Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 4
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Anaonyesha namna muji wa Yerusalemu utazungukwa kwa ajili ya vita (1-17)

        • Anabeba hatia kwa siku mia tatu makumi kenda na siku makumi ine (4-7)

Ezekieli 4:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 24:11; Yer 39:1
  • +2 Fal. 25:1
  • +Yer 6:6; 32:24
  • +Eze 21:22

Ezekieli 4:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 12:6; 24:24

Ezekieli 4:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “yake,” ni kusema, upande wa kushoto wa Ezekieli.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 17:21

Ezekieli 4:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 14:34; 1 Fal. 12:19, 20

Ezekieli 4:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 23:27

Ezekieli 4:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 52:4

Ezekieli 4:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 4:5

Ezekieli 4:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Karibu grame 230 (aunsi troi 7.3). Angalia Nyongeza B14.

Ezekieli 4:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Karibu Litre 0.6 (painti 1.3). Angalia Nyongeza B14.

Ezekieli 4:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ho 9:3

Ezekieli 4:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi yangu haijachafuliwa.”

  • *

    Ao “mubaya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 22:31; Law. 7:24; 11:40
  • +Kum 14:3; Isa 65:4; 66:17

Ezekieli 4:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nitavunja fimbo za mikate.” Inawezekana ni fimbo zenye zilikuwa zinatumiwa ili kuwekea mikate.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 26:26; Isa 3:1; Eze 5:16
  • +2 Fal. 25:3; Yer 37:21; Omb 1:11; 4:9; 5:9, 10
  • +Eze 12:18

Maandiko ingine

Eze. 4:22 Fal. 24:11; Yer 39:1
Eze. 4:22 Fal. 25:1
Eze. 4:2Yer 6:6; 32:24
Eze. 4:2Eze 21:22
Eze. 4:3Eze 12:6; 24:24
Eze. 4:42 Fal. 17:21
Eze. 4:5Hes 14:34; 1 Fal. 12:19, 20
Eze. 4:62 Fal. 23:27
Eze. 4:7Yer 52:4
Eze. 4:9Eze 4:5
Eze. 4:13Ho 9:3
Eze. 4:14Kut 22:31; Law. 7:24; 11:40
Eze. 4:14Kum 14:3; Isa 65:4; 66:17
Eze. 4:16Law. 26:26; Isa 3:1; Eze 5:16
Eze. 4:162 Fal. 25:3; Yer 37:21; Omb 1:11; 4:9; 5:9, 10
Eze. 4:16Eze 12:18
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 4:1-17

Ezekieli

4 “Na wewe, mwana wa binadamu, kamata tofali na ulitie mbele yako. Uchonge muji juu yake​—⁠Yerusalemu. 2 Uuzunguke kwa ajili ya vita+ na ujenge ukuta wa kuuzunguka kwa ajili ya vita,+ usimamishe boma la kuuzunguka kwa ajili ya vita,+ jenga kambi ili kuushambulia, na uzungushe juu yake vyombo vya kubomolea.+ 3 Kamata kikaangio cha chuma, na ukiweke kuwa ukuta wa chuma katikati yako na muji huo. Kisha ukaze uso wako juu ya muji, nao utazungukwa kwa ajili ya vita; na wewe utauzunguka kwa ajili ya vita. Hiyo ni alama kwa nyumba ya Israeli.+

4 “Kisha ulalie upande wako wa kushoto na utie hatia ya nyumba ya Israeli juu yako.*+ Utabeba hatia yao kwa hesabu ya siku zenye utalalia upande wako. 5 Na nitaweka juu yako siku mia tatu makumi kenda (390), zenye kulingana na miaka ya hatia yao,+ na wewe utabeba hatia ya nyumba ya Israeli. 6 Na unapaswa kuzitimiza.

“Kisha kwa mara ya pili utalala chini, kwenye upande wako wa kuume, na utabeba hatia ya nyumba ya Yuda+ kwa siku makumi ine (40). Nimekupatia wewe siku moja kwa ajili ya mwaka moja, siku moja kwa ajili ya mwaka moja. 7 Na utageuzia uso wako kuelekea kuzungukwa kwa Yerusalemu kwa ajili ya vita+ mukono wako ukiwa wazi, na unapaswa kutoa unabii juu yake.

8 “Angalia! Nitakufunga kwa kamba ili usigeuke kutoka upande wako mumoja kuenda upande wako mwingine mupaka utakuwa umetimiza siku za kuzunguka kwako kwa ajili ya vita.

9 “Na utakamata ngano, shayiri, maharagi ya munene-munene, dengu, mutama, na ngano ya kusemeti na uvitie katika chombo kimoja na uvifanye kuwa mukate kwa ajili yako. Kwa hesabu ya siku zenye unalalia upande wako, siku mia tatu makumi kenda (390), utaukula.+ 10 Utapima na kula shekeli makumi mbili (20)* za chakula kwa siku. Utakikula kwa nyakati zenye zimewekwa.

11 “Na utakunywa maji kwa kipimo, sehemu moja ya sita (1/6) ya hini.* Utayakunywa kwa nyakati zenye zimewekwa.

12 “Na utakikula kama vile ungekula mukate wa muviringo wa shayiri; na utaupika mbele ya macho yao, kwa kutumia mavi ya wanadamu yenye kukauka kuwa kuni.” 13 Yehova akaendelea kusema: “Ni vile Waisraeli watakula mukate wao​—⁠wenye hauko safi​—⁠kati ya mataifa kwenye nitawasambaza.”+

14 Basi nikasema: “Isikuwe vile, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova! Tangu ujana wangu mupaka sasa, sijachafuliwa* kwa kula nyama ya munyama mwenye amepatikana amekufa wala munyama mwenye amepasuliwa,+ na nyama chafu* haijaingia katika kinywa changu.”+

15 Kwa hiyo akaniambia: “Sawa, nitakuruhusu utumie mavi ya ngombe pa nafasi ya mavi ya wanadamu, na utapika mukate wako juu yake.” 16 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, angalia, nitaondoa akiba ya chakula* katika Yerusalemu,+ na kwa wasiwasi mwingi watakula kipimo chao cha mukate kwa kupima,+ na kwa woga mukubwa watakunywa kipimo chao cha maji kwa kupima.+ 17 Hilo litatukia ili wakose mukate na maji, nao waangaliane kwa mushituko na waharibike kabisa kwa sababu ya kosa lao.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine