Wimbo wa Sulemani
3 “Usiku nikiwa kwenye kitanda changu,
Nilitafuta ule mwenye ninapenda.+
Nilimutafuta, lakini sikumupata.+
2 Nitaamuka na kuzunguka katika muji;
Katika barabara na katika viwanja vya watu wote,
Acha nitafute ule mwenye ninapenda.*
Nilimutafuta, lakini sikumupata.
3 Walinzi wenye walikuwa wanazunguka katika muji walikutana na mimi.+
‘Mumeona ule mwenye ninapenda?’*
4 Kisha tu kuwapita
Nilipata ule mwenye ninapenda.*
Nikamushika, sikupenda kumuacha aende,
Mupaka wakati nilimuingiza katika nyumba ya mama yangu,+
Katika chumba cha ndani cha mwenye alibeba mimba yangu.
5 Ninawaapisha, Enyi mabinti wa Yerusalemu,
Kwa swala na paa wa pori:
Musijaribu kuamusha ao kuchochea upendo ndani yangu mupaka wakati huo wenyewe utataka.”+
6 “Ni kitu gani hiki chenye kupanda kutoka katika jangwa kama nguzo za moshi,
Chenye marashi ya manemane na ubani,
7 “Muangalie! Ni kitanda cha Sulemani.
Wanaume wenye nguvu makumi sita (60) wanakizunguka,
Kutoka kati ya wanaume wenye nguvu wa Israeli,+
8 Kila mumoja wao iko* na upanga,
Wote wamezoezwa kupigana vita,
Kila mumoja iko* na upanga kwenye upande wake
Ili kujilinda na mambo yenye kuogopesha sana ya usiku.”
10 Alitengeneza nguzo zake kwa feza,
Viegemeo vyake kwa zahabu.
Kiti chake ni cha manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau
Sehemu yake ya ndani ilipambwa kwa upendo
Na mabinti wa Yerusalemu.”