Wimbo wa Sulemani
5 “Nimeingia katika bustani yangu,+
Ee dada yangu, bibi-arusi wangu.
Nimechuma manemane pamoja na manukato yangu.+
Nimekula sega la asali na asali yangu;
Nimekunywa divai yangu na maziwa yangu.”+
“Mukule, marafiki wangu!
Mukunywe na mulewe maonyesho ya upendo!”+
2 “Nimelala, lakini moyo wangu uko macho.+
Kuko sauti ya mupenzi wangu akipiga hodi!
‘Unifungulie, Ee dada yangu, mupenzi wangu,
Njiwa wangu, wangu mwenye hana kasoro!
Kwa maana kichwa changu kimelowana umande,
Mashungi ya nywele zangu yamejaa umajimaji wa usiku.’+
3 Nimetosha kanzu yangu.
Niivae tena?
Nimenawisha miguu yangu.
Niichafue tena?
4 Mupenzi wangu aliondoa mukono wake kwenye tundu la mulango,
Na hisia zangu kumuelekea zikaamushwa.
5 Nilisimama ili nimufungulie mupenzi wangu;
Mikono yangu ikaangusha matone-matone ya manemane,
Na vidole vyangu manemane ya maji,
Ikaangukia kwenye mikono ya kifungio cha mulango.
6 Nilimufungulia mupenzi wangu,
Lakini mupenzi wangu alikuwa amegeuka, alikuwa ameenda zake.
Nilivunjika moyo* wakati alienda.*
Nilimutafuta, lakini sikumupata.+
Nikamuita, lakini hakunijibu.
7 Walinzi wenye walikuwa wanazunguka katika muji walinipata.
Wakanipiga, wakaniumiza.
Walinzi wa kuta wakaninyanganya kitambaa changu kikubwa.*
8 Ninawaapisha, Enyi mabinti wa Yerusalemu:
Kama munamupata mupenzi wangu,
Mumuambie kwamba ninagonjwa ugonjwa wa mapenzi.”
9 “Mupenzi wako anashindia wapenzi wengine wote na nini,
Wewe mwenye sura na umbo ya muzuri sana kuliko wanamuke wote?
Mupenzi wako anashindia wapenzi wengine wote na nini,
Ili utuapishe vile?”
10 “Mupenzi wangu anangaa na ni mwekundu;
Anavutia zaidi kati ya wanaume elfu kumi (10 000).
11 Kichwa chake ni zahabu, zahabu safi sana.
Mashungi ya nywele zake ni kama majani ya muti wa mutende yenye kutikisika.*
Ni meusi kama kunguru.
12 Macho yake ni kama njiwa pembeni ya mito midogo ya maji,
Wananawa miili yao ndani ya maziwa,
Wamekaa pembeni ya kiziwa cha maji chenye kujaa sana.*
13 Mashavu yake ni kama bustani ya manukato,+
Vilima vya mimea yenye harufu ya muzuri.
Midomo yake ni maua ya mayungiyungi, yanaangusha matone-matone ya manemane ya maji.+
14 Mikono yake ni viviringo vya zahabu, vyenye kupambwa na krisolito.
Tumbo lake ni pembe ya tembo yenye kungarishwa na kupambwa na yakuti.
15 Miguu yake ni nguzo za marumaru zenye kuwekwa kwenye vikalio vya zahabu safi.
Sura yake ni kama Lebanoni, ni ya muzuri sana kama miti ya mierezi.+
Huyo ndiye mupenzi wangu, huyo ndiye mupendwa wangu, Enyi mabinti wa Yerusalemu.”