Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 31
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 2 Mambo ya Nyakati

      • Hezekia anangoa uasi-imani (1)

      • Makuhani na Walawi wanategemezwa kwa njia yenye kufaa (2-21)

2 Mambo ya Nyakati 31:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Maana ya Maneno.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 23:24
  • +Kum 7:5; 2 Fal. 18:1, 4; 2Nya 14:2, 3; 34:1, 3
  • +Kum 12:2
  • +2Nya 23:16, 17
  • +2Nya 30:1, 18

2 Mambo ya Nyakati 31:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kambi za.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 24:1
  • +1Nya 23:6
  • +2Nya 8:14
  • +1Nya 23:13, 27-30

2 Mambo ya Nyakati 31:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 30:24
  • +Kut 29:39
  • +Hes 28:9
  • +Hes 10:10
  • +Kum 16:16

2 Mambo ya Nyakati 31:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wajitoe kikamili kwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 18:21; Ne 10:38, 39

2 Mambo ya Nyakati 31:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 18:12
  • +Kut 22:29; 23:19; Ne 10:37
  • +Mez. 3:9

2 Mambo ya Nyakati 31:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 27:30; Kum 14:28

2 Mambo ya Nyakati 31:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 23:16
  • +Law. 23:24

2 Mambo ya Nyakati 31:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 18:8
  • +Mal 3:10

2 Mambo ya Nyakati 31:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “vyumba vya kukulia chakula.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ne 10:38, 39; 12:44

2 Mambo ya Nyakati 31:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “zaka.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 27:30; Kum 14:28

2 Mambo ya Nyakati 31:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 26:17, 19
  • +Kum 12:5, 6; 16:10
  • +Hes 18:8
  • +Law. 2:10; 7:1

2 Mambo ya Nyakati 31:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 21:19
  • +1Nya 24:1

2 Mambo ya Nyakati 31:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 24:4
  • +Hes 4:2, 3; 8:24; 1Nya 23:24
  • +1Nya 23:6

2 Mambo ya Nyakati 31:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 25:33, 34; Hes 35:2; Yosh. 21:13

2 Mambo ya Nyakati 31:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 29:35

Maandiko ingine

2 Nya. 31:1Kut 23:24
2 Nya. 31:1Kum 7:5; 2 Fal. 18:1, 4; 2Nya 14:2, 3; 34:1, 3
2 Nya. 31:1Kum 12:2
2 Nya. 31:12Nya 23:16, 17
2 Nya. 31:12Nya 30:1, 18
2 Nya. 31:21Nya 24:1
2 Nya. 31:21Nya 23:6
2 Nya. 31:22Nya 8:14
2 Nya. 31:21Nya 23:13, 27-30
2 Nya. 31:32Nya 30:24
2 Nya. 31:3Kut 29:39
2 Nya. 31:3Hes 28:9
2 Nya. 31:3Hes 10:10
2 Nya. 31:3Kum 16:16
2 Nya. 31:4Hes 18:21; Ne 10:38, 39
2 Nya. 31:5Hes 18:12
2 Nya. 31:5Kut 22:29; 23:19; Ne 10:37
2 Nya. 31:5Mez. 3:9
2 Nya. 31:6Law. 27:30; Kum 14:28
2 Nya. 31:7Law. 23:16
2 Nya. 31:7Law. 23:24
2 Nya. 31:10Hes 18:8
2 Nya. 31:10Mal 3:10
2 Nya. 31:11Ne 10:38, 39; 12:44
2 Nya. 31:12Law. 27:30; Kum 14:28
2 Nya. 31:141Nya 26:17, 19
2 Nya. 31:14Kum 12:5, 6; 16:10
2 Nya. 31:14Hes 18:8
2 Nya. 31:14Law. 2:10; 7:1
2 Nya. 31:15Yosh. 21:19
2 Nya. 31:151Nya 24:1
2 Nya. 31:171Nya 24:4
2 Nya. 31:17Hes 4:2, 3; 8:24; 1Nya 23:24
2 Nya. 31:171Nya 23:6
2 Nya. 31:19Law. 25:33, 34; Hes 35:2; Yosh. 21:13
2 Nya. 31:212Nya 29:35
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
2 Mambo ya Nyakati 31:1-21

Cha Pili cha Mambo ya Nyakati

31 Wakati tu walikuwa wamemaliza mambo hayo yote, Waisraeli wote wenye walikuwa pale wakaenda katika miji ya Yuda, na wakavunja-vunja nguzo takatifu,+ wakakata miti mitakatifu,*+ na kubomoa mahali pa juu+ na mazabahu+ katika Yuda yote na Benyamini, na pia katika Efraimu na Manase,+ mupaka wakati walikuwa wameviharibu kabisa, kisha Waisraeli wote wakarudia katika miji yao, kila mumoja mahali pake mwenyewe.

2 Kisha Hezekia akaweka makuhani katika vikundi vyao+ na Walawi katika vikundi vyao,+ kila mumoja kati ya makuhani na Walawi kwa ajili ya utumishi wao,+ kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa na zabihu za ushirika, ili kufanya utumishi na kutoa shukrani na sifa katika milango mikubwa ya viwanja vya* Yehova.+ 3 Fungu moja la mali za mufalme mwenyewe lilitolewa kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa,+ kutia ndani matoleo ya asubui na mangaribi,+ na pia matoleo ya kuteketezwa kwa ajili ya Sabato,+ miezi mipya,+ na sikukuu mbalimbali,+ kulingana na mambo yenye yameandikwa katika Sheria ya Yehova.

4 Zaidi ya hayo, aliamuru watu wenye kuishi katika Yerusalemu watoe fungu lenye makuhani na Walawi walipaswa kupewa,+ ili washike kabisa* sheria ya Yehova. 5 Wakati tu agizo hilo lilitolewa, Waisraeli walitoa kwa wingi matunda ya kwanza ya nafaka, divai mupya, mafuta,+ na asali, na mazao yote ya shamba;+ walileta kwa wingi sehemu moja ya kumi (1/10) ya kila kitu.+ 6 Na watu wa Israeli na wa Yuda wenye walikuwa wanaishi katika miji ya Yuda walileta pia sehemu moja ya kumi (1/10) ya ngombe na kondoo na sehemu moja ya kumi ya vitu vitakatifu+ vyenye vilitakaswa kwa Yehova Mungu wao. Walivileta na kuvipanga katika marundo mengi. 7 Katika mwezi wa tatu (3),+ walianza kupanga michango yao katika marundo; na katika mwezi wa saba (7)+ wakamaliza. 8 Wakati Hezekia na wakubwa walikuja na kuona marundo hayo, walimusifu Yehova na kubariki watu wake Israeli.

9 Hezekia akauliza makuhani na Walawi juu ya marundo hayo, 10 na Azaria mukubwa wa makuhani wa nyumba ya Sadoki akamuambia: “Tangu wakati walianza kuleta michango ndani ya nyumba ya Yehova,+ watu wamekuwa wanakula na kushiba na kungali kiasi kikubwa cha ziada, kwa maana Yehova amebariki watu wake, na kiasi hiki kikubwa sana kimebakia.”+

11 Halafu Hezekia akawaambia watayarishe vyumba vya kuwekea vitu*+ katika nyumba ya Yehova, basi wakavitayarisha. 12 Waliendelea kuleta kwa uaminifu michango, zile sehemu moja za kumi (1/10),*+ na vitu vitakatifu; Konania Mulawi aliwekwa kuwa musimamizi wa vitu hivyo vyote, na Shimei ndugu yake alikuwa wa pili. 13 Yehieli, Azazia, Nahati, Asaheli, Yerimoti, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahati, na Benaya walikuwa wajumbe wenye walisaidia Konania na Shimei ndugu yake, kwa agizo la Mufalme Hezekia, na Azaria alikuwa musimamizi wa nyumba ya Mungu wa kweli. 14 Na Kore mwana wa Imna, Mulawi mwenye alikuwa mulinzi wa mulango mukubwa upande wa mashariki,+ alisimamia matoleo ya kujipendea+ ya Mungu wa kweli, na aligawa muchango wenye ulitolewa kwa ajili ya Yehova+ na pia vitu vitakatifu zaidi.+ 15 Na chini ya uongozi wake kulikuwa Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria, na Shekania, katika miji ya makuhani,+ katika vyeo vyao vyenye kutumainika, ili kugawia ndugu zao sawasawa katika vikundi,+ wakubwa na wadogo sawasawa. 16 Hilo lilikuwa kwa kuongezea ugawaji wenye ulikuwa unafanywa kwa ajili ya wanaume wa miaka tatu (3) na zaidi wenye waliandikishwa katika maandikisho kulingana na ukoo, wenye walikuja kila siku kutumika katika nyumba ya Yehova na kutimiza madaraka ya vikundi vyao.

17 Maandikisho ya makuhani kulingana na ukoo yalifanywa kulingana na jamaa yao ya upande wa baba,+ kama vile yale ya Walawi wenye walikuwa na miaka makumi mbili (20) na zaidi,+ kulingana na madaraka ya vikundi vyao.+ 18 Maandikisho kulingana na ukoo yalitia ndani watoto wao wote, bibi zao, watoto wao wanaume, na watoto wao wanamuke, kutaniko lao lote⁠—​kwa maana walijilinda wakiwa wenye kutakaswa kwa ajili ya mambo matakatifu kwa sababu ya vyeo vyao vyenye kutumainika⁠— 19 na pia wazao wa Haruni, makuhani wenye walikuwa wanaishi katika maeneo ya mashamba ya malisho yenye yalizunguka miji yao.+ Katika miji yote, wanaume walikuwa wametajwa kwa majina ili kupatia mafungu kila mwanaume kati ya makuhani na kila mutu mwenye kuwa katika maandikisho ya Walawi kulingana na ukoo.

20 Hezekia alifanya mambo hayo katika Yuda yote, na aliendelea kufanya mambo ya muzuri na yenye kuwa sawa na ya uaminifu mbele ya Yehova Mungu wake. 21 Na kila kazi yenye alifanya ili kumutafuta Mungu wake, ikuwe kuhusiana na utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli+ ao katika Sheria na amri, aliifanya kwa moyo wote, na alipata matokeo ya muzuri.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine