “Mwanaume mwenye nilitumika naye leo jina lake Boazi.” 20 Basi Naomi akamuambia binti-mukwe wake: “Mutu huyo abarikiwe na Yehova, mwenye hajakosa kuonyesha upendo mushikamanifu kwa wazima na wafu.”+ Naomi akaendelea kusema: “Mwanaume huyo ni mutu wa jamaa yetu.+ Ni mumoja wa wakombozi wetu.”*+ 21 Kwa hiyo Rutu Mumoabu akasema: “Aliniambia pia, ‘Ubakie karibu na vijana wangu mupaka wakati watamaliza mavuno yangu yote.’”+ 22 Basi Naomi akamuambia Rutu binti-mukwe wake: “Binti yangu, ni muzuri zaidi ufuatane na vijana wake wanamuke kuliko kusumbuliwa katika shamba lingine.”
23 Kwa hiyo akabakia karibu na vijana wanamuke wa Boazi na akaokota masalio+ mupaka mwisho wa mavuno ya shayiri na ya ngano. Na akaendelea kuishi pamoja na mama-mukwe wake.+