Mika
1 Neno la Yehova lenye lilikuja kwa Mika*+ wa Moresheti, katika siku za Yotamu,+ Ahazi,+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda,+ lenye alipata katika maono kuhusu Samaria na Yerusalemu:
2 “Musikie, ninyi vikundi vyote vya watu!
Sikiliza, Ee dunia na vitu vyote vyenye kujaa ndani yako,
Na Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova akuwe shahidi juu yenu,+
—Yehova katika hekalu lake takatifu.
3 Kwa maana angalia! Yehova anatoka mahali pake;
Atashuka na kukanyanga mahali kwenye kuinuka katika dunia.
4 Milima itayeyuka chini yake,+
Na mabonde* yatapasuka
Kama nta* karibu na moto,
Kama maji yenye kumwangwa kwenye muteremuko mukali.
Uasi wa Yakobo ni nini?
Haiko Samaria?+
Mahali pa juu pa Yuda ni nini?+
Haiko Yerusalemu?
6 Nitafanya Samaria kuwa rundo la mabomoko katika shamba,
Mahali pa kupanda mizabibu;
Nitatupa* majiwe yake katika bonde,
Na nitafunua misingi yake.
7 Sanamu zake zote za kuchongwa zitavunjwa-vunjwa,+
Na zawadi zote zenye alilipwa kwa sababu ya ukahaba wake zitateketezwa* kwa moto.+
Nitaharibu sanamu zake zote.
Kwa sababu alizikusanya kutokana na malipo ya ukahaba,
Na zitakuwa tena malipo ya makahaba.”
Nitalia kama mbweha,
Na kuomboleza kama mbuni.
Pigo hilo limeenea mupaka kwenye mulango mukubwa wa watu wangu, mupaka Yerusalemu.+
10 “Musitangaze jambo hili katika Gati;
Musilie hata kidogo.
Katika Bet-afra* mujizungushe-zungushe katika mavumbi.
11 Muende mukiwa uchi na wenye haya, Enyi wakaaji* wa Shafiri.
Wakaaji wa Saanani hawajatokea.*
Katika Bet-ezeli watu watalia, itaondoa tegemeo lao kutoka kwenu.
12 Kwa sababu wakaaji wa Maroti wamengojea* mambo ya muzuri,
Lakini mambo ya mubaya yameshuka kutoka kwa Yehova mupaka kwenye mulango mukubwa wa Yerusalemu.
13 Mufunge gari kwenye kikundi cha farasi, Enyi wakaaji* wa Lakishi.+
Ninyi ndio muliingiza binti ya Sayuni katika zambi,
Kwa maana uasi wa Israeli umepatikana ndani yenu.+
14 Kwa hiyo mutapatia Moreshet-gati zawadi za kuagana.*
Nyumba za Akzibu+ zilikuwa kitu cha kudanganya kwa wafalme wa Israeli.
15 Bado nitawaletea mushindi,*+ Enyi wakaaji* wa Maresha.+
Utukufu wa Israeli utafika Adulamu.+
16 Mujifanyie vipara na munyoe nywele zenu kwa sababu ya watoto wenu wapendwa.
Mujifanyie vipara kama vya tai,
Kwa maana wamepelekwa mbali na wewe, katika uhamisho.”+